Na Beatrice Lyimo-Maelezo
Kampuni ya SBC Tanzania
Limited, watengenezaji na wasambazaji wa vinywaji baridi imepunguza bei
ya vinywaji vyake kutoka shillingi mia sita (600) hadi mia tano (500)
kwa chupa yenye ujazo wa Mililita 350 na 300.
Hayo yamesemwa na Meneja
Mafunzo na Uwezeshaji Bw.Rashid Chenja alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa lengo la
kupunguza bei ni kutokana na hali ngumu ya uchumi iliyopo.
“Imekuwa vigumu kwa mnywaji
kuweza kudumu bei ya kinywaji akipendacho cha pepsi , gharama za maisha
zinapanda kila mwaka na soda imekuwa ghali kiasi cha wananchi wa kawaida
kushindwa kumudu kununua soda hivyo kampuni imeamua kupunguza bei”
alifafanua Meneja huyo.
Pia amesema kuwa kampuni ya SBC
Tanzania imefanya punguzo hilo kuanzia tarehe 16/11/2015 kwa vinywaji
vya Pepsi, Mirinda,7up, Mountain Dew na Evervess na maeneo yatakayo
husika na punguzo hilo la bei ni Dar es salaam,Morogoro, Dodoma, Pwani,
Tanga, Lindi, Mtwara na Zanzibar.
“Ni matumaini yetu mtaendelea
kutuunga mkono katika biashara yetu kwa kununua soda zetu kwa bei
iliyopendekezwa ya shilingi Mia Tano kwa chupa, shilingi elfu tisa mia
nne (9,400) kwa kreti moja na faida kwa wauzaji wa rejareja itakuwa ni
shilingi 2500 kwa kila kreti” aliongeza Bw. Chenja.
Mbali na hayo Kampuni ya SBC
Tanzania Limited inawashukuru wateja wake kwa kuwaunga mkono katika
biashara yao kwa kipindi cha miaka 14 hapa nchini.
CHAMA CHA ADC CHAFUTA VIKOSI VYAKE VYA ULINZI NA USALAMA
Na Magreth Kinabo- MAELEZO
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya
Siasa, imeviasa vyama vingine vya siasa kuiga mfano wa Chama cha
Alliance For Democratic Change(ADC- Dira ya Mabadiliko) kutokana na
juhudi zake za kutii sheria bila shuruti kutokana na kuvunja vikosi vya
ulinzi na usalama.
Kauli hiyo imetolewa leo na
Naibu Msajili wa Vyama Vya Siasa nchini, Sisty Nyahonza wakati
akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dares Salaam
jinsi chama hicho kilivyotekeleza Sheria ya Vyama Vya Siasa Sura ya 258
kifungu cha 9(C) ambayo hairuhusu chama chochote cha siasa kutumia
nguvu ili kufikia malengo yake, kwa kutumia vikosi hivyo.
Naibu Msajili huyo alisema
chama hicho kimefuta Idara ya Ulinzi na Usalama kijulikanacho kwa jina
la Star Guards kwa mujibu wa barua yao iliyowasilishwa katika ofisi
hiyo.
Alisema kwa mujibu wa barua ya
chama hicho, iliyosainiwa na Katibu Mkuu Taifa, Lydia Bendera, Novemba
13, mwaka 2015, yenye kumbukumbu namba ADC /HQ/GEN/VO1.1/81/15,ambayo
ilieleza kwamba kutokana na kikao cha Baraza la Vyama Vya Siasa
kilichofanyika Aprili 22,mwaka huu ambacho agenda kuu ilikuwa ni
kujadili suala la vyama vya siasa kuwa na vikundi hivyo ni ukiukwaji wa
sheria za nchi, na kufikiwa maamuzi yake kuwa;
1. Vyama vya siasa havina
budi kuheshimu sheria za nchi, na kutakiwa kuvunja vikundi vya ulinzi na
usalama vilivyoko katika vyama vya siasa.
2. Vyama vya siasa
vinatakiwa kuondoa katika Katiba za vyama vifungu,ibara zinazoruhusu
kuanzishwa kwa vikundi vya ulinzi na usalama.
