Mkuu wa Shirika la Kimataifa la
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira
Rodrigues (kulia) akimwelezea Katibu Tawala, Halmashauri ya Wilaya ya
Ngorongoro, Lemuel Kristian Kileo (wa pili kushoto), namna mradi wa
ujenzi wa kituo cha sanaa ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya
ujasiliamali wa bidhaa zinazotokana na mifugo kwa akinamama na wasichana
kutoka Kata tano za Wilaya ya Ngorongoro utakavyotekelezwa juzi katika
Kijiji cha Ololosokwan. Wengine ni maofisa miradi kutoka UNESCO
wakishuhudia.
………………..
SHIRIKA la Kimataifa la Sayansi,
Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania linatarajia kutekeleza mradi
wa ujenzi wa kituo cha sanaa ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya
ujasiliamali wa bidhaa zinazotokana na mifugo kwa akinamama na wasichana
kutoka Kata tano za Wilaya ya Ngorongoro kama jitihada za kuongeza
kipato kwa familia za jamii ya Wamasai.
Akitoa maelekezo ya mradi huo juzi
katika Kijiji cha Ololosokwan mbele ya Katibu Tawala, Halmashauri ya
Wilaya ya Ngorongoro, Lemuel Kristian Kileo, Mkuu wa Shirika la
Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Bi. Zulmira
Rodrigues alisema mradi huo unatarajia kutekelezwa kuanzia Mwezi Agosti,
2015.
Bi. Rodrigues alimueleza Kileo
kuwa mradi huo unajumuisha ujenzi wa kituo cha kisasa cha sanaa ambacho
kitatumiwa na wajasiliamali wa jamii ya Kimasai kwa ajili ya kuuza bidha
zao za asili mbalimbali kwa watalii wanaofika kutembelea vivutio anuai
vya utalii ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro inayozunguka vijiji
hivyo.
Akifafanua zaidi juu ya mradi huo,
Ofisa Mradi Utamaduni wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na
Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Rehema Sudi alisema mradi huo
utajumuisha mafunzo ya ujasiliamali juu ya utengenezaji wa bidhaa za
ngozi, pembe za ng’ombe pamoja na shanga ili kuziongezea thamani na
kuuzwa kwa watalii anuai wanaotembelea vivutio na kukuza vipato vya
familia hasa akinamama.
Bi. Sudi aliongeza kuwa kata
zinazotarajia kunufaika na mafunzo na ujenzi wa kituo hicho cha kisasa
kwa ajili ya mauzo ya bidhaa hizo za asili za Wamasai ni pamoja na Kata
za Ololosokwani, Arash, Soit Sambu, Oloipili na Kata ya Aoliani
Magaidulu zote za Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro.
“…Mradi huu utajumuisha akinamama
na wasichana kutoka kata tano ambazo ni Ololosokwani, Arash, Soit Sambu,
Oloipili na Kata ya Aoliani Magaidulu, tutawapatia mafunzo juu ya
utengenezaji wa bidhaa mbalimbali zinazotokana na ngozi na pembe za
ng’ombe pamoja na shanga ikiwa ni hatua ya kuziongezea thamani kisha
kuziuza kwa watalii ambao wanatembelea vivutio vya utalii eneo hili hasa
Kijiji cha Ololosokwan,” alisema Ofisa Mradi Utamaduni Unesco, Bi.
Sudi.
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira
Rodrigues (kulia) akimuonesha Katibu Tawala, Halmashauri ya Wilaya ya
Ngorongoro, Lemuel Kristian Kileo (wa pili kulia) kompyuta ndogo mpakato
ambazo zimefungwa katika darasa moja maalumu kwa mafunzo mbalimbali kwa
watoto na wahitaji wengine. Darasa hilo ni sehemu ya mradi wa
kidijitali unaojumuisha Kliniki ya kisasa ya matibabu
ya macho na meno pamoja na huduma za uchunguzi magonjwa mbalimbali kwa kutumia fipimo vya ‘X-Ray’ na ‘Ultra-sound’ na shule ya kisasa kwa ajili ya mafunzo anuai Kijijini hapo.
ya macho na meno pamoja na huduma za uchunguzi magonjwa mbalimbali kwa kutumia fipimo vya ‘X-Ray’ na ‘Ultra-sound’ na shule ya kisasa kwa ajili ya mafunzo anuai Kijijini hapo.
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira
Rodrigues (kulia) akitembelea eneo la mradi wa Kijiji cha kidijitali
unaojumuisha Kliniki ya kisasa ya matibabu ya macho na meno pamoja na
huduma za uchunguzi magonjwa mbalimbali kwa kutumia vipimo vya ‘X-Ray’
na ‘Ultra- sound’ na shule ya kisasa kwa ajili ya mafunzo anuai Kijijini
hapo. Katikati ni Katibu Tawala, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro,
Lemuel Kristian Kileo pamoja na Ofisa Mradi Utamaduni wa Shirika la
UNESCO nchini Tanzania, Rehema Sudi wakikagua mradi huo.
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira
Rodrigues (kulia) akitembelea eneo la mradi wa Kijiji cha kidijitali
unaojumuisha Kliniki ya kisasa ya matibabu ya macho na meno pamoja na
huduma za uchunguzi magonjwa mbalimbali kwa kutumia fipimo vya ‘X-Ray’
na ‘Ultra- sound’ na shule ya kisasa kwa ajili ya mafunzo anuai Kijijini
hapo. Katikati ni Katibu Tawala, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro,
Lemuel Kristian Kileo pamoja na Ofisa Mradi Utamaduni wa Shirika la
UNESCO nchini Tanzania, Rehema Sudi wakikagua mradi huo.
Alisema wataalam na wabunifu
wataletwa katika vijiji vya mradi na kutoa mafunzo kwa akinamama na
wasichana kabla ya ujenzi wa kituo maalumu ambacho kitatumiwa na
wanufaika wa mafunzo hayo kama eneo la kuuzia bidhaa zao ikiwa ni sehemu
pia ya kulinda na kukuza tamaduni za jamii ya Wamasai. “…Tutazunguka na
kutoa mafunzo juu ya ubunifu na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali za
ngozi, pembe za ng’ombe pamoja na shanga na kutengeneza bidhaa za asili
kwa ajili ya kuziuza kwa wateja hasa watalii,” alisema Bi. Sudi.
Hata hivyo Ofisa huyo mradi
Utamaduni wa UNESCO alisema sehemu ya maandalizi ya mradi huo
unaotekelezwa kwa msaada wa UNESCO pamoja na washirika wengine ambao ni
Umoja wa Ulaya (EU) na Chuo Kikuu cha Liechtenstein na pia Chuo Kikuu
cha Ardhi cha Dar es Salaam imeanza kutekelezwa tangu Februari 2015.
Mbali na mradi huo UNESCO pia
inatekeleza mradi wa ujenzi wa Kijiji cha Dijitali, ambao unajumuisha
ujenzi wa Kliniki ya kisasa ya matibabu ya macho, Kliniki ya kisasa ya
matibabu ya meno pamoja na huduma za uchunguzi wa magonjwa mbalimbali
kwa kutumia fipimo vya ‘X-Ray’ na ‘Ultra-sound’ na shule ya kisasa kwa
ajili ya mafunzo anuai katika Kijiji cha Ololosokwan huduma
itakayosaidia jamii za wafugaji maeneo ya Ngorongoro.
Sehemu ya majengo ya mradi wa
Kijiji cha kidijitali unaojumuisha Kliniki ya kisasa ya matibabu ya
macho na meno, huduma za uchunguzi wa magonjwa mbalimbali kwa kutumia
vipimo vya ‘X-Ray’ na ‘Ultra- sound’ na shule ya kisasa kwa ajili ya
mafunzo anuai Kijijini hapo. Mradi huo unatekelezwa na Shirika la
Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania kwa
kushirikiana na wafadhili wengine ikiwemo kampuni ya Samsung Tanzania
Kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro.
Sehemu ya majengo ya mradi wa
Kijiji cha kidijitali unaojumuisha Kliniki ya kisasa ya matibabu ya
macho na meno, huduma za uchunguzi wa magonjwa mbalimbali kwa kutumia
vipimo vya ‘X-Ray’ na ‘Ultra- sound’ na shule ya kisasa kwa ajili ya
mafunzo anuai Kijijini hapo. Mradi huo unatekelezwa na Shirika la
Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania kwa
kushirikiana na wafadhili wengine ikiwemo kampuni ya Samsung Tanzania
Kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro.
Sehemu ya majengo ya mradi wa
Kijiji cha kidijitali unaojumuisha Kliniki ya kisasa ya matibabu ya
macho na meno, huduma za uchunguzi wa magonjwa mbalimbali kwa kutumia
vipimo vya ‘X-Ray’ na ‘Ultra- sound’ na shule ya kisasa kwa ajili ya
mafunzo anuai Kijijini hapo. Mradi huo unatekelezwa na Shirika la
Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania kwa
kushirikiana na wafadhili wengine ikiwemo kampuni ya Samsung Tanzania
Kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro.
Sehemu ya majengo ya mradi wa
Kijiji cha kidijitali unaojumuisha Kliniki ya kisasa ya matibabu ya
macho na meno, huduma za uchunguzi wa magonjwa mbalimbali kwa kutumia
vipimo vya ‘X-Ray’ na ‘Ultra- sound’ na shule ya kisasa kwa ajili ya
mafunzo anuai Kijijini hapo. Mradi huo unatekelezwa na Shirika la
Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania kwa
kushirikiana na wafadhili wengine ikiwemo kampuni ya Samsung Tanzania
Kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro.
TRA yakutana na Baraza la Maaskofu Tanzania Kuijadili sheria mpya ya Kodi
Afisa Mwandamizi Idara ya Huduma
na Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Rose
Mahendeka akiwasilisha Taarifa ya Sheria mpya ya Kodi ya ongezeko la
Thamani ya mwaka 2014 kwa viongozi wa Baraza la Maaskofu Tanzania na
kuwaeleza jinsi ilivyoziongelea jinsi ilivyozieleza Taasisi za Dini hasa
katika masuala ya ulipaji kodi, wakati wa Mkutano uliofanyika leo
Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Viongozi wa Dini
wakimsikiliza Bi. Rose Mahendeka alipokuwa anawasilisha Taarifa ya
Sheria mpya ya Kodi ya ongezeko la Thamani ya mwaka 2014, wakati wa
Mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Askofu Mkuu Paul Ruzoka wa Jimbo
la Tabora akichangia kwenye moja ya maeneo ya Sheria mpya ya Kodi ya
ongezeko la Thamani ya mwaka 2014, wakati wa Mkutano uliofanyika leo
Jijini Dar es Salaam.
Father Longino Rutagwelera wa Chuo
Kikuu cha Mtakatifu Agustino tawi la Mtwara akichangia kwenye moja ya
maeneo ya Sheria mpya ya Kodi ya ongezeko la Thamani ya mwaka 2014,
wakati wa Mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu
Katoliki Tanzania Fr. Raymond Saba akiongea na wajumbe wa Baraza hilo
waliohudhuria mkutano huo uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Afisa Mwandamizi Idara ya Huduma
na Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Rose
Mahendeka akiwaeleza jambo wajumbe wa baraza la Maaskofu Tanzania
wakati wa Mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Na Hassan Silayo-MAELEZO
Airtel yazindua ofa ya LUKU DAR ES SALAAM
Meneja
Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando (katikati) akizungumza na
waandishi wa Habari leo katika ofisi za Airtel jijini Dar Es Salaam Juni
23, 2015 wakati wa uzinduzi wa ofa kabambe itakayowazawadia wateja wa
Airtel nchini kupata Unit za bure za LUKU pindi watakaponunua LUKU
kupitia huduma ya Airtel Money (Kulia) Meneja wa Airtel Money.Steven
Kimea.
