Tuesday, May 24, 2016

MAJALIWA AWASILI LUSAKA MAJA

MAJA 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri wa Ulinzi wa Zambia, Christopher Mulenga baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Keneth Kaunda uliopo Lusaka  Mei 23, may 2016 ambako leo atamwakilisha Rais John Magufuli kwenye mkutano wa  Benki ya Maendeleo ya Afrika _ADB. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MATUKIO KATIKA PICHA LEO KUTOKA BUNGENI, DODOMA

NG1 
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira ambaye pia ni Mbunge Jimbo la Kisesa, Mhe. Luhaga Joelson Mpina (kushoto) akiwa ameongozana na Mbunge wa CHADEMA Jimbo la Iringa Mjini, Mhe. Mchungaji Peter Simon Msigwa wakielekea Bungeni kwa ajili ya vikao vya asubuhi ndani ya bunge hilo leo 24 Mei, 2016.
NG2 
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Sospeter Mwijarubi Muhongo akiwasili Bungeni kwa jili ya kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
NG3 
Mbunge wa CHADEMA Jimbo la Mikumi, Mhe. Joseph Leonard Haule akiwasili Bungeni kwa jili ya kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
NG4 
Naibu Waziri, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mb), Mhe. Eng. Edwin Amandus Ngonyani (kushoto) akiwa ameongozana na Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Eng. Hamad Yusuf Masauni wakielekea ndani ya Bunge kwa ajili ya vikao vya asubuhi vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016.
NG5Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi, Mhe. Andrew John Chenge (kulia) akiwa ameongozana na Mbunge mwenzie wakielkea ndani ya Bunge kwa ajili ya vikao vya asubuhi ndani ya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.

No comments :

Post a Comment