Friday, April 21, 2017

SINTOFAHAM YAIBUKA TENA MGOGORO WA KUGOMBEA ENEO LA MADINI CHANGAA

IMG-20160309-WA0084-1024x576
Na Mahmoud Ahmad Kondoa
Sintofahamu imeibuka upya katika mgogoro wa Kikundi cha wachimbaji wadogo wa madini na kampuni ya Kidee Minning (T) Ltd katika eneo la Kata ya Changaa baada ya viongozi na watendaji wa serikali kudai hawana taarifa za uwepo wa kikundi hicho.
Kadhia hiyo imeibuka baada ya kuwepo malalamiko ya kuvamiwa kwa kikundi kinachoendesha shughuli za utafiti na uchimbaji wa madini,utunzaji wa mazingira,ufugaji wa
nyuki na ujasiriamali na kutambuliwa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kondoa.
Aidha ofisi ya Kitongoji cha changaa iliyobariki kupitia ofisi ya kata kupata hati ya utambuzi wa kikundi imeonekana viongozi wa kata na kitongoji kukanusha vikali mbele ya halmashauri ya wilaya ya kondoa kuwa hawakitambui kikundi cha Kumucha wakati mkurugenzi anakitambua na kutoa hati ya kikundi hicho june mwaka 2015.
Hata hivyo uongozi huo wa kata na kitongoji wametoa muhtasari halali kupitia mkutano mkuu wa kijiji kwa wakati huo na kikundi kubarikiwa kuendelea na kupata ridhaa ili kupata hati ya utambuzi wa kikundi hicho kupitia ofisi ya mkurugenzi wa halmashari ya Kondoa.
Akizungumza na mwanahabari hii diwani Issa Bou na Mwenyekiti wa kitongoji Kenyeta Fonda wamenukuliwa wakikitambua kikundi hicho lakini kwenye mamlaka husika wakikikataa ambapo diwani huyo ni mlezi wa kikundi hicho.
Dodoso za wanahabari hii zimeenda mbali baada ya kubaini kuwepo kwa ukiukwaji na matumizi mabaya ya ofisi za serikali kupitia viongozi hao kwa kutumia serikali ya kijiji kupitisha masuala mbali mbali yenye manufaa bila kuwashirikisha wananchi na kutoa maamuzi binafsi.
Mfano wa suala la utunzaji wa mazingira, serikali ya kijiji imewahukumu mmoja ya wanakikundi aliyenunua miche ya miti na kwenda kuipanda kwenye eneo lililoharibiwa kwa ukatwaji wa miti na kuchoma mkaa na kumuhuku kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya tsh.200,000
Aidha ndipo alipoamua  kuilipa serikali ya kijiji hicho faini hiyo bila kupewa stakabadhi ya ofisi ambapo alifuatilia kupewa risiti hadi leo bila mafanikio na ndipo ilipojitokeza hali ya kutaka kumridhisha kwa kumruhusu kuendelea na kusudio lake la upandaji wa miti ambapo awali walingoa miche aliopanda kwa madai ya kuwa eneo hilo si mali yake ni mali ya kijiji.
Nae Mwenyekiti wa Kumucha Donmillan Shirima amesema kuwa kumekuwapo na sintofahamu hiyo ambapo juzi mwekezaji amefyeka miti na kuharibu mazingira bila taarifa ambapo serikali ya mtaa wa tumbelo na kitongoji Changaa wakitupiana mpira katika suala hilo juu ya nani mhusika wa eneo hilo.
Amesema kuwa suala hilo lipo kwenye mamlaka husika ambapo serikali ya wilaya inalifanyiakazi na wao kwa sasa hawana la kuzungumza wanasubiria majibu ya msingi ya malalamiko yao ya uvamizi wa eneo lao,
Shirima amesema kuwa mamlaka husika na vijiji zimekuwa zikiwataka kukaa mezani na mwekezaji wakati wao wanahitaji tafsiri ya utambuzi wao na uhalali wa uwepo wa kisheria katika eneo hilo.

No comments :

Post a Comment