Meneja wa Airtel Money Steven Kimea (Kulia) akizungumza na waandishi wa
Habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa ofa kabambe
itakayowazawadia wateja wa Airtel nchini kujipatia nyongeza ya Unit za
bure za LUKU pindi watakaponunua LUKU kupitia huduma ya Airtel Money,
anayefwata kushoto ni Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson
Mmbando.
Picha na Philemon Solomon-Fullshangweblog
……………………………………………………
Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na shirika la umeme la (TANESCO) imezindua ofa kabambe itakayowazawadia wateja wake nchi nzima Unit za bure za Luku pindi watakaponunua LUKU kupitia huduma ya Airtel Money.
Ofa hii mpya ina lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma ya umeme na pia kuwazawadia wateja wa Airtel wanaonunua unit za LUKU kupitia huduma ya Airtel Money.
Akiongea kuhusu ofa hiyo, Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackosn Mmbandoalisema” Wateja wetu watazawadia unit LUKU za ziada Bure mara tu watakaponunua LUKU kupitia huduma ya Airtel Money. Tunaamini ofa hii inaendana na mahitaji na mwendendo wa maisha ya watanzania. Kwa sasa manunuzi ya umeme kupitia njia nyingine si tu yanaleta changamoto za kusafiri umbali mrefu na kupoteza muda mwingi kupata huduma bali husababisha watu kukaa foleni ndefu kusubiri kununua umeme. leo Airtel tunatoa ofa hii kwa wateja wetu na kuwawezesha kununua LUKU kwa urahisi wakiwa majumbani mwao pamoja na kunawazawadia kwa kuwapatia unit za Luku za ziada za bure”.
Aliongeza kwa kusema “ Airtel tunaendelea na dhamira yetu ya kutoa huduma za kibunifu zinazokithi na kutatua mahitaji ya wateja wetu , tukiwa na mawakala wa Airtel Money zaidi ya 45,000 nchini , wateja wetu wanafaidika na huduma ya mikopo, huduma za kuhamisha pesa, kutoa na kuweka pesa na nyingine nyingi.
Huduma ya Airtel Timiza inayotoa mikopo isiyo na dhamana kupitia simu za mkononi ni uthibitisho wa dhamira yetu ya kutoa huduma za kisasa zenye ubunifu kwa watanzania.” aliongeza Mmbando.
Rais Dkt. Jakaya Kikwete awatunuku Nishani watumishi wa umma walioliletea sifa Taifa
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete akiwa
katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi waliovishwa nishani
mbalimbali leo Jijini Dar es salaam.Kushoto ni Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman na kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi.
………………………………………………………………………..
Na Hassan Silayo
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo
amewavisha nishani mbalimbali watumishi wa Serikali kwa kutambua mchango
wao kitaifa.
Rais
Kikwete amefanya hivyo kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya sheria
ya mamlaka ya Rais (sura ya 9) kamailivyorekebishwa mwaka 2002 fungu la 4
kama ilivyotangazwa katika tangazo la serikali namba 227.
Nishani
zilizotunukiwa leo ni Nishani ya Jamhuri ya muungano Daraja la Kwanza,
Nishani ya Utumishi mrefu na Maadili mema Daraja la kwanza, Nishani ya
utumishi mrefu na Maadili mema Daraja la pili na Nishani ya Ushupavu.
Nishani hizo zinatunukiwa kwa watumishi ambao sifa zao zimekidhi mmatakwa ya nishani husika
KINANA AMALIZA ZIARA YAKE MISUNGWI LEO, KESHO NI JIMBO LA SUMVE
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katikati akiwa ameongozana na Nape
Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM wa pili kutoka kulia ni
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndugu Miraji Mtaturu wa pili kutoka kushoto
wakiingia kwenye kivuko cha MV Misungwi katika feri ya Busisi wakati
msafara wa Katibu mkuu huyo ukitoka wilaya ya Sengerema kuelekea Usagara
wilaya ya Misungwi mkani Mwanza ambapo ndipo alipopokelewa.
Leo
Kinana aliendelea na ziara yake katika jimbo la Misungwi linaloongozwa
na Mh. Charles Kitwanga ambaye pia ni naibu Waziri wa Nishati na Madini
akitembelea maeneo mbalimbali na kukagua utekelezaji wa Ilani ya
Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2015, inayotekelezwa na serikali ikiwa ni
pamoja na kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wananchi ili
kuzipatia ufumbuzi.
Akizungumza
katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Misungwi Nape Nnauye Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi amesema Chama cha Mapinduzi CCM kinaishauri
Serikali kuutoa na kuurudisha kwa wadau muswaada wa sheria ya habari
ambao umepelekwa bungeni kwa ajili ya kujadiliwa kwa, kuwa wadau
wanaulalamikia na wanataka kushirikishwa kuujadili ndipo uende bungeni
kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa kama sheria uli iweze kusainia na
Rais.
Ameongeza
kwamba “Sheria zinazotungwa ni kwa ajili ya wananchi hivyo Chama cha
Mapinduzi kinaishauri serikali kuwa, kama wadau wanaulalamikia muswaada
huo. Ni vyema ukarudhishwa kwa wadau ili ujadiliwe kwa pamoja na
serikali na wadau ndipo upelekwe Bungeni ukajadiliwe na kupitishwa
kama sheria”.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MISUNGWI-MWANZA)
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifuatana na Katibu wa CCM mkoa
wa Mwanza Miraji Mtaturu kupanda ngazi kwenda uneo la juu la kukaa
kwenye kivuko cha MV Misungwi leo asubuhi.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana naKatibu wa CCM mkoa
wa Mwanza Miraji Mtaturu na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi
CCM kuelekea eneo la kukaa kwenye kivuko cha MV Misungwi.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza jambo na Mbunge wa
jimbo la Sengerema Mh. William Ngeleja wakati msafara wake ukielekea
wilayani Misungwi kuendelea na ziara yake katika jimbo hilo mkoani
Mwanza
Vijana
wakijadili jambo wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
akielekea wilayani Misungwi kwa boti katika ziwa Victoria kutoka kushoto
ni Adam Mzee, Octavian Kimario aliyegeuka ni Msaidizi wa Katibu Mkuu
Edward Mpogolo, Suleiman Mwenda na Atley Kuni- Afisa habari Mwanza
Magari yakishuka kwenye kivuko baada ya kuvuka ziwa Victoria na kuingia Kigongo Feri wilaya ya Misungwi.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Katibu wa CCM mkoa
wa Mwanza Miraji Mtaturu katikati na Mbunge wa jimbo la Sengerema Mh.
William Ngeleja kushuka kwenye kivuko cha MV Misungwi mara baada ya
kuwasili Kigongo Feri wilayani Misungwi
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na mkuu wa mkoa wa
Mwanza Ndugu Magesa Mulongo mara baada ya kuwasili Kiogongo Feri
wilayani Misungwi.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozwa na mkuu wa mkoa wa
Mwanza Ndugu Magesa Mulongo kulia mara baada ya kuwasili Usagara wilaya
ya Misungwi ambapo alipokelewa katikati ni Mbunge wa jimbo la Misungwi
Mh. Charles Kitwanga maarufu “Mawe Matatu”
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia vikundi mbalimbali vya ngoma mara baada ya kupokelewa Usagara.
Mkuu
wa mkoa wa Mwanza Ndugu Magesa Mulongo akishiriki ujenzi wa zahanati ya
kijiji cha Nyang’omango wilayani Misungwi kulia ni mbunge wa jimbo hilo
Mh. Charles Kitwanga.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti wa kumbukumbu mara
baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa zahanati ya kijiji cha
Nyang’omango.
Mbunge
wa jimbo la Misungwi Mh. Charles Kitwanga akipanda mti wa Kumbukumbu
katika zahanati ya kijiji cha Nyang’omango wakati Kinana alipokagua
ujenzi wa zahanati hiyo.
Moja ya ofisi nzuri za CCM iliyojengwa katika kijiji cha Nyangomango
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua ofisi hiyo.
Wananchi
wakipalilia shamba la Dengu la wananchi katika kijiji cha Misasi ambapo
Katibu Mkuu Kinana na viongozi mbalimbali wamkoa wa Mwanza pia
walishiriki katika palizi hiyo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongoza viongozi wa mkoa wa
Mwanza na wilaya ya Misungwi pamoja na wananchi kushiriki kupalilia
shamba la wananchi la Dengu katika kijiji cha Misasi.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katikati, Mbunge wa jimbo la
Misungwi Mh. Charles Kitwanga, Mkuu wa mkoa wa Mwanza kushoto pamoja na
wananchi wakishiriki kupalilia shamba hilo.
Kikundi
cha ngoma kikitumbuiza wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu
Abdulrahman Kinana katika kijiji cha Mahando wilayani Misungwi.
Baadhi
ya vijana wakiwa na bango kubwa linalozungumzia kumrudisha tena mbunge
wao Mh. Charles Kitwanga katika ubunge wa jimbo la Misungwi katika
uchaguzi ujao.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa ameongozana na Mama Ntilie
wa Misungwi wakati alipowatembelea na kusomewa risala yao.
Mbunge
wa jimbo la Misungwi Mh. Charles Kitwanga akizungumza mafanikio
yaliyokwishapatikana katika uongozi wa awamu ya Nne ya CCM katika
mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Misungwi.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimuelezea jambo Katibu wa NEC
Itikadi na Uenezi Ndugu Nappe Nnauye huku Nape akionekana kufurahia
jambo hilo.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza akizungumza na wananchi katika mkutano huo.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nappe Nnauye akiwahutubia wananchi katika mkutano huo uliofanyika mjini Misungwi leo.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nappe Nnauye aksisitiza jambo wakati
akiwahutubia wananchi katika mkutano huo uliofanyika mjini Misungwi leo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Misungwi leo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati
akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini
Misungwi leo.
RAIS KIKWETE AMTUNUKU KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI, MBARAK ABDULWAKIL NISHANI YA UTUMISHI MREFU NA MAADILI MEMA DARAJA LA (I)
Rais Jakaya Kikwete (kushoto),
akimvisha Nishani ya Utumishi Mrefu na Maadili Mema Daraja la (I),
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil,
wakati wa sherehe ya kutunuku Nishani iliyofanyika kwenye Ukumbi mpya wa
Mikutano Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Rais Jakaya Kikwete (kushoto),
akimpongeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak
Abdulwakil, baada ya kumvisha Nishani ya Utumishi Mrefu na Maadili Mema
Daraja la (I), katika sherehe ya kutunuku Nishani iliyofanyika kwenye
Ukumbi mpya wa Mikutano Ikulu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (watatu kushoto) akiwa na baadhi ya
Watunukiwa wakiwa katika hafla hiyo wakati wakisubiri kutunukiwa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (wapili kwenda nyuma mstari wa kwanza)
akiwa na baadhi ya Watunukiwa wakiwa katika hafla hiyo wakati wakisubiri
kutunukiwa. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini,
(IGP) Ernest Mangu (kulia) akimpongeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil baada ya kutunukiwa Nishani ya
Utumishi Mrefu na Maadili Mema Daraja la (I) na Rais Jakaya Kikwete,
katika sherehe ya kutunuku Nishani iliyofanyika kwenye Ukumbi mpya wa
Mikutano Ikulu,
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini,
(CGP) John Minja (kulia) akimpongeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil baada ya kutunukiwa Nishani ya Utumishi
Mrefu na Maadili Mema Daraja la (I) na Rais Jakaya Kikwete.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya
Dar es Salaam, Suleiman Kova (kulia) akimpongeza Katibu Mkuu wa Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil baada ya kutunukiwa Nishani
ya Utumishi Mrefu na Maadili Mema Daraja la (I) na Rais Jakaya Kikwete.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kushoto) akiteta jambo na Mwakilishi
wa Shirika la Umoja wa Mtaifa la Kuhudumia Wakimbizi nchini (UNHCR),
Joyce Mends-Cole katika Ukumbi Mpya wa Mikutano Ikulu, jijini Dar es
Salaam, mara baada ya Rais Jakaya Kikwete kumtunukia Katibu Mkuu huyo,
Nishani ya Utumishi Mrefu na Maadili Mema Daraja la (I).
