Wednesday, November 23, 2016

TRA Kutoa Elimu ya Kodi na Uwekezaji kwa Wafanyabiashara 200 wa Kichina.

trb1
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka TRA Richard Kayombo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu semina kwa jumuiya ya wafanyabiashara wa china itakayofanyika tarehe 25 Novemba 2016, leo jijini Dar es Salaam.Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya  Jiteng Consultancy Limited Bw. Andrew Huong na Meneja Msaidizi wa Kampuni hiyo Bw. Wesley Huung (kushoto).
trb2
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka TRA Richard Kayombo akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu semina kwa jumuiya ya wafanyabiashara wa Kichina itakayofanyika tarehe 25 Novemba 2016.
trb3
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano uliowakutanisha  wadau kutoka TRA na Jumuiya ya wafanyabiashara wa China leo Jijini Dar es Salaam.
trb4
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya  Jiteng Consultancy Limited Bw. Andrew Huong (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu semina kuhusu elimu ya mlipa kodi na uwekezaji ikatakyofanyika tarehe 25 Novemba 2016 katika ukumbi wa BOT jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka TRA Richard Kayombo na Meneja Msaidizi wa kampuni hiyo Wesley Huung.Picha zote na: Frank Shija – MAELEZO.

…………………………………………………………………
Na. Lilian Lundo – MAELEZO
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kushirikiana na Ubalozi wa China hapa nchini imeandaa warsha kwa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa China kuhusu mambo ya kodi na uwekezaji.
Hayo yamesemwa leo, Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi kutoka TRA Bw. Richard Kayombo alipokuwa akiongea na vyombo vya habari juu ya warsha ya kutoa elimu ya mambo ya kodi na uwekezaji kwa wafanyabiashara hao wa Kichina.
Kayombo amesema kuwa warsha hiyo itafanyika Ijumaa Novemba 25, 2016 katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Jijini Dar es Salaam ambapo lengo kuu la warsha hiyo ni kuwawezesha wafanyabiashara hao wa Kichina kuzingatia na kuzitumia sheria za  kutoza kodi sahihi pamoja na kukokotoa kodi ya zuio katika bidhaa na huduma na hivyo kuongeza ulipaji wa kodi kwa hiari miongoni mwao.
“Mada zitakazowasilishwa ni pamoja na mabadiliko ya bajeti 2016/17, masuala ya forodha na uondoshaji wa bidhaa, kodi ya zuio hususani katika sekta ya ujenzi pamoja na kodi ya ajira,” alifafanua Bw. Kayombo.
Aliendelea kwa kusema kuwa, wafanyabiashara hao watapata fursa ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi wa masuuala mbalimbali ili kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.
Aidha mada hizo zimeandaliwa kwa kuzingatia umuhimu wa kuongeza uelewa miongoni mwa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa China na kuzingatia matakwa ya sheria.
Kwa upande wake, Mratibu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kichina Tanzania, Andrew Huang amesema kuwa warsha hiyo itawasaidia wafanyabiashara wa Kichina kufanya biashara kwa kufuata sheria za kodi za Tanzania kutokana na wengi wao kutokuwa na elimu hiyo.
Waziri wa Biashara na Viwanda Charles Mwijage anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wa warsha hiyo ambayo pia itahudhuriwa na Balozi wa China hapa nchini.

No comments :

Post a Comment