Wednesday, November 23, 2016

TBL Kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu Kwa kasi kubwa.

ngano1
Wataalamu wa kilimo wakiongea na wakulima wa zao la shahiri wanaoshilikiana na TBL -Karatu
ngano3
Wananchi wakipatiwa mafunzo ya ujasiriamali kupitia mpango wa RDP wa TBL
ngano4
Wakulima wanaoshirikiana na TBL katika mashamba yao wilayani Karatu
ngano5 ngano6
Moja ya panel ya kuvuna umeme wa jua katika kiwanda cha Mbeya
………………………………………………………………………
Kampuni ya TBL Group imeeleza mkakati wake wa kuendelea kutekeleza malengo yake yanayoshabihiana na Malengo ya Maendeleo Endelevu ((SDGs)  yaliyobainishwa na Umoja wa Mataifa ,lengo kubwa likiwa ni kuondoa changamoto mbalimbali zilizopo kwenye jamii na kuifanya dunia iwe sehemu nzuri ya Kuishi.

Meneja wa Uendelezaji Mauzo wa TBL,Bw. Malaki Sitaki,aliyasema hayo alipokuwa akitoa tathmini ya kampuni katika kutekeleza mpango wa kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wateja wanaouza bidhaa zake kupitia mpango wa Retail Development Programme ulioanza mwaka jana unaoenda sambamba na elimu ya Unywaji Kistaarabu.


 Alisema kuwa hivi sasa kampuni hiyo imejikita zaidi kufanya biashara sambamba na kwendana na malengo hayo dhamira kubwa ikiwa ni kuyafanikisha na kuondoa changamoto zilizopo kwenye jamii mojawapo ikiwa ni kuondoa umaskini uliokithiri kwenye jamii mbalimbali.


Tumeanza kwa kasi kufanya kazi na wananchi katika maeneo tunayofanyia biashara kwa kusaidia miradi mbalimbali yenye mwelekeo wa kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu  kama ulivyo mtizamo wa kampuni na mafanikio makubwa yameanza kupatikana hususani katika  nyanja za uchumi, ustawi wa jamii na utunzaji wa mazingira”.Alisema.


Sitaki alisema kampuni imejikita katika kutunza mazingira,kuboresha huduma za maji na uhamasishaji wa matumizi mazuri ya maji,kusaidia wanawake kwenye miradi ya kiuchumi endelevu,kutoa elimu ya ujasiriamali na unywaji kistaarabu,kusaidia wakulima kujikwamua kiuchumi kupitia shughuli za kilimo,kupanua wigo wa ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja na kusaidia miradi katika sekta ya afya na elimu.

Alisema TBL itaendelea kuunga mkono jitihada za serikali katika kuleta ufanisi kukabiliana na changamoto mbalimbali na kushirikiana na wananchi kuleta mabadiliko chanya kwa kuwa inaamini wananchi ndio wadau wakubwa wa kufanikisha malengo haya na hawapaswi kuachwa nyuma.


Kuhusiana na maendeleo ya mpango wa kutoa elimu ya ujasiriamali unaoendeshwa na kampuni alisema kuwa mafanikio makubwa yamepatikana katika kipindi cha miaka 2 tangia uanzishwe kwa kuwafikia wajasiriamali zaidi ya 2,500 kutoka mikoa yote ya Tanzania na matarajio  ya kampuni ni kuwafikishia elimu zaidi ya wajasiriamali 20,000 hadi ifikapo mwaka 2019.


“Mwitikio wa wahitaji wa mafunzo haya ni mkubwa na kinachofurahisha idadi kubwa ya wajasiriamali wanaoshiriki  mafunzo haya ni Wanawake.Hii kwetu ni faraja kubwa kwa kuwa tunaamini kuwaelimisha wanawake inakuwa umeelimisha jamii nzima na ni rahisi kuleta maendeleo na mabadiko endelevu kama ilivyo lengo la mpango huu”.Alisema Malaki

Alisema thatmini ya awali ya mpango imebainisha kuwa mafunzo yanaendelea  kuwanufaisha wasambazaji wa bidhaa za TBL ngazi ya chini (Retailer level) na asilimia kubwa ya waliopata mafunzo haya  wanaendelea kuendesha biashara zao na kujipatia faida inayowawezesha kuboresha maisha yao na familia zao  kwa kuzipatia lishe nzuri,watoto wao kupata huduma bora za kiafya na elimu .” Huu ndio mwelekeo wa uwekezaji wetu unaokwenda sambamba na kuleta mabadiliko kwenye jamii”.Alisema.

No comments :

Post a Comment