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (katikati) akiteta jambo na Mkuu wa
Jeshi la Magereza nchini, (CGP) John Minja (kulia) na Mkurugenzi wa Sera
na Mipango, wa Wizara hiyo, Haji Janabi, nje ya Ukumbi mpya wa Mikutano
Ikulu, jijini Dar es Salaam, mara baada ya Rais Jakaya Kikwete
kumtunuku Katibu Mkuu huyo, Nishani ya Utumishi Mrefu na Maadili Mema
Daraja la (I).
Rais Jakaya Kikwete (wanne kushoto
mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Watunukiwa wa Nishani
ya Utumishi Mrefu na Maadili Mema Daraja la Kwanza. Wakwanza kulia
mstari wa nyuma ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa
akijadiliana jambo na Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe wakati wa
kupiga kura bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha 2015/2016, Bungeni
mjini Dodoma Juni 23,2015 ( Kulia), Mbunge wa Mbunge wa Viti Maalum,
Mh. Anna Chilolo.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akipiga
kura ya ndio wakati bunge lilipokuwa likipitisha bajeti kuu ya serikali
kwa mwaka wa fedha 2015/2016, Bungeni mjini Dodoma ( Kulia), Mbunge wa
Mbunge wa Viti Maalum, Mh. Anna Chilolo.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa
(kushoto) akijadiliana jambo na Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mh. Mussa Azan
Zungu wakati wa kupiga kura bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha
2015/2016, Bungeni mjini Dodoma leo-juni 23, 2015.
MATUKIO KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA-JUNI 23,2015
Waziri wa Fedha, Saada Mkuya akihitimisha Hoja ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Fedha, Bungeni Mjini Dodoma Juni 23, 2015.
(Picha zote na ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa Mpanda Kati, Said Arfi, Bungeni mjini Dodoma.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Asiye na Wizara Maalum,
Profesa Mark Mwandosya na Mbunge wa kigoma Mjini Peter Serukamba kwenye
viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na
wabunge wa Viti Maalum, Anna Abdallah (kushoto) na Al Shymaa Kwegyir
wakitoka kwenye kumbi wa Bunge mjini Dodoma.
Kitendo kilichafanywa na Wajumbe wa CUF kutoka nje ya Baraza sio cha busara-WAZIRI Mohd Aboud
Na Kijakazi Abdalla / Maryam Kidiko -Maelezo Zanzibar
………………………………………………….
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
kupitia Chama cha Mapinduzi wamesikitishwa na kitendo cha wawakilishi
wenzao wa Chama cha Wananachi (CUF) kutoka nje ya kikao kilichojadili
mswada wa kupitisha matumizi ya Serikali kwa mwaka 2015/2016.
Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu
wa Pili wa Rais Mohd Aboud amesema kuwa kitendo kilichafanywa na
Wajumbe wa CUF kutoka nje ya Baraza sio cha busara na hakileti sura
nzuri ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa..
Amesema uamuzi waliochukuwa
wajumbe hao ni kukitia aibu chama hicho na kuwanyima haki wananchi
waliowachagua kuwaingiza ndani ya Baraza.
Waziri Aboud amesema kuwa
Serikali ya Mapinduzi ya Zazibar ina nia thabiti ya kufanya uchaguzi kwa
njia ya haki kwa wanannchi wote na sivyo kama wnavyofikiria
wawakilishi hao.
Amesema wakati huu ambapo
tunaelelekea katika uchaguzi mkuu wa mwezi wa Oktoba ilikuwa si busara
kuchukuwa hatua hiyo kwa vile hawakutumia sheria bali walitumia
siasa zaidi.
Wakichangia mswada huo baadhi ya
wawakilishi CCM wamewataka wananchi waliowachagua wawakilishi wa CUF
kuwakataa katika uchaguzi wa mwezi Oktoba kwa vile wameshindwa
kuwawakilisha vizuri katika vikao vya Baraza hilo tokea walipoingia
mwaka 2010.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
wa CUF wametoka nje ya Baraza kwa madai ya kutoridhika na zoezi zima la
uandikishaji wapiga kura linaloendelea Wilaya ya Magharibi A.
Akitoa taarifa baada ya kuanza
kikao cha asubuhi cha Baraza hilo huko Chukwani, nje kidogo ya mji wa
Zanzibar, mjumbe wa CUF Juma Duni Haji alisema kuwa wameamua kutoka nje
kutokana na kutokuwa na imani na zoezi la uandikishaji wapiga kura
linavyoendeshwa.
Alidai kuwa baadhi ya wanachama
wa CUF wenye sifa ya kuandikishwa wamekuwa wakunyimwa haki hiyo na
wamekuwa wakipigwa na askari wa vikosi vya SMZ wakati wakiwa njiani
kwenda kujiandikisha.
“Tumeshuhudia askari waliovaa
ninja (kufunika nyuso) wenye silaha katika mitaa wakiwakimbiza wananchi
wanaokwenda kujiandikisha kupiga kura,” alilalamika Juma Duni.
Pamoja na wajumbe hao kutoka nje
ya Baraza, Wajumbe wa Chama cha Mapinduzi CCM waliendelea kujadili na
kupitisha mswada wa matumizi ya fedha kwa mwaka 2015/2016 .
HABARI ZA KIMICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA TFF
Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania – TFF, Jamal Malinzi leo
ameagana rasmi na aliyekua kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania
(Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager,
mholanzi Mart Nooij.
Akiongea na waandishi wa habari
leo katika hoteli ya Tansoma, Malinzi amesema wameamua kuagana nae mbele
ya vyombo ya habari kama iliyofanyika pia wakati wa utambulisho wake
wakati wa kuanza kazi.
“Mpira wa miguu unachangamoto nyingi, watanzania tunasafari ndefu katika mafanikio ndio maana TFF imeanza kuwekeza katika soka la vijana, sababu ndio msingi wa kuwa na timu bora ya Taifa” alisema Malinzi.
“Mpira wa miguu unachangamoto nyingi, watanzania tunasafari ndefu katika mafanikio ndio maana TFF imeanza kuwekeza katika soka la vijana, sababu ndio msingi wa kuwa na timu bora ya Taifa” alisema Malinzi.
Duniani kote chimbuko la timu
bora ni soka la vijana na watoto, tukiwa na vijana wengi walioanza
kucheza mpira katika umri mdogo wanapofikia umri wa kuchezea timu ya
Taifa tutakua na kikosi bora.
Nchi za wenzetu inapofikia kocha
kuita wachezaji wa timu ya Taifa anakuwa na wigo mpana, kwetu sisi
wachezaji wanocheza soka nje ya nchi wanahesabika, hivyo ni lazima
tuanze kuwekeza kwenye soka la vijana
TFF ilishaanza mkakati huo ndio
maana kuna timu za U13, U15 ambazo zitakua zikiingia kambini na kucheza
michezo ya kirafiki ndani ya nje kwa lengo la kupata uzoefu kabla ya
kushiriki kuwania kufuzu kwa fainali za vijana mwaka 2016.
Kikosi cha U15 kinatarajiwa
kufanya ziara mwezi Disemba mwaka huu katika nchi za Malawi, Zambia,
Zimbambwe, Botswana na Afrika Kusini, kisha mwakani mwezi April 2016
kitaenda Rwanda, Burundi, Uganda na Kenya kucheza michezo ya kirafiki.
Naye Mart Nooij aliyekua kocha wa
Taifa Stars, akiongea na waaandishi wa habari alisema anawashukuru
watanzania wote, serikali, wadau wa mpira wa miguu nchini na TFF kwa
sapoti waliyompatia wakati akiwa kocha mkuu wa timu ya Taifa.
Nooij alisema alifurahia maisha
yake akiwa Tanzania kwa kipindi chote alichokua akifundisha timu ya
Taifa, lakini kwa sababu imefikia mwisho wa ajira yake hana jinsi
anaondoka, lakini ataendelea kuikumbuka Tanzania na watanzania wote kila
siku kwa ukarimu wao.
Wakati huo huo Rais wa TFF. Jamal
Malinzi amemtangaza Charles Mkwasa kuwa kocha mpya wa Taifa Stars
akisaidiwa na kocha Hemed Morocco, Mkwasa ambaye ni kocha wa Yanga na
Morocco kocha wa Mafunzo watafanya kazi kwa kipindi cha miezi mitatu
ambayo timu ya taifa itakua na michezo ya kuwania kufuzu kwa CHAN na
AFCON.
Malinzi amesema uteuzi wa makocha
hao wazawa umezingatia vigezo vya makocha wa timu ya Taifa kuwa na
leseni A ya ukocha kutoka CAF au zinazofanana kutoka mashiriksho mengine
duniani wanaozifanyia kazi, jambo ambalo makocha hao wazawa wamekizi.
Kocha Mkwasa atakua akipewa
hudumu zote na masilahi (zikiwemo posho) alizokuwa anapewa kocha
aliyeondoka, pia amepewa nafasi ya kuchagua benchi lake la ufundi la
kufanya nalo kazi, hivyo nawaomba wadau wa mpira wa miguu na watanzania
kwa ujumla tuwape sapoti makocha hao wazawa” aliongeza Malinzi”
Aidha Kamati ya utendaji ya TFF
Iimemteua Alhaj Ahmed Mgoyi kuwa mratibu wa timu ya Taifa, lengo la
uteuzi huo wa Mgoyi ni kuwa kiunganishi kati ya kamati ya Utendaji na
timu ya Taifa.
U15 YAINGIA KAMBINI
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 15 ya Tanzania, imeingia kambini jana na kuanza mazoezi leo katika uwanja wa Karume kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya kombaini U15 ya mkoa wa Mbeya siku ya jumapili.
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 15 ya Tanzania, imeingia kambini jana na kuanza mazoezi leo katika uwanja wa Karume kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya kombaini U15 ya mkoa wa Mbeya siku ya jumapili.
Kikosi hicho kilicho chini ya
makocha Bakari Shime na Peter Manyika kitacheza mchezo huo kwa lengo la
waalimu kupatawa fursa ya kuwaona vijana hao na kuwaongeza wengine
watakaoneka katika kikosi hicho.
U15 ni mpango wa TFF kuandaa
kikosi kizuri chenye ubora kuelekea kuwania kufuzu ka fainali za vijana
Afrika mwaka 2017 zitakazofanyika nchini Madagascar, ambapo vijana hao
watakua na umri wa miaka 16 kufikia mwakani wakati michezo ya kuwania
kufuzu itakaponza mwezi Julai, 2016.
