Mkurugenzi mkuu wa PSPF Bw. Adam
Mayingu
Na christian Gaya, Majira Machi 11 2014
Kufuatia kupitishwa na sheria ya Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Sheria Na. 8 ya mwaka, 2008 mtu yeyote anaweza kujiunga na PSPF, ili kukidhi matakwa ya watanzania PSPF hivyo imeanzisha mpango wa uchangiaji hiari maarufu unaojulikana kama PSS kwa lengo la kupanua wigo wa hifadhi ya jamii nchini. Hii ni kutokana na mabadiliko katika sekta ya hifadhi ya jamii ndiyo yamepelekea kuwepo na mabadiliko ya sheria ya Mfuko wa pensheni wa PSPF. Sheria ya Mfuko kwa sasa inaruhusu kusajili wanachama katika sekta zote za umma na binafsi. “Mfuko sasa una mpango wa uchangiaji wa lazima na mpango wa uchangiaji wa hiari, sasa mtu yeyote awe kwenye sekta binafsi, sekta rasmi na isiyo rasmi anaweza kujiunga na PSPF, pia hata mtanzania akiyepo nje ya nchi anaweza kujiunga na PSPF na wageni wote wanaofanya kazi nchini” Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Adamu Mayingu anasema
Kufuatia kupitishwa na sheria ya Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Sheria Na. 8 ya mwaka, 2008 mtu yeyote anaweza kujiunga na PSPF, ili kukidhi matakwa ya watanzania PSPF hivyo imeanzisha mpango wa uchangiaji hiari maarufu unaojulikana kama PSS kwa lengo la kupanua wigo wa hifadhi ya jamii nchini. Hii ni kutokana na mabadiliko katika sekta ya hifadhi ya jamii ndiyo yamepelekea kuwepo na mabadiliko ya sheria ya Mfuko wa pensheni wa PSPF. Sheria ya Mfuko kwa sasa inaruhusu kusajili wanachama katika sekta zote za umma na binafsi. “Mfuko sasa una mpango wa uchangiaji wa lazima na mpango wa uchangiaji wa hiari, sasa mtu yeyote awe kwenye sekta binafsi, sekta rasmi na isiyo rasmi anaweza kujiunga na PSPF, pia hata mtanzania akiyepo nje ya nchi anaweza kujiunga na PSPF na wageni wote wanaofanya kazi nchini” Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Adamu Mayingu anasema
Kulingana na matakwa ya sheria ya msimamizi
na mdhibiti wa mifuko ya pensheni ya hifadhi (SSRA) inasistiza ya kuwa kila
mtumishi aliye katika ajira rasmi anatakiwa kujiunga na Mfuko wowote wa Hifadhi
ya Jamii aupendao. Na dira ya mdhibiti na msimamizi wa mifuko ya pensheni ya
hifadhi ya jamiii nchini yaani SSRA ni kuwa na wigo mpana wa hifadhi ya jamii
ulio endelevu na wenye huduma bora kwa kila Mtanzania, lakini takwimu
zilizotolewa mwaka 2012 zinaonesha ya kuwa ni watu
milioni 1.7 tu ndio waliojiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii wakati idadi ya
watanzania wote ni milioni 44.9 hii ikiwa ni asilimia 6.5 tu ya nguvu kazi yote
ya watu milioni 23.7
Hivyo ni kwamba
asilimia 93.5 ya watanzania wote wanaotegemewa kuwa ni milioni 44.9 hawana
pensheni ya hifadhi ya jamii. Kwa kweli hata hao ambao wanahudumiwa na hifadhi
ya jamii nayo inazidi kupungua kwa sababu ya sera za serikali za kubinaifisha
mashirika ya umma kwa watu binafsi na matokeo yake yamekuwa yanakupunguza
wafanyakazi badala ya kuongeza kuajiri zaidi na kusababisha kila siku idadi
kubwa ya wanachama kutoa michango ya pensheni kutoka katika mifuko ya hifadhi
ya jamii. Wakati
dhima ya mdhibiti na msimamizi wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamiii
nchini ni kuhakikisha huduma bora za Hifadhi ya Jamii zinamfikia kila Mtanzania
kupitia usimamizi madhubuti wa sekta ya Hifadhi ya Jamii.
Hifadhi ya Jamii ni haki ya kila Mtanzania. Haki hii imeanishwa wazi katika Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 11(1) na Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003.
Haki
hii pia imeiainishwa kwenye mkataba wa kimataifa wa haki za binadamu wa mwaka
1948 pamoja na mikataba ya shirika la kazi duniani (ILO) ibara ya 102 ya mwaka
1952.
Kwa mujibu wa shirika
la kazi duniani hifadhi ya jamii ni mfumo ambao jamii husika imejiwekea kwa
lenga ya kujikinga dhidi ya matukio yasiyotarajiwa. Matukio hayo ni kama
Maradhi, ulemavu, kupoteza kazi, kuacha kazi kwa sababu ya uzee (kustaafu),
aidha kwa hiari au kwa lazima na mengineyo, ikiwamo huduma za matibabu, gharama
za msiba ikiwa mwanachama amefariki. Vilevile iwapo mwanachama atafariki kabla
ya kustaafu basi mafao yake hulipwa kwa warithi wake kiasi cha kwamba mifuko
mingine ya hifadhi ya jamii huweza hata kusaidia kusomesha watoto wa wanachama.
