Dkt. Lorah Madete, Kaimu Naibu
Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla, Tume ya Mipango (aliyesimama),
akitoa neno kwa washiriki wa mafunzo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi
ili afungue mafunzo hayo ya siku tano. Waliokaa ni Bw. Maduka Paul
Kessy, Kaimu Katibu Mtendaji, Tume ya Mipango (katikati) na Bw. John
Mduma, Mhadhiri Mwanamizi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mgeni Rasmi Bw. Maduka Paul
Kessy, Kaimu Katibu Mtendaji, Tume ya Mipango (aliyesimama) akitoa
hotuba ya ufunguzi wa mafunzo kuhusu Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji
wa Umma kwa washiriki kutoka Idara za Sera na Mipango za Wizara, Idara
zinazojitegemea na Wakala za Serikali. Wengine ni Bi. Lorah Madete,
Kaimu Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla, Tume ya Mipango
(kulia) na Bw. John Mduma, Mhadhiri Mwandamizi, Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (kushoto).
Washiriki wa Mafunzo wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada zilizotolewa.
Dkt. John Mduma, Mhadhiri
Mwandamizi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (aliyesimama), akitoa neno kwa
washiriki wa mafunzo mara baada ya mafunzo hayo kufunguliwa rasmi.
Washiriki wa mafunzo kuhusu
Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma kutoka Idara za Sera na
Mipango za Wizara, Idara zinazojitegemea na Wakala za Serikali pamoja na
wawezeshaji wa mafunzo wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi
mara baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo.
…………………………………………………………………………….
Na Thomas Nyindo.
Maofisa wa Idara za Sera na
Mipango kutoka Wizara, Idara na Wakala za Serikali wametakiwa kuongeza
ufanisi na ubunifu katika kuandaa na kusimamia miradi ya maendeleo
ili
kuharakisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025.
Kauli hiyo imetolewa leo na
Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bw. Maduka Kessy wakati
akifungua mafunzo ya Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma
yanayoendelea katika ukumbi wa Chuo cha Mipango Dodoma.
Kessy alieleza kuwa mafunzo hayo
yanalenga kuwajengea uwezo maofisa wanaosimamia masuala ya Sera na
Mipango katika kuibua na kutekeleza miradi ya maendeleo, hususan, ile
inayogharamiwa kwa fedha za Serikali ili kufanya Tanzania kuingia kwenye
nchi za kipato cha kati kama ilivyoaninishwa kwenye Dira ya Taifa ya
Maendeleo.
“Mipango ya maendeleo
tunayojiwekea, kama taifa, inapaswa kutafsiriwa katika miradi na
programu za utekelezaji, hivyo mafunzo haya yatatusaidia kuongeza
ufanisi, ubunifu na uwajibikaji katika kuandaa miradi na kusimamia
miradi yenye tija kwa wananchi,” alisema Kessy.
Aliwasisitiza washiriki wa
mafunzo hayo kuwa wao ni miongoni mwa wadau muhimu katika kuifanya
Tanzania ipige hatua za maendeleo kwa kuwa ndio wanaohusika katika
kupanga na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Aidha, Kessy alieleza kuwa
mafunzo hayo yatawasaidia washiriki kuongeza ufanisi na ubunifu katika
kuchagua miradi, kutafuta fedha za ugharamiaji na kuboresha uratibu wa
kufungamanisha uwekezaji wa umma kwa kubainisha hatua za kufuata katika
kujumuisha miradi ya maendeleo katika bajeti za maendeleo.
“Mwongozo huu utawasaidia kufanya
maamuzi katika kuchagua miradi sahihi ya uwekezaji katika sekta ya umma
na kuhakikisha ufanisi katika utekelezaji wake. Sote tunafahamu kuwa
azma yetu ya maendeleo kitaifa ni kufikia uchumi wa kipato cha kati
ifikapo 2025,” alisema.
Kaimu Katibu Mtendaji huyo
alieleza kuwa zipo changamoto zinazokabili usimamizi wa miradi ya
maendeleo, kuanzia hatua ya kubuni, kutekeleza hadi kukamilisha miradi
hiyo. Kwa hiyo Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji waRasilimali za Umma
ni mojawapo ya maandiko muhimu ambayo yamebuniwa kukabiliana na
changamoto hizo.
No comments :
Post a Comment