Alisema barua hiyo ambayo
iliendelea kufafanua kwamba “kwa kuzingatia maazimio yaliyofikiwa kati
ya viongozi wakuu wa vyama vya siasa na ofisi ya msajili wa vyama vya
siasa nchini yaliyofikiwa na vyama, chama chetu kimekwisha chukua hatua
ya utekelezaji wa maazimio ya baraza la vyama, na yale yote
uliyoyaelekeza kupitia barua yako yenye kumb. namba HA.322/362/20/22 ya
tarehe 16/06/2015.
“ Kupitia barua hii
ninakujulisha rasmi kuwa Mwenyekiti wa Chama Taifa kwa mamlaka aliyopewa
na kanuni za chama chetu , ametengua uteuzi wa Mhe. Omari Albert
Constantino kuwa mkuu wa idara ya STAR GUARDs,” ilieleza barua hiyo.
Naibu Msajili huyo alisema
chama hicho “kimetii sheria ya nchi na hii iwe chachu kwa vyama vingine
kwa kuwa kutuii sheria ni kipaumbele cha demokrasia,” alisema Nyahonza.
Aliongeza kwamba demokrasia
ina vitu vitatu ambavyo ni utii wa sheria, amani na utulivu, hivyo ili
demokrasia ifanye kazi lazima kuwe na vitu hivyo.
Aidha Nyahonza alisema Ibara ya 107 ya Katiba ya Nchi inaruhusu Serikali pekee kuanzisha vikosi hivyo.
Akizungumzia kuhusu kwa chama kitakachokiuka agizo hilo, kitachukulia hatua gani alisema kufanya hivyo ni kosa la jinai.
“Sisi tunafanya kazi na jeshi la polisi, ukikataa kufanya hivyo utakamatwa na utalazimishwa kutii sheria,” alisisitiza.
BALOZI WA UINGEREZA NCHINI AONGOZA UZINDUZI WA FILAMU YA KUPINGA UKEKETAJI YA SIMULIZI HALISI YA GHATI NA RHOBI
Balozi
wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose (kushoto), Mkurugenzi
Mtendaji wa Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Koshuma Mtengeti (kulia) na
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Wanawake wa Afya, Utafiti na Maendeleo
(Forward), Naana Otoo-Oyortey MBE, wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa
Filamu ya Simulizi halisi ya Ghati na Rhobi ulifanyika nyumbani kwa
balozi huyo, Oysterbay Dar es Salaam jana.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose (kulia), akizungumza kabla ya uzinduzi wa filamu hiyo.
Mwakilishi kutoka taasisi ya DFID, Jane Miller OBE (kushoto), akizungumza katika uzinduzi huo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Koshuma Mtengeti na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Wanawake wa Afya, Utafiti na Maendeleo (Forward), Naana Otoo-Oyortey MBE.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Wanawake Tanzania, Mary Rusimbi (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo.
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Sehemu ya filamu hiyo inavyoonekana.
Sehemu ya filamu hiyo inavyoonekana.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Mfuko wa Wanawake wa Afya, Utafiti na Maendeleo (Forward),
Naana Otoo-Oyortey MBE (katikati), akichangia jambo katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Koshuma Mtengeti (kulia),
akielezea kuhusu filamu hiyo na changamoto mbalimbali za ukeketaji
nchini.
……………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………
Na Dotto Mwaibale
LICHA ya MKOA wa Dar es Salaam kuwa na watu wenye uelewa mkubwa lakini unaongoza kwa asilimia 38 ya ukeketaji imeelezwa.
Hayo
yalibanishwa na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto Wizara ya Wanawake na
Watoto, Margaret Mussai Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa Filamu
ya Simulizi halisi ya Ghati na Rhobi uliofanyika nyumbani kwa Balozi wa
Uingereza hapa nchini.
“Hali
ya ukeketaji hapa nchini bado ni changamoto kubwa kutokana na jamii
kutokuwa na uelewa mkubwa ikiwa ni pamoja na mila za baadhi ya makabila”
alisema Mussai.
Alisema
suala la ukeketaji limekuwa na changamoto kubwa kwa sababu ya wahusika
wanaofanya ukeketaji wanatengeneza fedha na kwa msichana anayefanyiwa
kitendo hicho anaonekana kuwa na thamani kuliko yule ambaye hajakeketwa.
Alisema
kwa mkoa wa Dar es Salaam kuna maeneo ambayo yanaongoza kwa ukeketaji
na wasichana hupenda kufanyiwa hivyo ili waonekane wenye heshima.
