Saturday, March 25, 2017

KUSITISHWA KWA MNADA KUTOKANA NA MALIPO YALIYOFANYIKA KWA VIWANJA VILIVYOKUWA NA MADENI SUGU YA KODI YA PANGO LA ARDHI.


tanzania
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na Kampuni ya udalali ya Msolopa inatoa taarifu kwa wananchi wote kuwa zoezi la mnada lililotarajiwa kufanyika Jumapili – tarehe 26/03/2017  halitafanyika tena kwa sababu wadaiwa wote wa viwanja vilivyokuwa vinadiwe kutokana na kuwa na madeni sugu ya kodi ya pango la ardhi, wametimiza masharti ya malipo kabla ya siku ya mnada kufanyika.
Aidha, orodha ya viwanja vingine vya maeneo ya Kinondoni, Temeke na Ilala vyenye madeni sugu ya Kodi ya pango la ardhi itatolewa kuanzia wiki ijayo.
LIPA KODI YA PANGO LA ARDHI KWA WAKATI
Usipolipa Kodi ya Pango la Ardhi, utanyang’anywa umiliki wa Ardhi yako, kutokana na sheria ya Ardhi, Na. 4 ya mwaka 1999, katika kifungu cha 49 na 51.
Kodi ya ardhi hulipwa kila ifikapo Julai Mosi ya kila Mwaka katika Manispaa au Halmashauri husika na katika Ofisi za Malipo ya Kodi – Dar es Salaam
Imetolewa na:
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

No comments :

Post a Comment