NA
K-VIS MEDIA
MAUAJI
ya kitatanishi dhidi ya askari wa Jeshi la Polisiyamerejea tena naaba ya polisi
wannee kuuawa kwa kupigwa risasi huko Mbande, wilaya ya Temeke jijini Dar es
Salaam majira ya usiku kwenye tawi la benki ya CRDB.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akiwa amevalia magwanda ya polisi
alifika eneo la tukio akifuatana na polisi wa Kanda Maalumya Dar es Salaam,
Simon Siro na kuthibitisha vifo hivyo.
Alisema,
wavamizi hao waliokuwa na nia ovu, walitumia usafiri wa pikipiki na walifika
eneo la tukio wakati askari wakibadilishana lindo majiraya saa 1 na saa 2 usiku
wa Agosti 23, 2016, wavamizi walifyatua risasi na kuwauwa askari hao, alisema
Waziri Nchembakwa huzuni.
Vyanzo
vya habari vinasema, wauaji wametoroka na bunduki moja ya polisi aina ya (Sub-Machinegun-SMG),
lakini jambo la kustaajabisha, hawakuingia ndani ya benki hiyo.
Jambo
hilo ndilo linalostaajabisha mashuhuda wa tukio hilo na kutafsiri kuwa ni
mauaji ya makusudi dhidiya polisi, alisemashuhuda mmoja.
“Nitoe
pole kwa IGP na familia za marehemu, tayari vijana wameingia kazini na msako
unaendelea kila kona kuhakikisha wauaji haowanatiwa mikononimwa vtyombovya do,”
alisema Waziri Nchemba.
Jambo
la kutia shaka, wauaji hawakuingia ndaniya benki, kwani baada ya kutekeleza
shambulio hilo waliondoka.
Mwanzoni
mwa mwaka huu, kumeshuhudia matukio ya mauaji ya polisi kwenye maeneo kadhaa ya
nchi, ambapo silahapia ziliporwa. Hata hivyo polisi walifanikiwa kutuliza wimbi
hilo la mauaji kwa kufanya opereshenikubwa na tayari imewatia mbaroni baadhi ya
wanaotekeleza mauaji hayo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mwigulu Nchemba (mwenye kombati), akimjulia hali mmoja wa
askariwaliojeruhiwa kwenye shambulio hilo
Waziri akiwa na Kamanda wa Kanda Maalum
ya Dar es Salaam, SimonSiro (kushoto), kwenye eneo la tukio usiku wa
kuamkia leo Agosti 24, 2016
Waziri akitafakari na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es
Salaam, SimonSiro (kushoto), kwenye eneo la tukio usiku wa kuamkia leo
Agosti 24, 2016
No comments :
Post a Comment