Wednesday, August 24, 2016

MJUE MKURUGENZI MKUU MPYA WA IDARA YA USALAMA WA TAIFA ALIYEAPISHWA LEO NA RAIS MAGUFULI


Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.John Pombe magufuli akimuapisha Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016


KABLA ya kuteuliwa na Rais John Pombe Magufuli hivi karibuni, Kukaimu ukurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dkt. Kapilimba, (pichani), alikuwa Mkurugenzi wa Udhibiti Majanga wa BENKI Kuu ya Tanzania, ambako alifanya kazi kuanzia mwaka 2011, kabla ya kufanya kazi hiyo, Dkt. Kapilimba alikuwa Meneja wa Udhibiti Mfumo wa Majanga, Benki Kuu ya Tanzania, nafasi aliyoshikilia kutoka mwaka 2009 hadi 2011 alipopandishwa cheo kuwa Mkurugenzi wa Udhibiti Majanga Benki Kuu ya Tanzania.
Kabla ya kuwa Meneja udhibiti mfumo (System Risk), Dkt. Kapilimba alifanya kazi kama Mshauri wa Information Technology (IT), wa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, kuanzia mwaka 2008 hadi 2009.
Dkt. Kapilimba pia amewahi kuwa Mhadhiri na mkuu wa Idara ya Computer na Mifumo ya Habari, Chuo Cha Masomo ya Kitaaluma cha Manchester nchini Uingereza.(MCPS). Pia lifanya kazi ya uhadhiri kwa muda (Part time), Usanifu wa Computer, (Computer Architecture), Chuo Kikuu Cha Salford nchini Uingereza.
Dkt. Kapilimba ana PhD ya Sayansi ya Computer kutoka Chuo Kikuu cha Canterbury nchini Uingereza, MSc. Katika Sayansi ya Computer kutoka Chuo Kikuu Cha Salford nchini Uingereza, BSc.(Ed.) Hons katika Mahesabu, Fizikia na Elimu, kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Lakini pia Msomi huyo aliyebobea kwenye mifumo ya computer, ni mwanachama wa Mashirika mbalimbali vya Kitaaluma, ikiwa ni pamoja na Charter IT, cha Chama cha Sayansi cha Uingereza (British Computer Society), (MBCS CITP, pia cha Uingereza, Taasisi ya Uchambuzi na Programu (MIAP), cha Uingereza, na Taasisi ya Uhandisi wa Umeme na Vifaa vya Umeme (IEEE), cha Marekani.
Chanzo:-MetricStream




Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.John Pombe magufuli na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan pamoja na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki, Mwanasheria Mkuu wa  Serikali Mhe George Masaju na Katibu Mkuu kiongozi Mhandisi John Kijazi katika picha ya pamoja na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama baada ya kuapishwa kwa  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba  Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016
 (PICHA NA IKULU)

No comments :

Post a Comment