Madaktari bingwa wa upasuaji wa
magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa
kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Saifee ya nchini India
wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa moyo . Katika ziara aliyoifanya nchini
mwishoni mwaka jana kiongozi Mkuu wa Madheebu ya Bohora Duniani
Mtakatifu Dkt. Syedna Aliqadr Mufaddal Saifuddin alimuahidi Mheshimiwa
Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuleta madaktari wa Moyo nchini ambao
watashirikiana na Madaktari wa JKCI kufanya upasuaji kwa wagonjwa. Timu
ya wataalam hao ambao idadi yao ni sita imeshawasili nchini na tayari
wameanza kufanya upasuaji ambao utachukuwa siku tano na wanatarajia
kufanya upasuaji wa kuvuna mishipa ya damu mguuni na kuipandikiza katika
mishipa ya moyo iliyoziba ( CABG-Coronary Artery Bypass Graft) na
upasuaji wa milango miwili hadi mitatu ya moyo ambayo inamatatizo na
inahitaji kubadilishwa kwa wagonjwa 15.
Daktari bingwa wa upasuaji wa
magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Evarist
Nyawawa (kushoto) kwa kushirikiana na mwenzake wa Hospitali ya Saifee ya
nchini India Ali Oscar Behranwala wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa moyo .
Katika ziara aliyoifanya nchini mwishoni mwa mwaka jana kiongozi Mkuu
wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtakatifu Dkt. Syedna Aliqadr Mufaddal
Saifuddin alimuahidi Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuleta
madaktari wa Moyo nchini ambao watashirikiana na Madaktari wa JKCI
kufanya upasuaji kwa wagonjwa. Timu ya wataalam hao ambao idadi yao ni
sita imeshawasili nchini na tayari wameanza kufanya upasuaji ambao
utachukuwa siku tano na wanatarajia kufanya upasuaji wa kuvuna mishipa
ya damu mguuni na kuipandikiza katika mishipa ya moyo iliyoziba (
CABG-Coronary Artery Bypass Graft) na upasuaji wa milango miwili hadi
mitatu ya moyo ambayo inamatatizo na inahitaji kubadilishwa kwa wagonjwa
15.
Madaktari bingwa wa upasuaji wa
magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa
kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Saifee ya nchini India
wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa milango ya moyo ambayo inamatatizo na
kuweka milango mingine.
No comments :
Post a Comment