Alisema
mkoa wa Dar es Salaam una asilimia 38 ya ukeketaji, Mara asilimia 58,
Shinyanga asilimia 55 huku ikifuatia mikoa mingine.
Balozi
wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose filamu hiyo inawahusu
wasichana wawili ambao wanapinga ukeketaji katika jamii yao.
Alisema
wasichana hao waqnaonesha ujasiri wa kukataa kitendo hicho chenye
maumivu makali na kwa msaada wanafanikiwa kubadisha jinsi jamii yao
inavyomchukulia msichana katika kipindi chake cha mpito kutoka usichana
hadi kwenda kufikia utu uzima.
“Filamu
hii inaonesha kwamba si jamii zote ndani ya Tanzania zinazojihusisha na
ukeketaji na kwamba maeneo mengi wameamua kuachana na ukeketaji na
kuamini kwamba ukeketaji unawezwa kutokomezwa” alisema Melrose.
Alisema
mtoto wa kike ana haki ya kusomeshwa na kuendelezwa badala ya kuachwa
nyumbani na kufanyiwa vitendo hivyo vinavyodumaza jamii kimaendeleo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Koshuma Mtengeti alisema
changamoto kubwa ni sheria ya makosa ya ukeketaji kuto kuwa na meno
kwani ni mtu mmoja tu aliyehukumiwa kati ya watu 43 waliobainika na
makosa hayo.
Filamu
hiyo imeandaliwa na ubalozi huo kwa kushirikiana na Jukwaa la Utu wa
Mtoto (CDF) na Mfuko wa Wanawake wa Afya, Utafiti na Maendeleo
(Forward)
Stanslaus Mabula alitaka Tamasha la Kushukuru
Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Nyamagana Stanslaus
Mabula ameiomba Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Kushukuru
linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwewnye ukumbi wa Diamond Jubilee
jijini Dar es Salaam, lihamie jijini Mwanza kwa lengo la kufikisha
shukrani kwa Mungu baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa
Kamati ya maandalizi, Alex Msama wanayafanyia kazi mapendekezo ya Mabula
ili kufanikisha tamasha hilo adhimu lenye nia ya kushukuru Mungu baada
ya uchaguzi Mkuu.
Msama alisema tamasha hilo
litashirikisha waimbaji mbalimbali wa muziki wa Injili ambao
watawasilisha ujumbe wa neno la Mungu kwa jamii baada ya uchaguzi Mkuu
uliofanyika kwa amani na utulivu.
Msama alisema Kamati yake
inajipanga kufikisha ujumbe wa Shukrani kwa Mungu kupitia viongozi wa
dini wakiwemo maaskofu na wachungaji wa makanisa mbalimbali hapa nchini.
“Tamasha la Kushukuru Mungu lina
mtazamo wa kufikisha asante kwa Mungu baada ya kuendelea kudumisha tunu
ya amani ambayo ndio sifa ya Tanzania nje ya mipaka,” alisema Msama.
Aidha Msama alitoa wito kwa Wadhamini na wafadhili kujitokeza kwa lengo la kusaidia tamasha hilo.
MH. KASSIM MAJALIWA NDIYE WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Hatimaye kitendawili kimeteguliwa
na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli
baada ya kumteua Mh. Kassim Majaliwa Mbunge wa Ruangwa mkoa wa Lindi na
Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi anayeshughulia elimu kuwa
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akitangaza jina hilo Spika wa
Bunge Mh. Job Ndugai amewaeleza wabunge kuwa kwa mujibu wa katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inampa rais kuteua jina la Waziri Mkuu
na kuliwasilisha bungeni kwa ajili ya kuthibitishwa na wabunge
Hivyo bunge litamthibitisha rasmi
na kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Fullshangwe na
kikosi chake chote kimatakia Mh. Waziri Mkuu Mteule Kassim Majaliwa
afya njema na mafanikio katika majukumu yake mapya.
GAPCO KUDHAMINI KILIMANJARO MARATHON KILOMITA 10 KWA WALEMAVU 2016
Meneja Masoko wa GAPCO Tanzania,
Caroline Kakwezi (Wa pili kutoka kushoto) akishiriki katika uzinduzi wa
Kilimanjaro Marathon 2016 ambapo GAPCO ilitangaza kudhamini mbio za
kilomita 10 kwa walemavu. Wengine kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa
Kampuni ya Bia Tanzania Oscar Shelukindo, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro
Pamela Kikuli, Mkurugenzi Msaidizi wa Michezo katika Wizara ya Habari,
Michezo na Utamaduni, Alex Nkenyenge na Meneja Mawasiliano wa Tigo John
Wanyancha.
