Thursday, November 24, 2016

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA ATEMBELEA KIWANDA CHA MT. MERU MILLERS MJINI ARUSHA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na uongozi wa kiwanda cha Mt. Meru Millers mara baada ya kufanya ziara kiwandani hapo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mt. Meru Bw. Atul Mittal akitoa taarifa kwa Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan juu ya maendeleo ya kiwanda pamoja na changamoto wanazokutananazo wafanyabiashara wazawa.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia malighafi zinazotumika kuzalishia mafuta ya kupikia kutoka kiwanda cha Mt. Meru Miller kulia ni
Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mt. Meru Bw. Atul Mittal akitoa ufafanuzi juu ya malighafi hizo.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia malighafi zinazotumika kuzalishia mafuta ya kupikia kutoka kiwanda cha Mt. Meru Miller mjini Arusha.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akingalia ndoo za plastiki zinazotengenezwa na kampuni ya Mt. Meru Millers kwa ajili ya kuhifadhia mafuta ya kula ,kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mt. Meru Bw. Atul Mittal.

                          .....................................................................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inajipanga kuondoa utitiri wa kodi mbalimbali zinatozwa kwenye viwanda kama hatua ya kuviwezesha viwanda vingi nchini  kuongeza uzalishaji na kutoa ajira nyingi kwa watanzania.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo leo Jijini Arusha baada ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Mount Meru Millers ili kujua changamoto zinazokikabili kiwanda hicho ili Serikali iweze kuzifanyia kazi katika kuleta unafuu kwenye uzalishaji wa mafuta ya kupikia nchini.

Makamu wa Rais amesema mlolongo wa kodi zinazotozwa kwa wamiliki wa viwanda hazina uratibu mzuri hivyo mkakati ya Serikali wa awamu ya Tano inataka kuweka utaratibu mzuri wa ulipaji wa kodi hizo ikiwemo kuondoa kodi ambazo ni kero kwenye viwanda.

Amesisitiza kuwa Serikali ya awamu ya Tano imedhamiria kuhakikisha viwanda vingi vinajengwa nchini ambavyo vitatumia malighafi zinazozalishwa hapa nchini hali ambayo itasaidia uuzaji wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi kuuzwa kwenye masoko ya nje ya nchi na kuliingizia taifa mapato na kuongeza ajira kwa makundi mbalimbali ya wananchi.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema ziara ambazo anafanya kwenye viwanda mkoani Arusha ni kujionea jinsi viwanda hivyo vinavyofanya kazi za uzalishaji na pale kwenye changamoto zinazokwamisha viwanda hivyo kufanya kazi vizuri ziweze kufanyia kazi na Serikali.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mount Meru Millers Atul Mittal amesema kama Serikali itafuta au kuondoa utitiri wa kodi wanazotozwa kwenye Viwanda hivyo watakuwa na uwezo wa kuongeza maradufu uzalishaji na kutoa ajira nyingi kwa Watanzania.
Amesema kwa sasa Kampuni hiyo inafanya kazi kwenye nchi 10 barani Afrika na kwa Tanzania pekee imeajiri wafanyakazi zaidi ya 1000 ambao wanafanyakazi katika maeneo mbalimbali nchini.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini, (TANESCO), Mhandisi Felchesmi Mramba, (katikati), akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo Novemba 24, 2016. Alikuwa akitoa ufafanuazi kuhusu masuala muhimu ya TANESCO. Wengine pichani, kulia ni Meneja wa Vyuo vya TANESCO, Mhandisi Said Msemo na kushoto ni Kaimu Meneja Uhisano wa Shirika hilo, Leila Muhaji.