BONDIA WA KIKE MWANNE HAJI AWATAKA MABONDIA WA DAR ES SALAAM
……………
BONDIA wa kike Mwanne Haji
ambaye amejitokeza kupambana na mabondia kwa kike wa Dar es salaam baada
ya kuwasumbuwa sana mabondia wenzake wanaotoka Chunya Mkoa wa Mbeya na
sasa kujikita katija jiji lakitokea katika GYM ya Zugo iliyopo
Gongolamboto
bondia uyo wa kike ambaye amesha
panda uringoni kupambana na baadhi ya mabondiwa wa mkoani amesema
amekuja kwa ajili ya mchezo wa msumbwi jijini hivyo mabondia wa kike
wakae pembeni kwani sasa ata wasambalatisha mmoja baada ya mwingine
alitolea mfano wa mabondia
wanaotamba Dar es salaam kwa kupigana wenyewe kwa wenyewe kila wakati ni
Lulu Kayage,Halima Ramadhani, Fatuma Yazidu
sasa wakae foleni kwani atawapa
vipigo mmoja baada ya mwingine bondia uyo mpaka sasa amecheza michezo
mitatu ambapo mchezo wake wa kwanza alicheza na Vailet Modest na
kufanikiwa kumtwanga kwa point mchezo wake wa pili alicheza na Telesia
Kiwale na mchezo wake wa tatu alicheza na Jennifer Pius na
kumsambalatisha kwa pointi
hivyo amewaomba mapromota wajitokeza kumsaidi kupambanishwa na mambondia aliowataja hapo juu kwa uzito wa kg 49
mbali na hivyo ametowa wito kwa
tasisi mbalimbali pamoja na kmpuni kujitokeza kudhamini mchezo wa
masumbwi kwani unapendwa na mashabiki lukuki nchini
Chama cha wasambazaji wa filamu Tanzania wasitisha kukununua stika za TRA na kupeleka filamu zao Bodi ya filamu kwaajili ya kufanyiwa ukaguzi
Mwenyekiti wa kikosi kazi kutoka chama cha wasambazaji wa filamu Tanzania,Bw Moses Mwanyilu akionyesha baadhi ya filamu ambazo zinauzwa nchini bila kupata kibali kutoka bodi ya filamu Tanzania na kutokuwa na stika za ushuru za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakati wa mkutano na waandishi wa habari wakielezea changamoto zao kuhusiana na filamu za kitanzania kulazimishwa kukaguliwa na bodi ya filamu na kuwekwa stika za TRA ilhali filamu za nje hazifanyiwi hivyo na kupelekea filamu za kitanzania kutokuwa na ushindani sokoni.
Mwenyekiti wa kikosi kazi kutoka chama cha wasambazaji wa filamu Tanzania,Bw Moses Mwanyilu akionyesha filamu kutoka nje ambayo inasemekana kuwa na maadili yasiofahaa kutazamwa na watoto chini ya miaka 18 ambayo inaendelea kuuzwa nchini huku ikiwa haijakaguliwa na bodi ya filamu wala haina stika za TRa kitu ambacho kimekuwa kikiwaumiza watayarishaji na wauzaji wa filamu za kitanzania ambazo zimekuwa na mlolongo mrefu hadi kuingia sokoni.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa makini kuandika kile kinachozungumzwa.
Mjumbe wa chama cha wasambazaji wa filamu Tanzania, Bw Saleh Abdallah akizungumzia kauli moja waliyokubaliana kama wasambazaji kuwa Kuanzia tarehe 1 Julai 2015 wao kama watayarishaji na wasambazaji wa kazi za filamu Tanzania wamesitisha swala la kupeleka filamu zao bodi ya filamu kwaajili ya kukaguliwa wala kununua stika za TRA mpaka pale mamlaka husika zitakapokaa chini na kujadiliana kuhusu swala hili.
……………………………………………………….
HABARI PICHA- NA LUKAZABLOG
HABARI PICHA- NA LUKAZABLOG
Chama cha
wasambazaji wa kazi za filamu Tanzania leo wamekutana na waandishi wa
habari kuelezea nia yao ya kusitisha kupeleka filamu zao bodi ya filamu
Tanzania kwaajili ya kukaguliwa huku wakielezea sababu kuwa Bodi ya
filamu imekua ikikagua filamu za Tanzania tu huku zile za nje zikiwa
hazikaguliwi na kupelekea kuwaumiza wao katika soko la filamu.
Vilevile
wamesitisha zoezi la kununua stika za TRA kutokana na sababu kuwa kazi
nyingi za nje hazina stika na pia maafisa wa TRA wakipita kukagua filamu
wanachukua za Tanzania tu ambazo hazina stika huku wakiziacha zile
zinazotoka nje na zile zinaharamiwa huku sheria ya filamu ya mwaka 2012
ikisema kuwa filamu zote ziwe za nje au za ndani zinatakiwa kukaguliwa
na kupewa daraja.
Kutokana na sababu ambazo chama cha wasambazaji wamezieleza kuwa Pamoja na kuwaandikia barua Mamalaka ya Mapato Tanzania na Bodi ya Filamu kuhusiana na swala hilo hawakuweza kupatiwa majibu ya barua yao na ndipo walipoamua kusitisha kununua stika na kupeleka filamu zao bodi kwaajili ya kukaguliwa mpaka watakapokaa meza moja huku wakiendelea kupeleka filamu sokoni.
Kutokana na sababu ambazo chama cha wasambazaji wamezieleza kuwa Pamoja na kuwaandikia barua Mamalaka ya Mapato Tanzania na Bodi ya Filamu kuhusiana na swala hilo hawakuweza kupatiwa majibu ya barua yao na ndipo walipoamua kusitisha kununua stika na kupeleka filamu zao bodi kwaajili ya kukaguliwa mpaka watakapokaa meza moja huku wakiendelea kupeleka filamu sokoni.
Simbachawene -ataka ushirikiano kwa wananchi atekeleze majukumu ya Wizara
Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mwilowe,
Wilaya ya Mpwapwa, baada kuzuia msafara wake wakati alipopita katika
Kijiji hicho wakati wa ziara ya kukagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme
Vijijini Awamu ya Pili unaofadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
na Kutekelezwa na Shirika la Umeme Nchini, (TANESCO). Wanakijiji hao
walimweleza Waziri kuwa kijiji chao pia kiunganishwe na umeme.
2. Wananchi wa Kijiji cha Mwilowe
wakizuia msafara wa Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene
wakitaka kijiji hicho pia kiunganishwe na nishati hiyo. Waziri alikua
katika ziara ya kutembelea na kukagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme
Vijijini unaofadhiliwa na wakala wa Nishati Vijijini (REA) na
kutekelezwa na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO).
3. Baadhi ya akina mama wa Kijiji
cha Lukole, Wilaya ya Mpwapwa wakishangilia baada ya Waziri wa Nishati
na Madini, George simbachawene kuwahakikishia kukiunganisha Kisima cha
maji kijijini hapo na Nishati ya Umeme.
Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene akimsikiliza Mwananchi katika moja ya mikutano yake
na wananchi wakati akikagua utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini Awamu
ya Pili, katika Kijiji cha Malolo, Wilaya ya Mpwapwa.
Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene akiangalia mfano wa mashine ya kusaga inayotumia
umeme wa mota aliyotengenezwa na Kijana katika Kijiji cha Lukole.
Simbachawene aliahidi kumsaidia Kijana hiyo kuweza kufikia lengo lake.
Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene akizindua Albam ya nyimbo ya Kwaya ya Mtakatifu
Agustino katika Kijiji cha Kingiti, Kigango cha Kingiti, wilaya ya
Mpwapwa wakati wa ziara yake ya kukagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme
Vijijini, Awamu ya Pili.
8. Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene akionesha Album ya nyimbo ya Kwaya ya Mtakatifu
Agustino katika Kigango cha Kingiti, kijiji cha Kingiti baada ya
kuzindua Albam hiyo. Simbachawene alizindua album hiyo wakati wa ziara
yake ya kukagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini, Awamu ya Pili.
Waziri wa Nishati na Madini,
George simbachawene akishiriki kucheza ngoma ya Kabila la Wagogo wakati
wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Umeme Vijijini, Awamu ya Pili
katika Kijiji cha Malolo, Wilaya ya Mpwapwa, Mkoani Dodoma.
10. Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene akimkabidhi baskeli , Diana Kalenza, katika kijiji
cha Idodoma, Wilaya ya Mpwapwa wakati wa ziara yake ya kukagua
Utekelezaji wa Mradi wa Umeme vijijini, Awamu ya Pili. Kwa mujibu wa
Simbachawene baiskeli hiyo imetengenezwa na SIDO, Dar es Salaam.
11. Mmoja wa wananchi katika
kijiji cha Malolo akiimba wimbo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene wakati wa ziara ya Waziri katika Kijiji chicho.
Wimbo huo uliokuwa na ujumbe wa kumwomba waziri kukiunganisha Kijiji
hicho. Aidha, wimbo huo ulieleza namna wanakijiji hao watakavyotumia
nishati hiyo kwa maendeleo yao.
…………………………………………………………..
Na Asteria Muhozya, Mpwapwa
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene amewataka
wananchi kuwapa ushirikiano viongozi wa Wizara hiyo ili waweze
kutekeleza kikamilifu majukumu yao kutokana na kusimamia rasilimali
muhimu zinazobeba uchumi wa nchi.
Simbachawene aliyasema hayo kwa nyakati tofauti wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini unafadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), na kutekelezwa na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), katika vijiji vya Kinusi, Nzugilo, Idodoma, Malolo na Lukole, Wilaya ya Mpwapwa, Mkoani Dodoma.
“Tuko kwa ajili ya kuwatumikia wananchi. Tunataka mshuhudie mafanikio makubwa ya usambazaji umeme vijijini. Serikali inatambua umuhimu wa nishati hii kwa maendeleo,na tutahakikisha kuwa, tunavifikia vijiji zaidi katika Awamu ya Tatu”, alieleza Simbachawene.
Simbachawene aliongeza kuwa, Mradi wa usambazaji Umeme Vijijini ni endelevu na kuongeza kuwa, hivi sasa , serikali imezifikia takriban Kata na Tarafa nyingi nchini na kuongeza kuwa, serikali itahakikisha inayafikia maeneo mengi zaidi yakiwemo yale yenye huduma muhimu za kijamii zikiwemo zahanati, shule na visima vya maji.
Aidha, alisema wizara yake iko kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wote kuhakikisha kwamba wananufaika na rasilimali anazozisimamia bila kujali itikadi za vyama na hivyo kuwaomba wananchi kuonesha ushirikiano wakati serikali inapotekeleza Mradi huo wa usambazaji umeme Vijijini.
“Tuo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na si kwa kuangalia itikadi za vyama.Tutawatumikia wananchi wote bila kupokea rushwa kwa kuwa tunao uwezo wa kuwatumikia , nia tunayo, tunachotaka ni ushirikiano wenu”, alisema Simbachawene.
Katika hatua nyingine Simbachawene amepiga marufuku uchimbaji wa madini katika vyanzo vya maji na kueleza kuwa, wote watakaobainika kuchimba madini katika vyanzo hivyo, watafutiwa leseni zao za uchimbaji madini.
