Saturday, February 11, 2017

MKURUGENZI WA FEDHA NA UTAWALA PSPTB AFUNGA MAFUNZO YA UTAFITI YA SIKU TANO YALIYOANDALIWA NA BODI HIYO


 001
 Mkurugenzi wa Fedha na Utawala (PSPTB) Bw. Paul Bilabaye akifunga mafunzo ya wanafunzi waliofikia  Level 5 wanaotarajiwa kufanya mitihani ya Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi kwa niaba ya Kaimu  Mkurugenzi Mtendaji  wa bodi hiyo Godfred Mbanyi  katika Warsha ya siku tano ya Mafunzo  ya  Utafiti iliyondaliwa na Bodi hiyo, ambapo kila mwanafunzi amepangiwa msimamizi wa utafiti wake na baadaye utafiti wao utapimwa kitaalaam na  utawawezesha kufuzu katika taaluma ya Ununuzi na Ugavi wa Umma baada ya Kupata cheti cha kitaaluma cha (CPSP)
Mafunzo hayo yalikuwa yakifanyika kwenye jengo la Taasisi ya Elimu ya watu wazima jijini Dar es salaam ambapo wanafunzi hao sasa watakwenda kufanya utafiti wao katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
0001
01
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala (PSPTB) Bw. Paul Bilabaye akimkabidhi zawadi ya kikombe mmoja wa wanafunzi Sosera Mokiri aliyeshinda bahati nasibu katika ufungaji wa mafunzo hayo Katikati  Amani Ngonyani Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo (PSPTB)
1
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala (PSPTB) Bw. Paul Bilabaye akimkabidhi zawadi ya kikombe mmoja wa wanafunzi Grace Peter  aliyeshinda bahati nasibu katika ufungaji wa mafunzo hayo, Kulia ni Shamim Mdee Afisa Mwandamizi  Mahusiano ya Umma na Masoko (PSPTB) na katikati ni Amani Ngonyani Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo (PSPTB)
3
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakipokea vyeti vyao kutoka kwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala (PSPTB) Bw. Paul Bilabaye katikati ni Amani Ngonyani Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo (PSPTB) na kushoto ni Bi. Shamim Mdee Afisa Mwandamizi  Mahusiano ya Umma na Masoko. PSPTB
4 5 6
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala (PSPTB) Bw. Paul Bilabaye katikati  akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa zawadi hizo kutoka kulia ni Grace Peter , Gastor Masawe na kushoto ni Sosera Mokiri.
07
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala (PSPTB) Bw. Paul Bilabaye katikati na Amani Ngonyani Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo (PSPTB) wakifurahia jambo wakati Bi. Shamim Mdee Afisa Mwandamizi  Mahusiano ya Umma na Masoko (PSPTB) alipokua akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo.
7
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mkurugenzi wa Fedha na Utawala (PSPTB) Bw. Paul Bilabaye.
8 9 10
Amani Ngonyani Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo (PSPTB) akitoa shukurani zake kwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala (PSPTB) mara baada ya kufunga mafunzo hayo kulia ni Bi. Shamim Mdee Afisa Mwandamizi  Mahusiano ya Umma na Masoko (PSPTB)

No comments :

Post a Comment