Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (kulia)
akisalimiana na Katibu Mkuu wa Shirika la Forodha Duniani (World Customs
Organisation-WCO) Dk. Kunio Mikuriya alipotembelea TRA ili kujadili
masuala mbalimbali na kuona maendeleo ya miradi ya Forodha
inayotekelezwa na TRA kwa ushirikiano na WCO
Katibu Mkuu wa Shirika la Forodha
Duniani (World Customs Organisation-WCO) Dk. Kunio Mikuriya (kulia)
akifurahia zawadi ya kitabu cha historia ya Tanzania ambacho Kamishna
Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata alimkabidhi kama ishara ya ukumbusho wa
ziara yake nchini Tanzania. Dk. Mikuriya alitembelea TRA ili kujadili
masuala mbalimbali na kuona maendeleo ya miradi ya Forodha
inayotekelezwa na TRA kwa ushirikiano na WCO
Katibu
Mkuu wa Shirika la Forodha Duniani (World Customs Organisation-WCO) Dk.
Kunio Mikuriya akisisitiza jambo wakati wa kikao cha pamoja na Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (kulia)
alipotembelea TRA ili kujadili masuala mbalimbali na kuona maendeleo ya
miradi ya Forodha inayotekelezwa na TRA kwa ushirikiano na WCO
Meneja Mifumo ya Kielektroniki
ya Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Tinkasimile
Felix (aliyesimama) akitoa maelezo ya jinsi Mfumo wa Forodha (TANCIS)
unavyofanya kazi kwa Katibu Mkuu wa Shirika la Forodha Duniani (World
Customs Organisation-WCO) Dk. Kunio Mikuriya (aliyeketi katikati).
Wengine ni Meneja wa Maendeleo Ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini
kutoka Shirika la Forodha Duniani Bw. Patrick Gyan (kushoto) pamoja na
Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa Bw. Jocktan Kyamuhanga (kulia).
No comments :
Post a Comment