Sunday, November 20, 2016

TBL Group yaja na mkakati kabambe wa kufanya uzalishaji usioharibu mazingira

vict1
Gavin Van Wjik
vict2
Sehemu ya mitambo ya umeme ya kuzalisha umeme katika kiwanda cha TBL cha Mbeya
vict3
Sehemu ya mitambo ya umeme ya kuzalisha umeme katika kiwanda cha TBL cha Mbeya
vict4
……………………………………………………………..
Ni kwa kutumia nishati mbadala rafiki kwa mazingira
 
Mkurugenzi wa Ufundi wa kampuni ya TBL Group,Gavin Wijk,amesema njia kubwa ya kuondoa uchafuzi wa mazingira na  hewa kutokana na uzalishaji wa viwandani ni kutumia teknolojia za kisasa ambazo haziathiri mazingira mojawapo ikiwa ni  kufanya uzalishaji wa kutumia nishati ya umeme wa jua.
Akiongea na waandishi jijini Dar es Salaam,Gavin Van Wjik alisema kuwa TBL Group imejipanga kuhakikisha inaleta teknolojia rafiki kwa mazingira na tayari imeanza kufanya uzalishaji wa kutumia  nishati ya umeme wa jua katika kiwanda chake cha Mbeya.
Alisema umeme huo wa jua utaweza kupunguza  tani zipatazo 130 za hewa chafu  kwa mwaka na kampuni inao mkakati kuhakikisha teknolojia hii inasambazwa katika viwanda vyote  vilivyopo chini ya kampuni hiyo na alitoa ushauri kwa viwanda vingine vilivyopo nchini kuangalia uwezekano wa kufanya uzalishaji kwa kutumia teknolojia rafiki  kwa mazingira.
“Moja ya maazimio ya Wakuu wa nchi mbalimbali walipokutana mjini Paris nchini Ufaransa Desemba mwaka jana katika mkutano  kuhusiana na hali ya hewa duniani moja ya ajenda ilikuwa kuangalia uwezekano wa viwanda kufanya uzalishaji usioathiri mazingira.TBL Group tayari tumeanza kutekeleza maazimio hayo kwa vitendo na siku zote tutakuwa mstari wa mbele kulinda mazingira na vyanzo vya maji”.Alisema Gavin
Alisema uzalishaji wa kutumia nishati mbadala pia kwa kiasi kikubwa unaipunguzia kampuni gharama kubwa za kufanya uzalishaji wa kutumia umeme wa gridi ya Taifa na kutolea mfano wa umeme wa jua wa kiwanda cha Mbeya ambao unazalishwa Kilowati 268,000  kwa saa utaiwezesha kampuni kuokoa kiasi cha milioni 44 za malipo  ya ankra za umeme kwa mwaka.
“Umeme huu wa nishati ya jua tunautumia kwa asilimia 30 ya matumizi ya kiwanda iwapo tutakuwa na teknolojia ya kuweza kutuwezesha kupata umeme wa kutosheleza matumizi yote ya kiwanda gharama za uendeshaji zitazidi kupungua zaidi wakati huo tatizo la uchafuzi wa mazingira kupungua kwa kiasi kikubwa”.Alisema.
Gavin aliongeza kusema  kuwa mbali na TBL kuanza kutumia teknolojia ya umeme wa jua ikiwa ni  ya kwanza katika ukanda huu wa Afrika Mashariki vilevile katika kiwanda chake cha Mwanza inafanya uzalishaji wa kutumia pumba za mpunga na mashudu ya pamba.”Uzalishaji wa kutumia umeme unaotokana na mashudu ya pamba na pumba za mpunga unaendelea kupata mafanikio makubwa  kwa kupunguza uchafuzi wa mazingira , kuongeza ajira kwenye jamii na kupunguza gharama za uzalishaji”.
Alisema TBL Group inaunga mkono jitihada za serikali za kuigeuza Tanzania nchi ya viwanda na itaendelea kushirikiana na wadau wote katika sekta ya biashara na viwanda ili kuhakikisha  ndoto hii inatimia

No comments :

Post a Comment