“ Sheria ya madini, kanuni na taratibu zake haziruhusu kuchimba madini katika vyanzo vya maji, kwa yeyote atakaebainika kuchimba madini katika vyanzo hivyo, tutamfutia leseni kwa kufuata taratibu na kanuni hizo”,alisistiza Simbachawene.
Simbachawene aliyasema hayo kwa nyakati tofauti wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini unafadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), na kutekelezwa na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), katika vijiji vya Kinusi, Nzugilo, Idodoma, Malolo na Lukole, Wilaya ya Mpwapwa, Mkoani Dodoma.
“Tuko kwa ajili ya kuwatumikia wananchi. Tunataka mshuhudie mafanikio makubwa ya usambazaji umeme vijijini. Serikali inatambua umuhimu wa nishati hii kwa maendeleo,na tutahakikisha kuwa, tunavifikia vijiji zaidi katika Awamu ya Tatu”, alieleza Simbachawene.
Simbachawene aliongeza kuwa, Mradi wa usambazaji Umeme Vijijini ni endelevu na kuongeza kuwa, hivi sasa , serikali imezifikia takriban Kata na Tarafa nyingi nchini na kuongeza kuwa, serikali itahakikisha inayafikia maeneo mengi zaidi yakiwemo yale yenye huduma muhimu za kijamii zikiwemo zahanati, shule na visima vya maji.
Aidha, alisema wizara yake iko kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wote kuhakikisha kwamba wananufaika na rasilimali anazozisimamia bila kujali itikadi za vyama na hivyo kuwaomba wananchi kuonesha ushirikiano wakati serikali inapotekeleza Mradi huo wa usambazaji umeme Vijijini.
“Tuo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na si kwa kuangalia itikadi za vyama.Tutawatumikia wananchi wote bila kupokea rushwa kwa kuwa tunao uwezo wa kuwatumikia , nia tunayo, tunachotaka ni ushirikiano wenu”, alisema Simbachawene.
Katika hatua nyingine Simbachawene amepiga marufuku uchimbaji wa madini katika vyanzo vya maji na kueleza kuwa, wote watakaobainika kuchimba madini katika vyanzo hivyo, watafutiwa leseni zao za uchimbaji madini.
“ Sheria ya madini, kanuni na taratibu zake haziruhusu kuchimba madini katika vyanzo vya maji, kwa yeyote atakaebainika kuchimba madini katika vyanzo hivyo, tutamfutia leseni kwa kufuata taratibu na kanuni hizo”,alisistiza Simbachawene.
Kongamano la Huawei Cloud Conference lafanyika Dar es salaam
Katibu mkuu wa Wizara ya Sayansi
Pro. Patrick Makungu Md of Huawei Tanzania Bw. Zhan Yongquan
anayeshuhudia ni balozi wa china nchini Tanzania, Waziri wa Mawasiliano
Sayansi na technolojia na waziri wa afya wa Zanzibar. bw kombo,
wakisaini mkataba wa makubaliano kati yao ikiipa nafasi kampuni ya
Huawei Tanzania kua moja ya washauri wa mambo ya TEHAMA nchini.
Waziri wa Wizara ya Sayansi pro.
Makame Mbawara akielezea Data Center iliyojengwa hapa Tanzania kwa
waandishi wa habari. Pembeni yake ni Director wa ICT Dr. Ally Simba,
Mr. Jiang Xin (Product Manager wa Huawei Enterprises) akielezea Data Center.
………………………………………………………..
Kampuni ya Huawei Tanzania
ikishirikiana na Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia wameandaa
kongamano la kwanza la sekta ya TEHAMA (ICT) ijulikanayo kama Huawei
Cloud Conference kwenye ukumbi wa Julius Nyerere International
Convention Centre (JNICC).
Kongamano hili liliwakutanisha wadau wote wa TEHAMA (ICT) nchini, wakiwemo wa serikali na wa sekta binafsi na lilizinduliwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Balozi wa China nchini Tanzania Bw. Lv Youquin, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof Patrick Makungu pamoja na usimamizi wa makampuni shirika ya Huawei Tanzania kutoka; Airtel, Viettel, Tigo, Vodacom, na TTCL.
Katika Kongamano hilo la mada “Rahisisha Teknolojia, Rahisisha Biashara” ilizungumziwa hali ya sasa ya sekta ya TEHAMA, sera zake pamoja na kupanga jinsi ya kuiendeleza sekta hii nchini ili kufikia malengo ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia ya millenia ya 2025 ambayo ni kuendeleza Tanzania kupitia TEHAMA.
Katika kongamano hili kampuni ya Huawei Tanzania (ambao ni wabunifu wakubwa wa bidhaa na huduma za TEHAMA) pamoja na Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia walitia sahihi mkataba wa makubaliano kati yao huku ikiipa nafasi kampuni ya Huawei Tanzania kua moja ya washauri wa mambo ya TEHAMA nchini.
Baada ya kutia sahihi, Kampuni ya Huawei Tanzania ilielezea mipango yake ya kuendeleza na kukuza mawasiliano nchini Tanzania kwa kukuza sekta ya TEHAMA na kutoa elimu serikalini, mashuleni na kwa wananchi wote kwa ujumla kuhusu sekta iyo.
Tanzania imekua ikifanya kazi kwa karibu sana na Kampuni ya Huawei Tanzania na kwa mda wote kampuni hii imeshirikiana na wizara kwa karibu sana. Utiaji sahihi wa makubaliano ya kushirikiana katika shughuli za TEHAMA ni ushuhuda tosha wa jinsi Huawei Tanzania inavyojali sekta ya TEHAMA nchini na itaendeleza kukuza teknolojia hiyo nchini.
Akizungumza katika Kongamano hilo, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Technolojia, Prof. Makame Mbarawa alisema, “TEHAMA inachangia sana katika maendeleo ya Uchumi ya nchi kwani inawezesha mambo kufanyika kwa ufanisi zaidi. Wizara na serikali kwa ujumla imekuwa na mahusinao mazuri na Kampuni ya Huawei Tanzania, na tumesha shirikiana katika miradi mingi. Pamoja na ubunifu wake katika sekta ya TEHAMA, Huawei imechangia sana katika mambo mbali mbali nchini Tanzania. Kufikia kwenye Mkataba wa Makubaliano kati ya Wizara na Huawei ni ishara ya ubora wa kazi ambayo kampuni hii, na itaendeleza ubadilishinaji wa teknolojia kati ya Huawei na Tanzania. Huawei imechangia pakubwa katika ukuaji wa sekta ya TEHAMA nchini Tanzania.
Naye Balozi wa China nchini Tanzania Bw. Lv Youquin alisema, “ Kwa mda mrefu Tanzania na China wamekua na mahusiano mazuri hususan baada ya ujio wa raisi wa china bwa. Xi Jinping mwaka 2013; Kampuni nyingi za kichina zimekuja Tanzania kuwekeza na kukuza nchi. Kama kiongozi wa mambo ya TEHAMA duniani, Huawei imewekeza nchini Tanzania kwa Zaidi ya miaka 17 na kwa muda wote huo imetoa ajira nyingi kwa watanzania pamoja na kuwekeza kwenye shughuli za kijamii nchini, na kuwa mfani wa kuiga katika maswala ya kidiplomasia kati ya Tanzania na China.
Katika hotuba yake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof Patrick J Makingu aliwapongeza Huawei kwa mchango wao katika kujenga Tanzania bora kupitia TEHAMA na kuwasihi makampuni mengine ya TEHAMA kuiga mfano wa Huawei. Aliendelea kwa kusema, “Huawei imekuwa ikijikita katika kutafuta suluhisho mpya katika sekta ya TEHAMA duniani. Awali mwaka huu, Huawei ilihusika katika Kongamano la Mobile World Congress mjini Barcelona nchini Uhispania ambapo walikuwa moja kati ya mashirika makubwa kufanya maonyesho ya bidhaa zake mpya na sisi kama Wizara tunajivunia kufanya kazi nao”.
Naye Mtendaji Mkuu wa Huawei Tanzania Bw. Zhang Yongquan alisema “Kampuni ya Huawei Tanzania imekuwepo nchini kwa takribani miaka 17 na imejishughulisha katika shughuli mbalimbali za kujenga nchi ikiwepo shughuli za kijamii hususani kwenye michango vyuoni na mahospitalini. Bw. Zhang Yongquan, aliendelea kwa kusema “Tunashukuru serikali ya Tanzania pamoja na wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kwa kuendelea kuiunga mkono kampuni yetu”.
Katika kongamano hilo, kampuni ya Huawei Tanzania ilizindua bidhaa zake mpya Oceanstor V3 and Fusioncube. Pia imeonyesha Truck yao inayozunguka nchi mbalimbali kila mara moja kwa mwaka ikianzania nchini China, na kwa mwaka huu truck hili linazunguka kusini na magharibi mwa bara la Afrika.
Kampuni ya Huawei Tanzania inaongoza katika sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano nchini Tanzania na imekua ikishirikiana na wadau wengine wa mawasiliano kama Tigo, Vodacom, Airtel, Zantel na TTCL katika kuchangia ukuaji wa watu binafsi kwenye hii sekta (ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano).
Kongamano hili liliwakutanisha wadau wote wa TEHAMA (ICT) nchini, wakiwemo wa serikali na wa sekta binafsi na lilizinduliwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Balozi wa China nchini Tanzania Bw. Lv Youquin, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof Patrick Makungu pamoja na usimamizi wa makampuni shirika ya Huawei Tanzania kutoka; Airtel, Viettel, Tigo, Vodacom, na TTCL.
Katika Kongamano hilo la mada “Rahisisha Teknolojia, Rahisisha Biashara” ilizungumziwa hali ya sasa ya sekta ya TEHAMA, sera zake pamoja na kupanga jinsi ya kuiendeleza sekta hii nchini ili kufikia malengo ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia ya millenia ya 2025 ambayo ni kuendeleza Tanzania kupitia TEHAMA.
Katika kongamano hili kampuni ya Huawei Tanzania (ambao ni wabunifu wakubwa wa bidhaa na huduma za TEHAMA) pamoja na Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia walitia sahihi mkataba wa makubaliano kati yao huku ikiipa nafasi kampuni ya Huawei Tanzania kua moja ya washauri wa mambo ya TEHAMA nchini.
Baada ya kutia sahihi, Kampuni ya Huawei Tanzania ilielezea mipango yake ya kuendeleza na kukuza mawasiliano nchini Tanzania kwa kukuza sekta ya TEHAMA na kutoa elimu serikalini, mashuleni na kwa wananchi wote kwa ujumla kuhusu sekta iyo.
Tanzania imekua ikifanya kazi kwa karibu sana na Kampuni ya Huawei Tanzania na kwa mda wote kampuni hii imeshirikiana na wizara kwa karibu sana. Utiaji sahihi wa makubaliano ya kushirikiana katika shughuli za TEHAMA ni ushuhuda tosha wa jinsi Huawei Tanzania inavyojali sekta ya TEHAMA nchini na itaendeleza kukuza teknolojia hiyo nchini.
Akizungumza katika Kongamano hilo, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Technolojia, Prof. Makame Mbarawa alisema, “TEHAMA inachangia sana katika maendeleo ya Uchumi ya nchi kwani inawezesha mambo kufanyika kwa ufanisi zaidi. Wizara na serikali kwa ujumla imekuwa na mahusinao mazuri na Kampuni ya Huawei Tanzania, na tumesha shirikiana katika miradi mingi. Pamoja na ubunifu wake katika sekta ya TEHAMA, Huawei imechangia sana katika mambo mbali mbali nchini Tanzania. Kufikia kwenye Mkataba wa Makubaliano kati ya Wizara na Huawei ni ishara ya ubora wa kazi ambayo kampuni hii, na itaendeleza ubadilishinaji wa teknolojia kati ya Huawei na Tanzania. Huawei imechangia pakubwa katika ukuaji wa sekta ya TEHAMA nchini Tanzania.
