Wednesday, December 14, 2016

SERIKALI KUTOWAVUMILIA WALE WOTE WATAKAOBAINIKA KUTMIA MADARAKA YAO VIBAYA

arushaaaaaaaaaa
Na Mahmoud Ahmad Arusha
Serikali imesema kuwa haipo teyari kuwavumilia watendaji wasiona uchungu na nchi yao na kutumia madaraka yao vibaya na kupelekea serikali kuingia hasara kubwa na kushindwa kuwahudumia wananchi.

Hayo yalisemwa na mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro wakati akifunga  mkutano wa mwaka wa kongamano la saba wa bodi ya manunuzi na ugavi uliofanyika kwa siku mbili jijini Arusha.
Alisema kuwa kumekuwawepo na baadhi ya maofisa wa serikali wanaofanya ubadhirifu katika sekta hiyo ya manunuzi na kuwa wao wamekuwa na ubinafsi mkubwa unaopelekea serikali kuingia hasara kubwa hivyo hawapo teyari kuwavumilia watu wa aina hiyo.
Daqarro aliekuwa akiongea kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha alisema kuwa watu wa manunuzi ni muhimu kwani wamekuwa wakifanyakazi nzuri hivyo endapo wakisimamia maadili vizuri na kuwaka mbele uzalendo na uchungu kwa taifa lao watafanikiwa katika majukumu yao itasaidia kama taifa kupata maendeleo.
“Nawasihi Ndugu zangu kuwa na uchungu na uzalendo kwa taifa lenu kwa kuhakikisha maendeleo yanapatikana kupitia utaalamu wenu kwani nchi yetu imekuwa ikipata hasara kwa asilimia 50% ya manunuzi kama ripoti ya mkaguzi mkuu wa serikali inavyoainisha”alisisitiza Daqarro
Kwa Upande wake Kaimu mkurugenzi mkuu wa bodi ya manunuzi na ugavi Godfrey Mbayi alisisitiza kuwepo utawala bora katika mchakato wa manunuzi ya umma ilikuondoa hali ya udanganyifu inayotokea mara kwa mara.
Alisema kuwa masuala mbali mbali katika manunuzi ya umma yanahitaji wigo mpana na kuweka mbele uzalendo utakaosaidia kuliondoa taifa eneo moja kwenda jingine na sisi wataalama tunahitajika kulivalia njga suala hili.
Nae mwenyekiti wa bodi ya manunuzi na ugavi sister Helen Bandiko alitoa Rai  kwa wale wote wanaofanya manunuzi ya serikali kuwa na sifa zinazostahili ili kulida upotevu wa fedha za serikali katika manunuzi ya umma ikiwemo fedha za miradi ya serikali.

No comments :

Post a Comment