Friday, March 24, 2017

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI MALIASILI NA MAZINGIRA YATEMBELEA UJENZI WA UKUTA WA OCEAN RAOD


MAZ1
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Mazingira Mhe. Stanslaus Nyongo (Mb.) Maswa Mashariki akiongea na waandishi wa Habari baada ya ukaguzi wa ujenzi wa ukuta wa Ocear Road katika Barabara ya Baraka Obama Jijini Dar es Salaam leo.
MAZ2
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi maliasili na Mazingira wakipokea taarifa ya utekelezejai wa mradi wa mabadiliko ya tabia nchi unaohusisha ujenzi wa ukuta wa Ocean Road. Katika mkutano uliofanyika katika Ofisi ya Makamu wa Rais Jijini dare s Salaam.
MAZ3
Sehemu ya ukuta wa fukwe ya Ocean Road kama unavyooneka katika picha ukiwa katika matengenezo.
MAZ4
Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais  Bw. Richard Muyungi akiwasilisha taarifa utekelezaji wa ujenzi wa ukuta wa fukwe ya Ocean Road kwa wajumbe wa kamati ya Bunge ya Ardhi malisili na Mazingira. (Picha na Evelyn Mkokoi wa OMR)
………………………………………………………………………………….
Evelyn Mkokoi – Dar es Salaam
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Mazingira, imetembelea mradi wa ujenzi wa ukuta wa fukwe ya Ocean Road katika Barabara ya Barak Obama Jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kukagua  mradi wa Mabadiliko ya Tabia nchi, unaoratibiwa na  Ofisi ya Makamu wa Rais.
Akiongea na waandishi wa Habari katika eneo la ujenzi wa ukuta huo, kaimu mwenyekiti wa
  kamati hiyo Mhe. Stanslaus Nyongo (MB) Maswa Mashariki alisema kuwa kuwa, kamati inaishauri serikali kutumia vizuri  mahusiano ya nchi yetu na wahisani ili kuweza kupata pesa za kusaidia suala zima la kuhimili na kukabiliana na mbadiliko ya tabianchi.
Aidha, Mhe. Nyogo aliongeza kwa kusema kuwa Serikali nayo iongeze jitihada za kupambana na  kukabiliana na athari na hasara zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi kwa kutoa elimu ya kulinda mazingira kwa umma.
Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo Mhe Dk. Rafael Chegeni, alisema kuwa uharibifu wa mazingira utokanao na ukataji miti ovyo kwa matumizi ya nishati ya mkaa ni mkubwa na ndiyo unaopelekea athari kubwa za mabadiliko ya tabia nchi, na nishati mbadala bado zinapatikana kwa gaharama za juu, na kushauri kuwa kuwe na mikakati kwa serikali na sekta husika ya kumsaidia mwanachi wa kawada kutunza mazingira aidha, kuwe na mkakati unaonekana  na kusadia kuwa na upatikani wa haraka wa nishati mbadala.
Baada ya wajumbe wa kamati hiyo kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kwa upande wa Dar es Salaam na  Pwani, Mhe Hawa Mwaifunga alitaka kufahamu kuhusu mradi wa majiko banifu, utekelezaji wake na ugawaji wa majiko hayo kwani athari za mabadiliko ya tabia nchi yapo nchi nchi nzima.
Awali akiwasilisha ripoti ya utelelezaji wa mradi wa mabadiliko ya tabia nchi unaohusisha ujenzi wa ukuta wa ocean road, urejeshaji wa upandaji wa mikoko katika maeneo ya mbweni, daraja la salenda, ununio na ujenzi wa mitaro katika maeneo ya ilala Bungoni kata ya Buguruni, maeneo ya Mtoni katika Wilaya ya Temeke na katika maeneo ya chuo cha Mwalimu Nyerere KIgamboni, Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi , alisema kuwa takribani kiasi cha dola milioni 500 zinahitajika kila mwaka nchini kwa ajili ya utekelezaji wa kazi hiyo ikiwa ni pamoja na kusaidia mafunzo kwa wananchi katika ngazi za familia ili kuweza kukabilianda na janga hili la mabadiliko ya tabia nchi. Aliongeza kwa kusema kuwa ujenzi huo wa ukuta wa ocean road utahusisha pia ujenzi wa njia za waendao kwa miguu, viti vya kumpuzikia, na taa.
Mradi wa ujenzi wa ukuta wa Ocean Rpoad unaoendelea kujengwa, umekalimika kwa asilimia 30% yenye urefu wa mita 820, kwa pande nyingine kwenda juu kwa urefu wa mita 2.5, na pande nyingine kwenda juu kwa urefu wa mita 4.
Mradi huo huo unafadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) , na kusimamiwa na shirika lingine la umoja wa maitaifa la Huduma kwa Miradi, (UNOPS) ambalo linasimamia miradi yote ya mabadiliko ya tabia nchi duniani. Mradi huo upo chini ya Uratibu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira. Na ujenzi huo wa ukuta unafanywa na kampuni ya Dezo Civil Constractions ya jijjini Dar es Salaam

No comments :

Post a Comment