Naye Balozi wa China nchini Tanzania Bw. Lv Youquin alisema, “ Kwa mda mrefu Tanzania na China wamekua na mahusiano mazuri hususan baada ya ujio wa raisi wa china bwa. Xi Jinping mwaka 2013; Kampuni nyingi za kichina zimekuja Tanzania kuwekeza na kukuza nchi. Kama kiongozi wa mambo ya TEHAMA duniani, Huawei imewekeza nchini Tanzania kwa Zaidi ya miaka 17 na kwa muda wote huo imetoa ajira nyingi kwa watanzania pamoja na kuwekeza kwenye shughuli za kijamii nchini, na kuwa mfani wa kuiga katika maswala ya kidiplomasia kati ya Tanzania na China.
Katika hotuba yake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof Patrick J Makingu aliwapongeza Huawei kwa mchango wao katika kujenga Tanzania bora kupitia TEHAMA na kuwasihi makampuni mengine ya TEHAMA kuiga mfano wa Huawei. Aliendelea kwa kusema, “Huawei imekuwa ikijikita katika kutafuta suluhisho mpya katika sekta ya TEHAMA duniani. Awali mwaka huu, Huawei ilihusika katika Kongamano la Mobile World Congress mjini Barcelona nchini Uhispania ambapo walikuwa moja kati ya mashirika makubwa kufanya maonyesho ya bidhaa zake mpya na sisi kama Wizara tunajivunia kufanya kazi nao”.
Naye Mtendaji Mkuu wa Huawei Tanzania Bw. Zhang Yongquan alisema “Kampuni ya Huawei Tanzania imekuwepo nchini kwa takribani miaka 17 na imejishughulisha katika shughuli mbalimbali za kujenga nchi ikiwepo shughuli za kijamii hususani kwenye michango vyuoni na mahospitalini. Bw. Zhang Yongquan, aliendelea kwa kusema “Tunashukuru serikali ya Tanzania pamoja na wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kwa kuendelea kuiunga mkono kampuni yetu”.
Katika kongamano hilo, kampuni ya Huawei Tanzania ilizindua bidhaa zake mpya Oceanstor V3 and Fusioncube. Pia imeonyesha Truck yao inayozunguka nchi mbalimbali kila mara moja kwa mwaka ikianzania nchini China, na kwa mwaka huu truck hili linazunguka kusini na magharibi mwa bara la Afrika.
Kampuni ya Huawei Tanzania inaongoza katika sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano nchini Tanzania na imekua ikishirikiana na wadau wengine wa mawasiliano kama Tigo, Vodacom, Airtel, Zantel na TTCL katika kuchangia ukuaji wa watu binafsi kwenye hii sekta (ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano).
SERIKALI YA MAREKANI YAZINDUA MRADI WA DOLA MILIONI 14.5 WA KULINDA MAZINGIRA,KUKUZA UHIFADHI NA UTALII NCHINI TANZANIA
Balozi wa Marekani nchini
Tanzania Mark Childress akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa PROTECT
wa dola za kimarekani Milioni 14.5 wa kulinda mazingira,kukuza uhifadhi
na utalii nchini hapa unaolenga kujenga uwezo wa uhifadhi na
kukabiliana na ujangili na usafirishaji haramu wa wanyamapori nchini
kote Tanzania,uzinduzi huu ulifanyika jana katika eneo la hifadhi ya
wanyamapori linalosimamiwa na jumuiya ya uhifadhi ya wanyamapori {WMA}
la Randilen linalopakana na hifadhi ya taifa tarangire Wilayani Monduli
mkoani Arusha.
Balozi wa Marekani nchini
Tanzania Mark Childress wakitiliana saini mkataba wa mradi wa PROTECT na
Waziri wa Mali Asili na Utalii nchini Tanzania Lazaro Nyalandu
Waziri wa Mali Asili na Utalii
nchini Tanzania Lazaro Nyalandu akizungumza katka uzinduzi huo,
ameishukuru serikali ya Marekani kwa msaada huo huku akiongeza kuwa
kumekuwa na uvamizi mkubwa katika maeneo ya hifadhi za taifa na kusema
kuna mpango makakati wa kuhakikisha njia zote zinafunguliwa ili
kuwezesha wanyamapori wote kuwa huru kuzunguka katika hifadhi zote
nchini.
Mkuu wa mradi huo wa PROTECT Jon
Anderson akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa PROTECT wa dola za
kimarekani Milioni 14.5 wa kulinda mazingira,kukuza uhifadhi na utalii
nchini hapa.
Mwenyekiti wa jumuiya ya hifadhi ya jamii Randilen Daniel Loishaye akizungumza katika uzinduzi huo.
Wadau wa wanyamapori wakiwa wanafatilia hotuba ya Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mark Childress.
Balozi wa Marekani nchini
Tanzania Mark Childress akiwa anapunga mikono ishara ya kuagana na wadau
mbalimbali waliofika katika uzinduzi huo
Wanyama aina ya Twiga wakiwa wanapamba hifadhi ya Tarangire.
…………………………………
(Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog
Serikali ya Marekani kwa kupitia shirika la ushirikiano wa kimataifa
{USAID} imezindua rasmi mradi wa miaka mitano wa kulinda mazingira na
kukuza uhifadhi wa utalii wa dolla za kimarekani milioni14.5 hapa
nchini ujulikanao kama PROTECT=PROJECT
{USAID} imezindua rasmi mradi wa miaka mitano wa kulinda mazingira na
kukuza uhifadhi wa utalii wa dolla za kimarekani milioni14.5 hapa
nchini ujulikanao kama PROTECT=PROJECT
Uzinduzi huu ambao umefanyika ndani ya eneo la hifadhi ya wanyamapori
linalosimamiwa na jumuiya ya uhifadhi ya wanyamapori {WMA} la Randilen
linalopakana na hifadhi ya taifa tarangire Wilayani Monduli mkoani
Arusha, balozi wa marekani nchini Tanzania mark Childress amesema
mradi huu unalenga kujenga uwezo wa uhifadhi na kukabiliana na
ujangili na usafirishaji haramu wa wanyamapori nchini kote Tanzania.
linalosimamiwa na jumuiya ya uhifadhi ya wanyamapori {WMA} la Randilen
linalopakana na hifadhi ya taifa tarangire Wilayani Monduli mkoani
Arusha, balozi wa marekani nchini Tanzania mark Childress amesema
mradi huu unalenga kujenga uwezo wa uhifadhi na kukabiliana na
ujangili na usafirishaji haramu wa wanyamapori nchini kote Tanzania.
Balozi Mark amesema mradi wa PROTECT utalenga kutoa ufumbuzi wa muda
mfupi kwa tatizo kubwa lililopo sasa la ujangili huku likiweka misingi
ya mafanikioya muda mrefu katika vita dhidi ya ujangili sanjari na
kuhimiza ushirikiano kati ya jumuiya za kiraia.
mfupi kwa tatizo kubwa lililopo sasa la ujangili huku likiweka misingi
ya mafanikioya muda mrefu katika vita dhidi ya ujangili sanjari na
kuhimiza ushirikiano kati ya jumuiya za kiraia.
Amesema mradi huu pia utatoa ruzuku ya miaka mitano ya dolla za
kimarekanio 2.75 milioni kwa jamii inayozunguka hifadhi kwa lengo la
kuwajengea uwezo wa kusimamia raslimali hizo.
kimarekanio 2.75 milioni kwa jamii inayozunguka hifadhi kwa lengo la
kuwajengea uwezo wa kusimamia raslimali hizo.
Aidha balozi ametangaza mradi mpya wa dola 14 milioni za kimarekani
unaotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni utakaoshughulikia maeneo ya
bayoanuai zilizopo katika hatari ya kutoweka katika ukanda wa
kaskazini mwa Tanzania utakao fahamika kama Endangered Ecosystems
Northern Tanzania project kwa lengo la kupambana na ujangili.kutoa
msaada ya moja kwa moja kwa MWA ,jamii na wadau katika sekta ya utalii
ili kuboresha usimamizi wa wanyamapori.
unaotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni utakaoshughulikia maeneo ya
bayoanuai zilizopo katika hatari ya kutoweka katika ukanda wa
kaskazini mwa Tanzania utakao fahamika kama Endangered Ecosystems
Northern Tanzania project kwa lengo la kupambana na ujangili.kutoa
msaada ya moja kwa moja kwa MWA ,jamii na wadau katika sekta ya utalii
ili kuboresha usimamizi wa wanyamapori.
Kwa upande wa Waziri wa Mali Asili na Utalii Lazaro Nyalandu baada ya
uzinduzi na kusaini mkataba amesema kumekuwa na uvamizi mkubwa katika
maeneo ya hifadhi za taifa na kusema kuna mpango makakati wa
kuhakikisha njia zote zinafunguliwa ili kuwezesha wanyamapori wote
kuwa huru kuzunguka katika hifadhi zote nchini.
uzinduzi na kusaini mkataba amesema kumekuwa na uvamizi mkubwa katika
maeneo ya hifadhi za taifa na kusema kuna mpango makakati wa
kuhakikisha njia zote zinafunguliwa ili kuwezesha wanyamapori wote
kuwa huru kuzunguka katika hifadhi zote nchini.
Pia amewataka wana jamii wa maeneo ya hifadhi ya jumuiya ya WMA
Randilen kukaa na uongozi wa hifadhi na kutatua changamoto zilizopo.
Randilen kukaa na uongozi wa hifadhi na kutatua changamoto zilizopo.
NHC LAFANYA UHAKIKI WA VIKUNDI VYA VIJANA KATIKA MKOA WA LINDI NA MTWARA
Uhakiki wa vikundi vya
vijana vilivyopewa msaada wa mashine na NHC ili kujiajiri na kusaidia
wananchi kupata matofali ya kujengea nyumba bora umeanza katika Mikoa
mbalimbali ukianzia na Mkoa wa Lindi na Mtwara. Katika hali
isiyotarajiwa Mkoa wa Mtwara ambao kwa muda mrefu umekuwa ukililia
kuletewa maendeleo umeshindwa kutumia fursa ya msaada wa mashine kwa
vijana waliyopewa na NHC hali iliyolifanya Shirika kutwaa baadhi ya
mashine ili zipewe vikundi vingine vinavyofanya vizuri Fuatilia kupitia
habari picha hizi ili ufahamu kilichojiri katika mikoa hiyo ya kusini
mwa Tanzania. Leo uhakiki huo unaendelea Mkoani Ruvuma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri
ya Wilaya ya Ruangwa Bw. Nicholous Kombe akimsikiliza Meneja wa Huduma
kwa Jamii wa NHC Bw. Muungano Saguya akimshukuru kwa Halmashauri hiyo
kusaidia kikundi cha vijana kwa kuwawezesha fedha na udongo kwa ajili ya
kutengeneza matofaliya kufungamana. Katikati ni Meneja wa NHC Mkoa wa
Lindi Bw. Mussa Patrick Kamendu.
