Wednesday, February 22, 2017

Hukumu Kesi ya Kikatiba Sheria ya Makosa ya Mtandao ‘Kuzungumkuti’

Kutoka kushoto ni Wakili wa Jamii Media, Benedict Ishebakaki Alex, Mmiliki Mwenza wa Jamii Media, Mike Mushi, Mkurugenzi wa Jamii Forum, Maxence Melo pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Sikika, Irenei Kiria wakitoka Mahakamani leo walipoitwa kupokea hukumu yao.
Wakili wa Jamii Media, Benedict Ishebakaki Alex (kushoto) akiwaongoza baadhi ya viongozi Jamii Media walipokuwa wakitoka Mahakama Kuu leo.
HUKUMU ya kesi ya Kikatiba namba 9 ya mwaka 2016 iliyofunguliwa mwaka jana na Kampuni ya Jamii Media ikipinga baadhi ya vifungu vya sheria ya makosa ya mtandao kwa kile kuingilia uhuru wa maoni na kujieleza wa wananchi imeshindwa kusoma huku kukiwa hakuna sababu zilizotajwa.
Akizungumza leo eneo la Mahakama Kuu, jijini Dar es Salaam Wakili wa Jamii Media, Benedict Ishebakaki Alex alisema awali walipata wito wa mahakama kuwa hukumu ya kesi yao ilikuwa isomwe leo lakini wamefika mahakamani na kutokuta taarifa zozote za kusomwa kwa hukumu hiyo.
“..Kama mnavyojua leo tulikuwa tumekuja kwa ajili ya hukumu ya kesi yetu iliyofunguliwa toka mwaka jana mwezi wa tatu kutokana na rekodi za mahakama tuliambiwa tuje leo saa sita mchana kuja kupokea hukumu kama mnavyojua majaji ambao walikuwa wanasikiliza kesi yetu ni majaji watatu Mh. Jaji Koroso, Mh. Jaji Khalfan na Mh. Jaji Kitusi lakini tumefuatilia leo hapa pamoja na mawakili wa serikali, lakini tulikuwa tunajua jaji Koroso hayupo kuna taarifa kuwa amehamishwa…lakini tulikuwa tunajua labda kuna rekodo yoyote kuwa labda amemwachia faili nani au hukumu itasomwa lini tena…tunaona makarani wanasema hawana taarifa zozote juu ya hukumu hiyo.
Wakili huyo alisema yeye pamoja na mawakili wa Serikali wataendelea kufuatilia kujua hukumu hiyo itasoma lini ili waweze kuipokea.
Kwa upande wake Mwanaharakati wa haki ya kupata habari nchini, Simon Mkina, akizungumzia kadhia ya hukumu hiyo kutoonekana, amesema inashangaza kuona mahakama hiyohiyo iliyotoa tarehe ya kutolewa hukumu, watendaji wake wanatupiana mpira kuhusu ilipo.
Wamiliki wa mtandao wa Jamii Media na mkuregenzi wa mtandao huo Maxence Melo akizungumza na Maria Sarungi ambaye ni
mdau wa masuala ya habari nje ya Mahakama kuu jijini Dar es Salaam.

No comments :

Post a Comment