Wednesday, December 14, 2016

MAHAKAMA YAMUACHIA HURU ALIEKUWA MWENYEKITI WA UVCCM ARUSHA POLISI YAMSHIKILIA TENA


ole-gai
Na Mahmoud Ahmad Arusha
 
MAHAKAMA ya hakimu mkazi Arusha, Desemba 14 imemwachia huru, Mwenyekiti wa UVCCM ,mkoa wa Arusha, aliyesimamishwa  Lengai Thomas Sabaya  ,baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuwasilisha ushahidi  dhidi yake kwenye kesi iliyokuwa ikimukabili.
 
Uanmuzi huo umetolewa leo na Hakimu Mkazi Gwantwa Mwankuga, baada ya upande wa mashitaka kuridhia kufutwa kwa kesi hiyo.
 
Haklimu alimwambia mtuhumiwa kuwa kwa kuwa serikali imeshindwa kuwasilisha ushahidi mahakama inakuachia huru.
 
Hata hivyo mara baada ya kutoka kizimbani Sabaya,ambae pia ni Diwani wa kata ya Sambasha, wilayani Arumeru, alikamatwa na jeshi la polisi na kufunguliwa mashitaka mapya .
 
Kesi ya awali mtuhumiwa alikuwa akishitakiwa kwa makosa mawili ambayo ni kujifanya mtumishi wa Umma na shitaka linguine ni kughushi  na kujipatia kitambulisho cha usalama wa taifa kinyume cha sheria.
 
Upande wa jamhuri uliwasilishwa na Grace Medikenga, ambae aliiambia mahakama hiyo iondolewe kwa sababu hawajajipanga hivyo hawaoni haja ya kuendelea na kesi hiyo.
 
Kwa upande wake wakili wa utetezi Yoyo Asubuhi, akizungumza mara baada ya kesi hiyo kufutwa, amesema kwa mjibuwa sheria mkurugenzi wa mashitaka anayo mamlaka ya kumkamata mtu pindi anapoaachuiliwa huru na mahakama na hivyo kufungua mashitaka mapya.
 
Desemba 7 mahakama hiyo iliuamuru upande wa jamhuri kuhakikisha Desemba 14 unatoa maelezo  ya kesi hiyo vinginevyo itaifuta.
 Kwenye kesi hiyo Jamhuri ilikuwa na mashahidi watatu ambao ni Philip John Sihaki ,ambae ni meneja wa hotel ya Sky way, mwingine ni Inspekta Rogati wa jeshi lan polisi kituo kikuu cha Arusha, na shahidi wa tatu ni Editer Evareen kutoka ofisi ya rais.(rso)

No comments :

Post a Comment