Jengo la Ofisi ya kikundi cha
vijana cha Narunye(hakuna kutegeana) katika Halmashauri ya Wilaya ya
Lindi Vijijini likiwa limeonwa na Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru
kama inavyoonekana. Kikundi hiki kimeshaanza kupata maombi mengi ya
matofali kutoka kwa wananchi wanaohitaji.
Kikundi cha vijana cha Ruangwa
Materials Group katika Halmashauri ya Wilaya Ruangwa kimeshatengeneza
matrofali kwa kutumia mashine ya msaada kutoka NHC. Halmashauri ya
Wilaya hiyo imeamua kuyatumia matofali ya vijana hawa kujengea zahanati
na majengo mengine yanayohitajika katika Halmashauri zikiwemo nyumba za
Waalimu.
Meneja wa NHC Mkoa wa Lindi Bw.
Mussa Patrick Kamendu akitoa mawaidha kwa kikundi cha vijana cha Narunye
kilichopo katika Wilaya ya Lindi vijijini baada ya kutembelea kikundi
hicho kukagua kazi zake.Vijana hawa wanajihusisha pia na utunzaji
mazingira.
Baada ya Wakurugezi wa Halmashauri
za Kilwa na Lindi Vijijini kutokuwa karibu na vikundi vya vijana,
Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC na Meneja wa Mkoa wa Lindi waliweza
kufanya mazungumzo nao ya kina na hatimaye wamekubali kuwasaidia vijana
waliopewa msaada wa mashine na NHC katika Halmashauri zao ili waweze
kujiajiri. Kulia ni Bi. Oliver Vavunge ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini na wa pili kulia ni Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Kilwa Bi. Maimuna Mtanda.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Manispaa ya Lindi Bw. Daniel Kaluse hakuwa nyuma kutembelea kikundi cha
Vijana na Maendeleo kilichopo eneo la Mitwero nje kidogo ya Manispaa
hiyo ili kuwapa moyo na kufahamu maendeleo yao akiwa ameandamana na
ujumbe wa NHC.
Meneja wa NHC Mkoa wa Mtwara Bw.
Joseph John akitoa taarifa ya Mkoa kwa Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC
ya maendeleo ya vikundi vya vijana waliosaidiwa mashine na NHC . Katika
taarifa yake Meneja huyo alisikitishwa na vijana wa Mkoa wa Mtwara
kushindwa kutumia kikamilifu msaada huo na akalaumu Halmashauri za Mkoa
huo kushindwa kushiriki kikamilifu katika programu hiyo ya kusaidia
vijana.
Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC
Bw. Muungano Saguya akikemea na hatimaye kukinyanganya mashine kikundi
cha Likonde katika Manispaa ya Mtwara kwa kuifungia stoo mashine
waliyopewa msaada na NHC bila kufanya kazi iliyokusudiwa ya kufyatua
matofali. Mashine hiyo itapewa kikundi kingine ili itumike kikamilifu.
Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC
Bw. Muungano Saguya akiwa Wilayani Tandahimba akikagua matofali
yaliyotengenezwa na kikundi cha vijana cha Maendeleo Group kilichopewa
msaada wa mashine na NHC. Kikundi hiki kinasubiri kulipwa na Halmashauri
matofali hayo yanayotarajiwa kujengea nyumba za waalimu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri
ya Tandahimba Bw Dennis Mwaitete akielezea mkakati wa Halmashauri yake
wa kusaidia vijana ulivyo alipotembelewa na ujumbe wa NHC uliokuwa
ukihakiki vikundi vya vijana Mkoani Mtwara.
Kikundi cha vijana cha Umoja
Lekanelo kilichopo Wilaya ya Newala kilichoshindwa kutumia kikamilifu
mashine ya msaada kilichopewa na NHC kiliweza kupokonywa mashine hiyo
jana. Wilaya ya Newala ina shughuli za madini na kilimo cha korosho
kiasi cha kuwafanya vijana kushindwa kujihusisha kikamilifu na mradi wa
kufyatua matofali.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri
ya Wilaya ya Newala Bw. Marx Kamaoni akizungumza na ujumbe wa NHC
uliofika Ofisini kwake kuhamasisha Halmashauri za Wilaya kusaidia
vikundi vya vijana vilivyopewa msaada wa mashine za kufyatulia matofali
na NHC.
Vyombo vya habari vimehusishwa
katika uhakiki huu na hapa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Newala
Bw. Marx Kamaoni akiongea na waandishi wa habari kuelezea mkakati wa
Halmashauri yake kusaidia vijana.
Kikundi cha Vijana cha For Energy
Group kilichopo Wilayani Masasi kilitembelewa na baada ya kuridhishwa na
utendaji wake NHC ilikiongezea mashine mbili zilizopokonywa vikundi
vingine vilivyoshindwa kuzitumia Wilayani Newala na Masasi Vijijini. Hii
ni nyumba iliyojengwa na kikundi hicho Wilayani Masasi.
Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC
Bw. Muungano Saguya akivionya vikundi vya vijana vya Nayoden na Mangaka
Wilayani Nanyumbu waliokula fedha ya mtaji waliopewa na NHC ambapo
aliamuru kuchukuliwa kwa mashine zao na kuwapa muda wa kujiandaa.
Aliwataka kuziomba mashine hizo kwa maandishi watakapokuwa tayari
kuzitumia. Mashine hizo zilifungiwa Ofisi ya Kata ya Mangaka kwa muda wa
miezi nane wakisubiri kupata fedha nyingine kutoka NHC.
Mashine iliyopokonywa vijana
wazembe Wilayani Nanyumbu ikipandishwa katika gari baada ya vijana hao
kuzembea kuitumia na kuifungia Ofisi kwa muda mrefu.
TBL FAMILY DAY ILIVYOFANA BAHARI BEACH DAR es salaam
Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), wakiandika majina ya
watoto waliofika pamoja na wazazi wake kwa ajili ya kuwapatia zawadi
wakati ya sherehe ya siku ya familia ya TBL iliyofanyika kwenye ufukwe
wa bahari beach.
Ofisa Uhisano wa TBL, Dorris Malulu akiwa na mumewe wakipata mlo.
Wakipata chakula wakati wa siku ya familia.
Watoto wa wafanyakazi wa TBL wakiogelea wakati wa siku ya familia.
Wafanyakazi wa TBL NA FAMILIA ZAO WAKICHEZA MUZIKI.
Mabalozi wa Bia mpya ya Twist wakiwasili kwa boti katika hafla hiyo.
Mabalozi wa Bia mpya ya Twist wakiselebuka kanda ya bahari ya Hindi
baada ya kushuka kwenye boti iliyowaleta kwenye ufukwe wa Bahari Beach,
Dar es Salaam kushiriki siku ya familia ya Kampuni ya Bia tanzania (TBL)
Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia
Tanzania (TBL), wakicheza muziki kando ya ufukwe wa bahari beach, dar es
salaam wakati wa sherehe ya siku ya familia ya TBL.
Msaani mwenye vimbwanga katika
sanaa ya maigizo na sarakasi, Emsi Amani wa kundi la Sanaa la Bantu
Acrobatics akionyesha uwezo wake wa kucheza na jukwaa wakati wa siku ya
familia ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
BARAZA LA USHAURI LA WATUMIAJI USAFIRI WA ANGA TCAA-CCC WASHIRIKI KIKAMILIFU WIKI YA UTUMISHI WA UMMA MNAZI MMOJA DAR ES SALAAM
Kikosi
kazi cha Watumishi wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma za Usafiri
wa Anga (TCAA-CCC) wakiwa tayari kutoa huduma kwa wageni mbalimbali
watakaotembelea banda hilo katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma
viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Athuman
Bakari, Aziza Tamim na Debora Mligo.
Watumishi
wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma za Usafiri wa Anga
(TCAA-CCC)wakitoa huduma kwa wageni mbalimbali waliotembelea banda hilo
leo.
Katibu
Mtendaji wa Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri wa anga
(TCAA-CCC), Hamza Johari akizungumza jambo wakati wa mahojiano na
waandishi wa habari waliotembelea banda hilo.
Katibu
Mtendaji wa Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri wa anga
(TCAA-CCC), Hamza Johari akiwa katika mahojiano na waandishi wa habari
wa Magazeti ya serikali(Daily News na Habarileo) waliotembelea banda
hilo Dar es Salaam jana.
Debora Mligo na Aziza Tamim wa TCAA-CCC wakiwasikiliza wageni waliotembelea banda hilo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA)
Charles Chacha akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za
Usafiri wa anga (TCAA-CCC) liliopo kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa
Umma yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Kutoka
kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza Hamza Johari
,waelimishaji na wahamasishaji wa baraza
hilo Debora Mligo na Athuman Bakari.
Charles Chacha akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za
Usafiri wa anga (TCAA-CCC) liliopo kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa
Umma yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Kutoka
kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza Hamza Johari
,waelimishaji na wahamasishaji wa baraza
hilo Debora Mligo na Athuman Bakari.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) Charles Chacha
(mwenye suti) katikati akiwa katika picha na ya Pamoja na wafanyakazi
wa Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri wa anga (TCAA-CCC)wakati alipotembelea
kwenye banda lhilo kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini
Dar es Salaam.
(mwenye suti) katikati akiwa katika picha na ya Pamoja na wafanyakazi
wa Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri wa anga (TCAA-CCC)wakati alipotembelea
kwenye banda lhilo kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini
Dar es Salaam.
BERNARD MEMBE APATA WADHAMINI WILAYANI CHAMWINO -DODOMA, ATEMBELEA MNARA WA KUMBUKUMBU YA MW. NYERERE KATIKA KIJIJI CHA CHAMWINO IKULU
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe
(kushoto) akilakiwa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliofika
kwenye viwanja vya Ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Chamwino Ikulu,
wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kumdhamini
ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama
hicho.
Picha zote na John Badi
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe
(kushoto) akiangalia kikundi cha ngoma za asili wakati alipowasili
kwenye viwanja vya Ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Chamwino Ikulu,
wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta
wadhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi
ya chama hicho.
Mzee Aidan Mazego (kushoto),
akitoa salamu za baraka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (katikati)
alipofika kwenye Ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Chamwino Ikulu,
wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta
wadhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi
ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kulia ni Mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa
Dodoma, Mzee William Kusila.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe
(kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Chamwino
Ikulu, Joseph Seganje kuhusu Mnara wa kumbukumbu ya Hayati Baba wa
Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyeishi katika kijiji hicho,
kuanzia Julai 10.1971 hadi Oktoba 30.1971 akihimiza siasa ya ujamaa na
kujitegemea nchi nzima, wakati Waziri Membe alipofika wilayani Chamwino
Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze
kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM). Wa pili (kushoto) ni Katibu wa CCM wa wilaya hiyo,
Janeth Mashele.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe
(kushoto) akisoma falsafa za Mwl. Nyerere alipotembelea Mnara wa
kumbukumbu ya Hayati Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere
aliyeishi katika Kijiji cha Chamwino Ikulu, kuanzia Julai 10.1971 hadi
Oktoba 30.1971 akihimiza siasa ya ujamaa na kujitegemea nchi nzima,
wakati Waziri Membe alipofika wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni
22.2015, kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania urais katika
uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wa tatu
(kushoto) ni Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Janeth Mashele.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe
(kushoto) akitazama picha za matukio mbalimbali ya Mwl. Nyerere
alipotembelea Mnara wa kumbukumbu ya Hayati Baba wa Taifa, Mwl. Julius
Kambarage Nyerere aliyeishi katika Kijiji cha Chamwino Ikulu, kuanzia
Julai 10.1971 hadi Oktoba 30.1971 akihimiza siasa ya ujamaa na
kujitegemea nchi nzima, wakati Waziri Membe alipofika wilayani Chamwino
Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze
kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM). Kushoto ni Mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Dodoma,
Mzee William Kusila na (wa tatu kushoto) ni Katibu wa CCM wa wilaya
hiyo, Janeth Mashele.