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
SERIKALI kupitia Shirika lake la umeme nchini TANESCO limefanya uwekezaji mkubwa kwenye miradi mbalimbali ya umeme yenye thamani ya Shilingi Trilioni 5.35, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Mhandisi Felchesmi Mramba amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo Novemba 24, 2016.
Akitoa ufafanuzi juu ya masuala mbalimbali muhimu ya Shirika hilo, Mhandisi Mramba alisema, “Katika historia ya sekta ya umeme, haijawahi kutokea uwekezaji mkubwa kufanyika kwa wakati mmoja kama ilivyo sasa, Miradi yote ya umeme inayoendelea na ambayo tayari iemtengewa fedha ina thamani ya Shilingi Trilioni 3.85, na majadiliano kati ya Serikali na Exim Bank ya mradi wa Dar es Salaam-Arusha wa Shilingi Trilioni 1.5 yakiwa katika hatua za mwisho.” Alifafanua Mhandisi Mramba.
“ Uwekezaji huu unathibitisha kwamba nia ya Serikali ya awamau ya tano ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda sio ya maneno matupu bali inaambatana na vitendo kwa uwekezaji madhubuti kwenye umeme.” Alisema.
Mhandisi Mramba alitaja Miradi hiyo mikubwa ya umeme kuwa ni pamoja na ule wa upanuzi wa Kinyerezi I, Kinyerezi II, mradi wa Backbone, Kenya-Tanzania, TEDAP, Makambako-Songea, Uboreshaji umeme jijini Dar es Salaam, City Centre-Dar es Salaam, Electricity V, Bulyanhulu-Geita, Geita Nyakanazi na Rusumo Power Plant (T), miradi yote hii ikiwa na jumla ya thamani ya Shilingi Trilioni 3.85.
Akifafanua zaidi kuhusu uwekezji huo, Mhandisi Mramba alisema, Miradi yote ambayo thamani yake imetajwa haihusishi Miradi ya usambazaji umeme Vijijini chini ya mpango wa REA.
Akizungumzia utaratibu mpya wa manunuzi,(Procumbent), Mhandisi Mramba alisema, TANESCO imechukua hatua kadhaa ili kuboresha manunuzi ambapo kuanzia sasa makampuni yanayomilikiwa na mtu mmoja kuhodhi manunuzi ya Shirika hilo, na kwamba zabuni zote zilizotangazwa kuanzia mwaka huu wa fedha, haitaruhusiwa kampuni moja kuwa na mikataba miwili kwa wakati mmoja.
Akifafanua zaidi alisema, Katika zabuni moja haitaruhusiwa kampuni moja kupewa zaidi ya Lot 1, “Hii imeanza kusaidia kuondoa ukiritimba katika manunuzi na kuwapa Watanzania wengi zaidi nafasi pana ya kushiriki katika zabuni za kusambaza vifaa vya umeme.” Alifafanua Mhandisi Mramba.
Aidha Mhandisi Mramba alisema, ili kuwezesha Watanzania wengi kushiriki katika uchumi wa nchi, TANESCO itanunua vifaa vya umeme vinavyozalishwa hapa nchini na kuachana na mtindo wa kuagiza kutoka nje.
“Mfano kwa nguzo za umeme tumewapa Sao Hill, ambao watatuuzia nguzo 96,500, na new Forest watatuuzia nguzo za umeme 9,668, na kwa upande wa Transfoma za umeme, kandarasi hiyo imepewa kampuni ya TANELEC itakayotuuzia transfoma 1,500” Alifafanua
Akieleza zaidi kuhusu ununuzi wa vifaa, Mhandisi Mramba alisema, kampuni ya East Africa Cables, intarajiwa kupewa kazi ya kusambaza waya na kuongeza kuwa utaratibu huo pia utatumika kwenye huduma nyingine kama vile Bima, ambapo alisema Shirika linatarajia kulitumia Shirika la Bima la Taifa, (NIC), kutoa huduma hiyo.
Akizungumzia kuhusu hali ya umeme, Mhandisi Mramba aliwahakikishia Watanzania kuwa kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Shirika hilo katika kuboresha miundombinu ya umeme, hakutakuwa na mgao wa umeme nchini na ndio maana kwa muda mrefu sasa hakuna mgao wa umeme.“Mwaka 2015 nchi ilikuwa na mgao wa umeme wa jumla ya MW300, na maeneo mengine yalikuwa na hali mbaya hususan Mwanza, Arusha na Kilimanjarolakini kwa sasa hali ya umeme katika mikoa yote na mingine ni nzuri hakuna mgao na kama ikitokea umeme umekatika ni matatizo ya kiufundi katika eneo dogo na kwa muda mfupi.” Alisema.
Hata hivyo alisema Shirika lake linaongeza juhudi za kusambaza umeme kwa watanzania wengi zaidi kote nchini, kutokana na uwekezaji wa miundombinu unaoendela kila kona ya nchi.
Mhandisi Mramba aliwaondoa wasiwasi wananchi kuhusu ombi la Shirika hilo la kuongeza asilimia 18.9 ya bei ya umeme kuanzia Januari mwakani, kwa kusema ongezeko hilo halitaathiri watumiji wa kawaida majumbani. “Tunachoomba kutoka kwa Msimamizi (Regulator), ni kufanya mabadiliko ya kutenganisha watumiaji umeme wa majumbani na wale wanaotumia kibiashara kama vile mabango ya matangazo, kwani hivi sasa wote wanalipa gharama sawa na hili si sawa.” Alisema.
Aliwaasa wananchi kuridhia ongezeko hilo kwani Shirika limo katika jitihada kubwa za kuhakikisha Wananchi wengi zaidi wanapatiwa umeme kwa kufikisha miundombinu ya umeme kwenye maeneo mbalimbali ya nchi, ambapo gharama za kufanya hivyo zimeongezeka.

 Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo
  Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo
 Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji, (kushoto), akizunguzma jambo

Wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Kanda ya Kaskazini walipokutana na wanahabri mkoa Kilimanjaro kuzungumzia tukio la uzinduzi litakalo fanyika kesho Ijumaa katika viwanja vya kituo kikuu cha Mabasi mjini Moshi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Kanda ya Kaskazini ,Elizabeth Mushi akizungmza walipkkutana na wanahabari mkoani Kilimanjaro.
Wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya siku 16 za kupinga ukatili kutoka Mtandao wa Jinsia wa jeshi la Polisi (TPF Network) , Grace Lyimo (Kushoto) na Theresia Nyangasa.(Kulia).
Meneja Programu wa Shirika lisililo la Kiserikali linalojishughulisha na kupinga ukeketaji (NAFGEM) Honorata Nasuwa akizungumza mbele ya wanahabri juu ya uzinduzi rasmi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia .
Afisa Programu wa Shirika linalotoa msaada wa Kisheria Kilimanjaro-KIWECO,Hilaly Tesha akizungumza wakati wa mkutano wa na wanahabari kuzungumzia tukio hilo .
Baadhi ya wanahabari wa vyombo mbalimbali mkoa wa Kilimanjaro wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa.
Mwenyekiti wa Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi ,Elina Maro akizungumza katika mkutano huo na wanahabari.
Baadhi ya Wanahabari wakiwa katika mkutano huo.
Mkutano na Wanhabari mkoa wa Kilimanjaro ukiendelea.
Baadhi ya Wanahabri mkoa wa Kilimajaro wakiwa katika mkutano huo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) imeshirikiana na kampuni ya Getenrgy kuandaa mkutano wa Afrika wa Mafuta na Gesi (GETENERGY VTEC AFRICA 2016) ambao unafanyika nchini kwa siku tatu kuanzia Novemba, 21-23, 2016.

Katika hotuba yake ya utangulizi, Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida alisema kuwa mkutano huo umekutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya mafuta na gesi kutoka nchi mbalimbali Afrika ikiwepo serikali, viwanda, mashirika ya maendeleo na vyuo ambavyo vinatoa elimu ya mafuta na gesi.

Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida akitoa neno la utangulizi katika Mkutano wa Afrika wa Mafuta na Gesi.

"Malengo ya mkutano huu ni kuangalia changamoto gani ambazo zinalikabili Bara la Afrika katika sekta ya mafuta na gesi, kubadilisha ujuzi kwa wataalamu wa mataifa ambayo yameshiriki na kujadili hatua ya kuchukua ili kuboresha sekta hii lakini pia utasaidia kukuza ushirikiano baina ya nchi washiriki,

"Katika mkutano washiriki wataisaidia Serikali na wadau kuweka mikakati ya kutekeleza na yenye ufanisi kuhusu sekta ya mafuta na gesi na kama Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamiii tutaendelea kushirikiana na wadau kutafuta changamoto zinazokabili sekta na mbinu za kutumia ili kuyatatua," alisema Dkt. Kida.

Mgeni rasmi katika mkutano huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu akizungumza umuhimu wa mkutano huo na jinsi ambavyo unaweza kuwanufaisha Watanzania.

