Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya
kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Mazingira Mhe. Stanslaus Nyongo
(Mb.) Maswa Mashariki akiongea na waandishi wa Habari baada ya ukaguzi
wa ujenzi wa ukuta wa Ocear Road katika Barabara ya Baraka Obama Jijini
Dar es Salaam leo.
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Ardhi maliasili na Mazingira wakipokea taarifa ya
utekelezejai wa mradi wa mabadiliko ya tabia nchi unaohusisha ujenzi wa
ukuta wa Ocean Road. Katika mkutano uliofanyika katika Ofisi ya Makamu
wa Rais Jijini dare s Salaam.
Sehemu ya ukuta wa fukwe ya Ocean Road kama unavyooneka katika picha ukiwa katika matengenezo.
Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira
kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi akiwasilisha taarifa
utekelezaji wa ujenzi wa ukuta wa fukwe ya Ocean Road kwa wajumbe wa
kamati ya Bunge ya Ardhi malisili na Mazingira. (Picha na Evelyn Mkokoi
wa OMR)
………………………………………………………………………………….
Evelyn Mkokoi – Dar es Salaam
Kamati ya kudumu ya Bunge ya
Ardhi Maliasili na Mazingira, imetembelea mradi wa ujenzi wa ukuta wa
fukwe ya Ocean Road katika Barabara ya Barak Obama Jijini Dar es Salaam,
kwa lengo la kukagua mradi wa Mabadiliko ya Tabia nchi, unaoratibiwa
na Ofisi ya Makamu wa Rais.
Akiongea na waandishi wa Habari
katika eneo la ujenzi wa ukuta huo, kaimu mwenyekiti wa
kamati hiyo
Mhe. Stanslaus Nyongo (MB) Maswa Mashariki alisema kuwa kuwa, kamati
inaishauri serikali kutumia vizuri mahusiano ya nchi yetu na wahisani
ili kuweza kupata pesa za kusaidia suala zima la kuhimili na kukabiliana
na mbadiliko ya tabianchi.
Aidha, Mhe. Nyogo aliongeza kwa
kusema kuwa Serikali nayo iongeze jitihada za kupambana na kukabiliana
na athari na hasara zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi kwa kutoa
elimu ya kulinda mazingira kwa umma.
Kwa upande wake mjumbe wa kamati
hiyo Mhe Dk. Rafael Chegeni, alisema kuwa uharibifu wa mazingira
utokanao na ukataji miti ovyo kwa matumizi ya nishati ya mkaa ni mkubwa
na ndiyo unaopelekea athari kubwa za mabadiliko ya tabia nchi, na
nishati mbadala bado zinapatikana kwa gaharama za juu, na kushauri kuwa
kuwe na mikakati kwa serikali na sekta husika ya kumsaidia mwanachi wa
kawada kutunza mazingira aidha, kuwe na mkakati unaonekana na kusadia
kuwa na upatikani wa haraka wa nishati mbadala.
Baada ya wajumbe wa kamati hiyo
kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kwa upande wa Dar es Salaam
na Pwani, Mhe Hawa Mwaifunga alitaka kufahamu kuhusu mradi wa majiko
banifu, utekelezaji wake na ugawaji wa majiko hayo kwani athari za
mabadiliko ya tabia nchi yapo nchi nchi nzima.
Awali akiwasilisha ripoti ya
utelelezaji wa mradi wa mabadiliko ya tabia nchi unaohusisha ujenzi wa
ukuta wa ocean road, urejeshaji wa upandaji wa mikoko katika maeneo ya
mbweni, daraja la salenda, ununio na ujenzi wa mitaro katika maeneo ya
ilala Bungoni kata ya Buguruni, maeneo ya Mtoni katika Wilaya ya Temeke
na katika maeneo ya chuo cha Mwalimu Nyerere KIgamboni, Mkurugenzi wa
Idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi ,
alisema kuwa takribani kiasi cha dola milioni 500 zinahitajika kila
mwaka nchini kwa ajili ya utekelezaji wa kazi hiyo ikiwa ni pamoja na
kusaidia mafunzo kwa wananchi katika ngazi za familia ili kuweza
kukabilianda na janga hili la mabadiliko ya tabia nchi. Aliongeza kwa
kusema kuwa ujenzi huo wa ukuta wa ocean road utahusisha pia ujenzi wa
njia za waendao kwa miguu, viti vya kumpuzikia, na taa.
Mradi wa ujenzi wa ukuta wa Ocean
Rpoad unaoendelea kujengwa, umekalimika kwa asilimia 30% yenye urefu wa
mita 820, kwa pande nyingine kwenda juu kwa urefu wa mita 2.5, na pande
nyingine kwenda juu kwa urefu wa mita 4.
Mradi huo huo unafadhiliwa na
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) , na kusimamiwa na
shirika lingine la umoja wa maitaifa la Huduma kwa Miradi, (UNOPS)
ambalo linasimamia miradi yote ya mabadiliko ya tabia nchi duniani.
Mradi huo upo chini ya Uratibu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira. Na
ujenzi huo wa ukuta unafanywa na kampuni ya Dezo Civil Constractions ya
jijjini Dar es Salaam
No comments :
Post a Comment