Meneja Masoko wa GAPCO Tanzania,
Caroline Kakwezi (Wa tatu kutoka kushoto) akishiriki katika picha ya
pamoja mara baada ya kumaliza uzinduzi wa Kilimanjaro Marathon 2016
ambapo GAPCO ilitangaza kudhamini mbio za kilomita 10 kwa walemavu.
—————————————————
GAPCO, kampuni ya mafuta inayoongoza Tanzania imetangaza udhamini wake wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2016 kilomita 10 kwa walemavu.
—————————————————
GAPCO, kampuni ya mafuta inayoongoza Tanzania imetangaza udhamini wake wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2016 kilomita 10 kwa walemavu.
Akitangaza udhamini huo jana
wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo ya Kilimanjaro Marathon, Meneja
Masoko wa GAPCO Tanzania, Caroline Kakwezi alisema GAPCO inaona fahari
kudhamini mbio hizo za kilomita 10 kwa walemavu.
“Tumeshuhudia mbio hizi za
Kilimanjaro Marathon zikikua tangu tuanze kudhamini mwaka 2011 na pia
kufurahia faida wanayopata washiriki na jamii inayozunguka maeneo ambayo
mbio hizi hufanyika kila mwaka. Tunayo furaha kufanya kazi na Wild
Frontiers ambao ndio waandaaji wa mashindano haya,” alisema Kakwezi.
“Kama sehemu ya kusaidia jamii
ambayo tunafanya biashara, GAPCO Tanzania imeamua kusaidia wanariadha
ambao ni walemavu kwa kudhamini mbio ambazo wanashiriki walemavu pekee,”
alisema.
Alisema udhamini wa GAPCO pia
utahusisha usafiri, malazi na chakula kwa washiriki kutoka Dar es Salaam
na pia zawadi za pesa kwa washindi wa mbio hizo za kilomita 10 ambazo
zinafanyika pamoja na mbio nyingine za Kilimanjaro Marathon.
Kakwezi aliendelea kusema kuwa
Kilimanjaro Marathon limekua tukio kubwa linalovutia washiriki kutoka
ndani na nje ya Tanzania na hivyo limesaidia sana kutangaza vivutio vya
utalii kama vile Mlima Kilimanjaro na pia kuwaongezea kipato
wafanyabiashara wa Moshi.”.
WAZIRI MKUU KUJULIKANA LEO
Na Tiganya Vincent – MAELEZO
……………………………………….
Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaendelea na kikao chake mjini Dodoma kwa Spika wa Bunge hilo Mheshimiwa Job Ndugai kuendelea kuwaapisha Wabunge waliosalia.
Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaendelea na kikao chake mjini Dodoma kwa Spika wa Bunge hilo Mheshimiwa Job Ndugai kuendelea kuwaapisha Wabunge waliosalia.
Wakati zoezi hilo likiendelea ,shauku kubwa ya Waheshimiwa Wabunge na Watanzania ni kusubiri jina la atakayekuwa Waziri Mkuu.
Jina la Waziri Mkuu ajae
linatarajiwa kujulikana leo na hatimaye kupigiwa kura na wabunge mara
baada ya Spika kumtangaza rasmi kama mteule wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kushika wadhifa huo.
Mara baada ya zoezi la kupitishwa
kwa jina la Waziri Mkuu kupitishwa na Bunge Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli atamwapisha mjini Dodoma.
Waziri Mkuu atakaye teuliwa na Mheshimiwa Rais atakuwa ni wa 11 kushika wadhifa huo tangu mwaka 1961.
Mawaziri Wakuu waliowahi kushika
nafasi hiyo ni pamoja na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere( 1961-1962),
Mzee Rashid Mfaume Kawawa(1962,1972-1977),Edward Moringe
Sokoine(1977-1980,1983-1984), Cleopa David Msuya 1980-1983,1994-1995),
Dk. Salim Ahmed Salim 1984-1985), Joseph Sinde Warioba (1985-1990), John
Malecela (1990-1994), Fredrick Sumaye(1995-2005),Edward Lowassa
(2005-2008) na Mizengo Pinda (2008-2015)


No comments :
Post a Comment