Wednesday, December 21, 2016

MAMLAKA YA MAPATO NCHINI (TRA) YAWAASA WASANII WA FILAMU NA MUZIKI KURASIMISHA KAZI ZAO.


img_5244
Katibu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime kulia  akizungumza katika semina iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) juu ya Elimu ya Mlipa Kodi.Kulia kwake ni Rais wa Shirikisho la Filamu Nchini (TAFF) Bw.Simon Mwakifamba.
img_5255
Viongozi mbalimbali kutoka COSOTA,BASATA,Bodi ya Filamu,Shirikisho la Filamu Nchini(TAFF) na Shirikisho la Muziki Tanzania (TMF) wakipata Elimu ya Mlipa kodi kutoka kwa maafisa wa Mamlaka ya Mapato nchini(TRA) leo Jijini Dar es Salaam.
img_5259
Afisa wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi za ndani wa TRA  Bw.George Haule akizungumza na wasanii wa filamu na Muziki nchini juu ya Umuhimu wa Kulipa kodi na kusajili mali zao ili wachangie katika pato la Taifa.
img_5265
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Bi.Joyce Fissoo akiskiliza mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasiliswa na maafisa wa mamlaka ya mapato nchini(TRA) wakati wakitoa elimu ya mlipa kodi kwa wasanii wa Filamu na Muziki iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
img_5266
Wasanii mbalimbali wa Filamu na Muziki wa nchini wakiwa makini kusikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasiliswa na maafisa wa mamlaka ya mapato nchini(TRA) leo Jijini Dar es Salaam.Wasanii hao wamepata elimu ya mlipa kodi.
img_5282
img_5334
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma na Elimu kwa mlipa kodi Bi.Diana Masalla akizungumza na baadhi ya wasanii wa Filamu na Muziki nchini juu viwango mbalimbali vya Kodi wanavyolipa wafanyabishara nchini.
img_5346
Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania (TMF) Bw.Addo Novemba akichangia  jambo wakati wa semina kwa wasanii wa filamu na Muziki  iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) juu ya Elimu ya Mlipa Kodi.
………………………………………………………………………………
Na Daudi Manongi-MAELEZO.
Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imewaasa wasanii wa Filamu na Muziki kurasimisha kazi zao ili zitambulike na hivyo kuwasaidia katika kujiongezea vipato vyao wenyewe.

Hayo yamesemwa  na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA Bi.Diana Masalla wakati wa semina iliyoandaliwa na Mamlaka hiyo kwa wasanii wa Filamu na Muziki leo Jijini Dar es Salaam.
“Tumeamua kuwaandalia warsha hii ili muweze kupata uelewa juu ya suala zima la urasimishaji wa kazi zenu, kwa kuziwekea Stamp na kulipa Kodi ya mapato’’, Alisema Bi. Masalla.
Aidha ametoa wito kwa wasanii hao kujitokeza na kuwafichua wale wote ambao wanauza CD feki bila idhini yao kwani itawasaidia kujipatia kipato kupitia jasho lao na zaidi uwekaji wa stika utaisaidia kupata haki yao na Serikali kupata kodi kwa ajili ya maendeleo ya nchi.
Aidha kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Nchini (KBF). Bi.Joyce Fissoo amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kurasimisha Sekta ya Filamu nchini kwa kuwa sekta hii imekuwa mkombozi mkuu wa Ajira nchini na hivyo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Bodi ya Filamu wataweka kipaumbele katika kuweka adhabu stahili ili zichukuliwe kwa wezi wa kazi za wasanii hawa.
Mbali na hayo Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imesema kuwa semina hizi zitakuwa endelevu na hivyo makundi mbalimbali nchini na wadau watapata elimu hii muhimu kwa mlipa kodi  na hivyo kusaidia sekta hii kusonga mbele na pia kuchangia pato la Taifa.

No comments :

Post a Comment