SIMBA SPORT CLUB WAZINDUA TOVUTI YAKE Dar es salaam
Afisa Mtendaji Mkuu wa EAG
Group Imani Kajula Akimwelezea Jambo Rais wa Simba Sport Club Evans
Aveva (Aliyekaa) Wakati wa Uzinduzi wa Tovuti ya Club Hiyo Anayeshuhudia
ni Makamu wa Rais wa Club ya Simba Geofrey Nyange ‘Kaburu
Simba Sports Club leo
hiiimezindua tovuti yake Ili kukuza mawasiliano na wadau wake
mbalimbali hususani; wanachama, wapenzi, vyombo vya habari na wadau
wengine muhimu.
…………………………………………
Na Mwandishi wetu-Dar es Salaam
Akizungumza
wakati wauzinduzi huo Rais wa Simba Evans Aveva alisema ‘’Katika
dunia na zama za utandawazi tovuti ndio na mitandao ya jamii
ndio njia kuu ya mawasiliano. Sisi tuliliona hili na leo hii
nafurahi kuwa Simba Sports Club itazindua rasmi tovuti yake
ambayo itakuwa jukwaa kuu la mawasiliano na utoaji wa taarifa zake
za club ya Simba. Natarajia wengi wenu mtaitumia kikamilifu na muhimu
zaidi mtatupa mrejesho chanya kuhusu tovuti yetu’’.
AfisaMtendajiMkuuwa
EAG Group Imani Kajula ambao ni washauri watekeleza ji wa Masokona
Biashara wa Simba alisema ‘’Tovuti hii sio tuitaiwezesha Simba kuwapa
wadau wake taarifa mbalimbalibali pia itatumika kwa ajili ya uuzaji
wa vifaa vya Simba, Bidhaa mbalimbali mpya na muhimu zaidi
kuwaunganisha wanachama, mashabiki na wapenzi wa Simba kutumia
mitandao ya jamii iliyo rasmi ya Simba Sports Club’’.
Mkutano
huo wa wandishi wa habari ulitumika kutaarifu Wanachama,
Wapenzina Vyombo vya habari juu ya kocha mpya wa Simba.
Alizungumza wakati wakumtambulisha kocha mpya wa Simba, Rais
Aveva alisema ‘’Baada ya kupitia vyeti na maombi ya makocha
mbalimbali, Napenda kuwa taarifu kuwa Klabu ya Simba imeingia kwenye
mkataba wa kuifundisha na kocha Dylan Kerr raia wa
Uingereza. Ni kocha mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 30,
akiwa amefanya kazi Nchi mbalimbali zikiwemo Uingereza,
Scotland, Vietnam na AfrikayaKusini’’.
Aliendelea
kusema ‘’Tunaamini ujuzi na uzoefu wake wa ukocha na pia kama
mchezaji wa kiwango cha juu utakuwa chachu ya kuifanya Simba
ifanye vizuri’’
Continue reading →
Continue reading →
WIZARA YA HABARI UTAMADUNI UTALII NA MICHEZO YAMUAGA RASMI MTALAMU WA KUPIGA PICHA KUTOKA SHIRIKA LA (JICA) LA JAPAN
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk akitoa shukrani kwa mwalimu wa picha
kutoka Japan Mitsuhiro Matsuda katika hafla ya kumuaga iliyofanyika
Ofisini kwake Mnazimmoja.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar
Afisa habari Mkuu wa Idara ya
Habari Maelezo Ramadhani Ali akitoa maelezo ya mafunzo yaliyoendeshwa na
Mtaalamu wa Japan Mitsuhiro Matsuda katika hafla ya kumuaga
iliyofanyika Wizara ya Habari Mnazimmoja Zanzibar.
Mtaalamu wa kupiga picha kutoka
Shirika la JICA la Japan Mitsuhiro Matsuda akizungumza katika hafla ya
kumuaga iliyofanyika Wizara ya Habari Mnazimmoja Zanzibar.
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk akiangalia baadhi ya picha za
wanafunzi waliopata mafunzo ya mwalimu kutoka Shirika la JAICA la
Japan Mitsuhiro Matsuda katika hafla ya kumuaga iliyofanyika Wizara
Habari Mnazimmoja baada ya kumaliza muda wa miaka miwili ya kutoa
mafunzo ya kupiga picha Zanzibar.
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii
na Michezo Said Ali Mbarouk akimkabidhi zawadi Mitsuhiro Matsuda
zilizotolewa na Idara ha Habari Maelezo Zanzibar katika hafla ya kumuaga
iliyofanyika Wizara ya Habari Mnazimmoja Zanzibar
Picha ya pamoja ya Mitsuhiro
Matsuda na baadhi ya wanafunzi wake waliopata mafunzo ya miaka miwili ya
kupiga na kusafisha picha katika hafla ya kumuaga iliyofanyika Wizara
ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Mnazimmoja Zanzibar.
KINANA AKAGUA MIRADI MBALIMBALI SENGEREMA LEO, KESHO KUINGIA MISUNGWI
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuaindua rasmi
kivuko cha Super Sumar kinachofanya safari zake kati ya Pwani ya Kamanga
wilayani Sengerema na Mwanza wakati Katibu Mkuu huyo alipo fanya ziara
katika jimbo la Sengerema leo akikagua, Kuhimiza na kusikiliza kero
mbalimbali za wananchi ili kuzipatia ufumbuzi. Huku akihimiza uhai wa
Chama cha Mapinduzi CCM, Akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC
Itikadi na Uenezi.
Katika
picha kutoka kulia ni Miraji Mtaturu Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza,
Mbunge wa jimbo la Sengerema Mh. William Ngeleja, kutoka kushoto ni Mkuu
wa mkoa wa Mwanzan Ndugu Magesa Mulongo na Mkurugenzi wa Kampuni ya
Songoro Marine ya Mwanza Salum Ali wakishiriki katika uzinduai huo
uliofanyika katika Feri ya Kamanga wilayani Sengerema.(PICHA NA
KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-SENGEREMA)
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua kivuko cha Super Sumar akiwa ameongozana na viongozi wa mkoa wa Mwanza.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia chumba cha kapteni wa
kivuko hicho mara baada ya kukizindua rasmi katika feri ya Kamanga
wilayani Sengerema.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijaribu kuendesha kivuko hicho.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza jambo na Mbunge wa
Sengerema Mh. William Neleja, katikati ni Kada wa CCM Bw. Laurence
Masha na kulia ni Mkurungenzi wa Songoro Marine ya Mwanza Bw. Salim
Ali.
Mbunge
wa Sengerema Mh. William Neleja akizungumza katika uzinduzi huo huku
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akimsikiliza.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza katika uzinduzi huo
ambapo amesema ni muhimu kuitengeneza barabara ya Kamanga Sengerema kwa
kiwango cha lami ili kuboresha huduma za usafiri kwa wananchi wanaotumia
feri hiyo ya Kamanga.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mradi wa ujenzi wa mtambo
wa kusukuma maji kutoka ziwa Victoria katika kijiji cha Nyamazugo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa
Mhandisi Anhony Sanga Mkurugenzi wa MWAUWASA wakati alipokagua mradi wa
ujenzi wa mtambo wa kusukuma maji kutoka ziwa Victoria kwenda katika mji
wa Sengerema na vijiji vyake.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akilagua mradi wa ujenzi wa mtambo
wa kusukuma maji kutoka ziwa Victoria kwenda katika mji wa Sengerema na
vijiji vyake.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa
Mhandisi Anhony Sanga Mkurugenzi wa MWAUWASA wakati alipokagua mradi wa
ujenzi wa tanki kubwa la maji katika eneo la Igogo mjini Sengerema
ambalo litapokea maji kutoka ziwa Victoria kwenda katika mji wa
Sengerema na vijiji vyake.
Hii ni sehemu ya tanki la maji linalojengwa katika keneo la Igogo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Mhandisi Anhony
Sanga Mkurugenzi wa MWAUWASA wakati alipokagua mradi wa ujenzi wa tanki
kubwa la kupokea maji kutoka ziwa Victoria kwenda katika mji wa
Sengerema na vijiji vyake, Katikati ni Mbunge wa jimbo al Sengerema Mh
William Ngeleja na Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu mwenye
kofia.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mradi huo kutoka kushoto
ni Miraji Mtaturu Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza , Mhandisi Anhony Sanga
Mkurugenzi wa MWAUWASA na Mbunge wa jimbo la Sengerema Mh. William
Ngeleja wakati alipokagua mradi wa ujenzi wa tanki kubwa la kupokea maji
linalojengwa eneo la Igogo kutoka ziwa Victoria kwenda katika mji wa
Sengerema na vijiji vyake.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiendelea na ukaguzi huo
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa
Mhandisi Anhony Sanga Mkurugenzi wa MWAUWASA wakati alipokagua
mradi huo.
Mafundi wakiendelea na kazi katika mradi huo
Miraji
Mtaturu Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza akizungumza na wananchi wakati
akimkaribisha Ndugu William Ngelea kupanda jukwaani kwenye mkutano wa
hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa CCM mjini Sengerema.
Mbunge wa jimbo la Sengerema Mh. William Ngereja akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Sengerema.
Katibu
wa CCM Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akiwahutubia maelfu ya
wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa CCM
Sengerema.
Katibu
wa CCM Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akiwahutubia maelfu ya
wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa CCM
Sengerema.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ndugu Magesa Mulongo akizungumza na wananchi katika mkutano huo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika
mkutano huo uliofanyika kwenye uwanja wa CCM mjini Sengerema
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati akihutubia katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumzia masuala mbalimbali yanayohusu matatizo ya wananchi katika mkutano huo.
Umati wa wananchi akiwa umefurika katika mji wa Sengerema.
MATUKIO KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA-JUNI 22,2015
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta
na Mbunge wa Peramiho na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,
Uratibu na Bunge,Jenista Mhagama bungeni mjini Dodoma Juni 22, 2015.
(Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri
Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama akiteta na Mbunge wa
Kibakwe na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene bungeni
mjini Dodoma Juni 22, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akteta na Mbunge wa Nkenge, Asumta Mshama kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 22, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George masaju kwenye
Viwanja vya Bunge mjini Dodoma juni 22, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akizungumza na mbunge wa Mji Mkongwe, Muhammad Sanya (kushoto ) na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju kwenye Viwanja vya Bunge
mjini Dodoma Juni 22, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa
katika picha ya pamoja na watoto wa Shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu la
Parokia ya Karatu kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma juni 22, 2015.
Kushoto kwake ni Mbunge wa Viti Maalum, Cecilia Paresso.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akizungumza na watoto wa Shirika la Moyo Mtaktifu wa Yesu wa Parokia ya
Karatu, kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 22, 2015.
Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai akiteta na Mbunge wa Viti Maalum Maria Hewa kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 22, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akizungumza na Mbunge wa Mafia , Abdulkarim Shahah (kulia) na Mbunge wa
Moshi Mjini Philemon Ndesamburo (katikati) kwenye jengo la Utawala la
Bunge mjini Dodoma juni 22, 2015.








No comments :
Post a Comment