Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania bara timu ya Simba imewashusha kileleni mahasimu wao
wakubwa Yanga baada ya kupata ushindi wa jumla ya magoli 3-0 dhidi ya
Tanzania Prisons mchezo uliopigwa kwenye dimba la uwanja wa Taifa jijini
Dar es salaam.
Juma Luizio alikuwa wa kwanza
kuiandika bao Simba mnamo dakika ya 18 akimalizia kazi nzuri toka kwa
beki Janvier Besala Bokungu na kumchambua milnda mlango wa Prisons na
dakika ya 28 Mshambuliaji mchachari Ibrahim Ajib alifunga la pili baada
ya kupokea pasi toka kwa Laudit Mavugo hadi mapumziko Simba walikuwa
mbele kwa magoli mawili.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu
zote kufanya mabadiliko hata hivyo Simba waliweza kunufaika na
mabadiliko hayo kwani dakika ya 67 Mrundi Laudit Mavugo alipigilia
msumari wa tatu kwa Prisons kwa krosi safi ya Ibrahim Ajib huku likiwa
goli lake la tano na akiendelea kung’ara baada ya kuendelea kufumania
nyavu mara mbili mfululizo akianza kule mkoani Ruvuma ambapo Simba
walishinda jumla ya magoli 3-0 dhidi ya Majimaji huku yeye akifunga bao
moja.
Simba wameweza kulipa kisasi hicho
baada ya mzunguko wa kwanza kufungwa jumla ya magoli 2-1 kwenye uwanja
wa Sokoine mjini Mbeya hadi mwamuzi Alex Mahaggi toka Mwanza anamaliza
Mpira Simba wameibuka na ushindi wa magoli 3-0.
Kwa matokeo hayo Simba wamefikisha
jumla ya pointi 51 na kuwaacha Yanga wakiwa na pointi 49 na wanatarajia
kukutana mnamo Februari 25 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kikosi cha Simba kilikuwa; Daniel Agyei, Janvier Bokongu,
Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Novaty Lufunga, Method Mwanjali/Mwinyi
Kazimoto dk62, James Kotei, Said Ndemla, Muzamil Yassin, Laudit Mavugo,
Ibrahim Hajib/Pastory Athanas dk74 na Juma Luizio/Shizza Kichuya dk70.
Prisons; Laurian Mpalile, Aaron Kalambo, Salum Kimenya, James Mwasote, Nurdin Chona, Jumanne Elfadhil, Lambert Sibiyanka, Kazungu Nchinjayi/Kassim Hamisi dk38, Victor Hangaya/Salum Bosco dk76, Mohammed Samatta na Benjamin Asukile/Meshack Suleiman dk56.
Prisons; Laurian Mpalile, Aaron Kalambo, Salum Kimenya, James Mwasote, Nurdin Chona, Jumanne Elfadhil, Lambert Sibiyanka, Kazungu Nchinjayi/Kassim Hamisi dk38, Victor Hangaya/Salum Bosco dk76, Mohammed Samatta na Benjamin Asukile/Meshack Suleiman dk56.
No comments :
Post a Comment