Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Kampuni ya Whitedent nchini
Tanzania imekabidhi magari manne aina ya Suzuki Alto K10 kwa washinda wa
promosheni ya miezi mitatu iliyokuwa inasherekea kuadhimisha miaka 25
ya bidhaa hiyo ambayo imefanyika na mikoa mbalimbali na kutoa jumla ya
magari 25.
Akizungumza na katika hafla hiyo
ya makabidhiano yaliyofanyika maeneo ya Mabibo jijini Dar es
salaam,Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Chemi & Cotex Raja Swaminatha
amesema kuwa Shindano hilo lililokuwa chini ya uangalizi mkubwa na wa
makini wa bodi ya bahati Nasibu Tanzania lililochukua miezi mitatu na
kushirikisha mikoa yote ya Tanzania bara na visiwani Zanzibar.
Anamalizia kwa kusema kuwa katika
bidhaa za afya ya ngozi wana Bannisters Glycerine inayotumika kila siku
na familia katika kutunza ngozin na pia wana bidhaa nyingine
inayoongoza katika utunzaji wa ngozi kama
Sweetheart,U&ME,Siri,Bodyline na Zawadi Zanzibar na Chemi &
Cotex ina bidhaa za utunzwaji nywele chini ya Tressa.
No comments :
Post a Comment