Thursday, September 8, 2016

LEO KATIKA BUNGE MJINI DODOMA SEPTEMBA 8, 2016; WAZIRI MKUU MAJALIWA APAMBANA NA MASWALI YA PAPO KWA HAPO, SPIKA AONYA FUKUZA FUKUZA WANACHAMA WA VYAMA VYA SIASA


Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa, (kushoto), akisikiliza maswali kutoka kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mh. Freeman Mbowe, wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, kwenye kikao cha 3 cha Mkutano wa 4 wa Bunge la 11 mjini Dodoma, Septemba 8, 2016. (PICHA NA HASSAN SILAYO WA MAELEZO)

 Waziri MkuuMajaliwa akijibu sehemu ya maswali aliyoulizwa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akisalimiana na Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzania Bungeni na Mbunge wa Hai Mhe. Freeman Mbowe (MB) kwenye kikao cha 3 cha Mkutano wa 4 wa Bunge la 11 mjini Dodoma, Septemba 8, 2016 ambapo Waziri Mkuu alikuwa akijibu maswali ya papo kwa hapo.

 Waziri Mkuu, akishukuru wakati alipopongezwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Micehzo, Nape Nnauye, marabaada ya kujibu kwa usahihi maswali hayo
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu), Dkt. Abdallah Possi, akijibu swali bungeni ambapo alisema kuwa serikali ipo tayari kushirikiana na raia katika kuhakikisha inakabiliana na biashara haramu ya Madawa ya Kulevya.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dkt. Suzan Kolimba akijibu swali bungeni ambapo alisema serikali ipo katika mazungumzo na serikali ya China kwa ajili ya kuboresha zao la Tumbaku.


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akijibu swali bungeni ambapo alisema Wizara imetenga Shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kuboresha hali ya Magereza nchini.



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongea na wabunge na kuviasa vyama vya siasa vyenye tabia ya kufukuza wabunge kuacha hivyo kwani haviwatendei haki wapiga kura na ni gharama kwa serikali

No comments :

Post a Comment