SWALA YA ED-EL-FITR ILIVYOFANYIKA VIWANJA VYA MWEMBE YANGA JIJINI DAR ES SALAAM LEO ASUBUHI
MOTO WATEKETEZA MABWENI MATATU YA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA MGONGO, IRINGA
Mkuu
wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela alishiriki katika kuzima moto
uliounguza bweni wanalokaa watoto yatima katika kituo cha Mgongo.
Moto huo ilioanza kwa hitilafu ya umeme umeteketeza mabweni 3 na kuunguza mali za watoto hao ikiwemo nguo, madaftari magodoro.
Kikosi
cha zimamoto chini ya Mrakibu Komba kilifanya kazi ya ziada kuzuia moto
huo usieneee majengo mengine. Wananchi wa eneo la Mgongo wamefanya kazi
kubwa wakisaidiana na jeshi la zima moto.
Akizungumza
na wananch,i Mh Kasesela ameahidi kuomba wahisani pia kuangalia
uwezekano wa kuwasaidia waathirika wa janga hili la moto. Inakadiriwa
watoto zaidi ya 45 wameathirika na moto huu ingawaje hamna majeruhi hata
mmoja.
"
nilipata taarifa nikiwa kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki
ya CRDB ikabidi niache nije mara moja nafurahi kuona tumefanikiwa kuzima
moto ingawaje umeleta madhara makubwa Pongezi ziwandee jeshi la
Zimamoto pamoja na changamoto walifanikiwa kuzima moto huo" aliesema
Mkuu wa Wilaya.
Mkuu
wa wilaya alikutana na watoto na kuwapa matumaini serikali ipo pamoja
nao. Serikali ya Wilaya ya irnga inawaomba wadau wajitokeze kusaidia
watoto hawa mahitaji makubwa ni magodoro, blanketi na nguo hasa kipindi
hiki cha baridi.






No comments :
Post a Comment