WAPINZANI wa Zimamoto kwenye
michuano ya Kombe la Klabu Bingwa Barani Afrika timu ya Ferroviario de
Beira imeshawasili Zanzibar katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid
Amani Karume ikitokea Msumbiji na wapo tayari kwa ajili ya pambano
litakalo pigwa Jumamosi kwenye uwanja wa Amaan Saa10:00 za jioni.
Timu hiyo ya Ferroviario de
Beira ambao ni mabingwa wa ligi kuu soka ya Msumbiji, wamefikia katika
Hoteli ya Mtoni Marine iliopo Maruhubi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja
ambapo msafara wao umekuja na wachezaji 20 pamoja viongozi 7.
Kikosi hicho ambacho kina
wachezaji watano wa kigeni kilipokelewa na viongozi wa ZFA akiwemo
Makamo wa rais, Katibu mkuu na Afisa habari wa chama hicho sambamba na
viongozi wa Zimamoto.
Miongoni mwa wachezaji wageni ni
pamoja na Fabrice Sikanda kutoka Congo ambaye amesema wanaifahamu kiasi
Zimamoto na ni timu ambayo kamwe haiwezi kuwapa shida.
“Sisi tumekuja hapa Zanzibar
kuchukua point na kurudi nyumbani, Zimamoto tumeshaiona katika Kombe la
Mapinduzi kwenye TV, hivyo kichapo wanacho tu mana wanafungika vizuri
tu”. Alisema Sikanda.
No comments :
Post a Comment