Kwa upande wa mgeni rasmi katika mkutano huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu alisema, Serikali kwa sasa inataka kuhakikisha kunakuwapo na wataalamu wengi ili kunapokuwepo na sehemu ambazo kunapatikana mafuta au gesi waweze kushiriki wenyewe ili kipato kinachopatikana kiwanufaishe wananchi na Taifa kwa ujumla.

"Nchi ina akiba nyingi ya gesi na tunategemea kupata mafuta baadae lakini tunangaalia upande wa wataalamu, tunahitaji kuwa na wataalamu katika sekta ya mafuta na gesi ili tutakapoanza shughuli ya uchimbaji tayari tuwe na wataalamu wanaohitajika hapa nchini,

"Huu ndiyo mchango wa ndani, hatuwezi kufanya sisi pekee lazima tuwe na wageni lakini pia tuwe na Watanzania wanaotumikia sekta hii na wanaofaidika na uchimbaji wa hayo mafuta," alisema Mama Samia.

Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo akieleza jinsi ambavyo Serikali imejipanga kuinua sekta na mafuta na gesi ili Watanzania wengi wanufaike na uwepo wa mafuta na gesi nchini.

Nae Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo alisema Serikali imejipanga kuboresha sekta ya mafuta na gesi kwa kutoa elimu kuhusu sekta hiyo katika baadhi ya vyuo mbalimbali nchini ili wahitimu wanapomaliza waweze kuingia moja kwa moja katika sekta hii.

"Tupo katika orodha ya nchi 20 Afrika ambazo zinafanya vizuri, baada ya miaka mitano tutakuwa tumepiga hatua na mtaona ni jinsi gani tumefanikiwa, kwasasa tuna wanafunzi wamehitimu UDOM na tunashirikiana na China na Uingereza kwahiyo niwahakikishie kuwa tumejipanga," alisema Prof. Muhongo.

Mkurugenzi wa kampuni ya Getenergy, Virginia Baker akitoa taarifa kuhusu kampuni hiyo, malengo na umuhimu wa kufanyika kwa mikutano hiyo.

Mikutano ya GETENERGY VTEC kwa mwaka 2016 tayari imeshafanyika katika nchi ya Mexico na Uingereza na imekuwa ikikutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya mafuta na gesi ili kujadili jinsi sekta hiyo inaweza kuboreshwa na kuwa bora zaidi kuliko ilivyo sasa.

Wadau mbalimbali wa sekta ya mafuta na gesi kutoka mataifa mbalimbali wakifuatilia mkutano wa mafuta na gesi ambao mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu.



Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu akipewa maelekezo kutoka kwa msimamizi wa banda la Chuo cha AGR TRACS kuhusu masomo yanayotolewa na chuo hicho. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki kuimba wimbo wa mshikamano kabla ya kufungua Mkutano  Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi  (TUCTA) kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23, 2016.  Kulia kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu   Mkuu  Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama    na kushoto kwake ni  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana . (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Wafanyakazi (TUKTA) kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23, 2016.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri  Mkuu   Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama akiwasalimia wajumbe
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi, Angela Kairuki akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) uliofunguliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23,2016


Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) , Gratian Mukoba  akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) uliofunguliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23,2016
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Wafanyakazi (TUKTA) kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23, 2016.
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Sita wa  Shirikisho la Wafanyakazi (TUCTA) wakiimba wimbo wa Mshikamano kabla ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kufungua mkutano wao kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23, 2016.

Baadhi ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) wakimsikilza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipofungua mkutano huo kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23, 2016
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Ulumbi Shani ambaye alikuwa ni mmoja wa washiriki wa Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Vyama  vya Wafanyakazi (TUKTA)  uliofunguliwa na Waziri Mkuu kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) na wananchama wa TUCTA baada ya kufungua Mkutano  Mkuu wa Sita kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma Novemba 23, 2016. Kulia kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Kazi,  Ajira , Vijana na Walemavu, Jenista Mhagama na kulia kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi, Angela Kairuki

 Waziri Mkuu akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana
Waziri Mkuu akisalimiana na Rais wa CWT, Gratian Mukoba

No comments :

Post a Comment