Mradi
wa Kuwawezesha wanawake Kiuchumi Kupitia Tasnia ya urembo ujulikanao
kama Manjano Dream-Makers ulioasisiwa na Taasisi ya Manjano Foundation
wataendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa wanawake wa Mkoa wa Mtwara
kuanzia Jumatatu, tarehe 27 March 2017 kwenye ukumbi wa SIDO Mkoani
Mtwara. Mafunzo hayo yatatolewa kwa jumla ya wanawake watakaochaguliwa
30 kutoka mkoani Mtwara.
Baada
ya mafunzo hayo wanaweke hao watakuwa chini ya uangalizi wa Taasisi
hiyo kwa lengo la kuhakikisha wanawake wa Mkoa wa Mtwara wanafikia
malengo yao waliojiwekea katika kujikita kwenye kujiajiri. Wanawake
wakazi wa Mkoa wa Mtwara waliotuma maombi kupitia tovuti ya Manjano
Foundation na wanaopenda kunufaika na mradi huo wanaombwa kujitokeza kwa
ajili ya usaili siku ya Jumamosi tarehe 25 Machi 2017 kuanzia saa tatu
(9:00AM) asubuhi kwenye ukumbi wa wa SIDO Mkoani Mtwara.
Mafunzo
yana lengo la kumsaidia mjasiriamali mwanamke kujikwamua na kujiongezea
kipato. Awamu ya kwanza ni kumfundisha maswala ya biashara namna ya
kuibua na kubuni miradi mbalimbali namna ya kuandika mpangilio wa
biashara ikiwemo matumizi sahihi ya rasilimali muda, kutokufuja fedha na
pia namna ya kujitunzia akiba itokanayo na biashara yake.
Awamu
ya pili itahusu kuwafundisha jinsi ya kupamba ma harusi na matumizi
sahihi ya vipodozi vya LuvTouch Manjano. Baada yanawake hawa kuhitimu
mafunzo haya Taasisi ya Manjano Foundation itawaunganisha na taasisi za
fedha zinazotoa mikopo bila riba waweze kupata mtaji wa kununua bidhaa
za vipodozi kwa ajili ya kuwawezesha kuanzisha biashara wakiwa chini ya
uangalizi maalum wa Taasisi hiyo kwa lengo la kuhakikisha kila mhitimu wa mafunzo haya anapiga hatua na kuweza kujitegemea.
Wasiliana nasi kwa Simu namba +255 784 661 080 au +255 714 646 322
No comments :
Post a Comment