Lengo la hifadhi ya
jamii ni kuwezesha mwananchi kuishi maisha yenye staha kwa kuwawezesha kupata
huduma za msingi pale wanapokuwa hawana kipato kutokana na sababu mbalimbali
zinatokana na uzee, kifo,ugonjwa, uzazi n.k
Dhana ya hifadhi ya
jamii inahusisha taratibu za ulinzi dhidi ya majanga ya kiuchumi na ya kijamii
yanayosababishwa na kukoma au kupungua kipato kutokana na maradhi, uzazi,
kuumia kazini, ukosefu wa ajira, ulemavu, uzee, kifo na kuongezeka kwa gharama
za matibabu.
Hata mfuko wa pensheni
wa hifadhi ya jamii unaotoa huduma kwa watu ambao wako katika sekta ya kilimo,
sekta ya uchumi isiyokuwa rasmi na kwa wale ambao wako sekta rasmi na isiyo
rasmi wanaofanya kazi kwa mkataba, na vibarua wengi wao idadi kubwa yao
hawajawa wanachama wa mifuko hii ya pensheni ya hifadhi ya jamii. Pensheni
zinatolewa na mifuko iliyopo haitoshelezi mahitaji ya wastaafu kwa sababu ya
kutokwenda na hali halisi ya mfumuko wa bei sokoni hivyo kuzidisha ukali wa
hali maisha ya kila siku. Hivyo kuna haja watanzania kuelemishwa juu ya
kujiunga na mifuko ya pensheni ya ziadi ya kujiunga kwa hiari hata kama ni
mwanachama wa mchangiaji mzuri wa mifuko hii ya lazima kisheria, jaribu
kuchangua mwenyewe sokoni ni upi unaweza kukusaidia hapo baada ya kustaafu ili
kutunisha kikapu cha pensheni yako na familia yako
Katika kusaidia kukuza na kupanua
wigo wa hifadhi ya jamii mdhibiti na msimamizi wa mfuko ya pensheni ya hifadhi
ya jamii SSRA sheria inasema kila Mtanzania aliye katika ajira binafsi au
anayejiajiri anaweza kuamua kujiunga na Kuchangia Mfuko wa Msingi wa Hifadhi ya
Jamii aupendao
Na kwa upande mwingine ni kwamba
SSRA inatamka wazi ya kwamba waajiriwa au wanaojiajiri wanayo haki ya kujiunga
na Mifuko ya Hiari waipendao.
Kwa kawaida kulingana na utaratibu
wa uendeshaji wa hifadhi ya jamii mfuko unatakiwa kutoa namba maalumu na kadi
ya uanachama kwa kila mwanachama wa Mfuko.
SSRA unatamka wazi vile vile ya
kwamba ni kinyume cha Sheria kwa Mfuko mmoja kumwandikisha kwa mara ya pili,
mwanachama ambaye tayari ameandikishwa na Mfuko mwingine wa msingi yaani kwa
mfuko wa kujiandikisha kwa lazima kisheria
“Ili kusaidia kukuza na kupanua wigo
wa hifadhi ya jamii nchini mfuko wa pensheni wa PSPF inatamka wazi ya kwamba
waajiriwa au wanaojiajiri wanayo haki ya kujiunga na Mfuko wake wa Hiari yaani
PSS. Ili kuwahudumia Watanzania wote walioko ndani na nje ya nchi pamoja na
raia wa kigeni wanaofanya kazi nchini, PSPF imeanzisha Mpango wa Uchangiaji wa
Hiari (PSPF Supplimentary Scheme) maarufu kama PSS.” Mayingu anatamka ambaye
ndiye mkurugenzi mkuu wa PSPF.
Anasema kujiandikisha ni rahisi sana
kwani mwanachama anatakiwa kujaza fomu PSS. FN.1 na kuambatanisha picha moja ya
rangi (passport size) pamoja na taarifa muhimu za mwanachama. Mara baada ya kukamilisha
usajili, mwanachama hupewa nambari na
kitambulisho cha uanachama. Mkurugenzi mkuu anasema mwanachama wa mpango
wa hiari atakuwa kisheria ana haki ya kunufaika na Fao la Elimu, Fao la
Ujasiriamali, Fao la Uzeeni, Fao la Kifo,Fao la Ugonjwa ,Fao la Kujitoa, Mkopo
wa nyumba kwa atakayekidhi vigezo
“Mwanachama atapaswa kuchangia si chini ya Tshs 10,000 kwa
mwezi. Michango inaweza kuwasilishwa kwa siku, wiki, mwezi au awamu. Mwanachama
atawekewa gawio la akiba yake kwa kila mwaka mara moja ambayo ni gawio la
asilimia sita (6) kwa mwaka. Uanachama ni kwa watanzania wote na wasio
watanzania wanaofanya kazi nchini na hata waliopo nje ya nchi. Wanachama
waliokwisha kujiunga na Mifuko mingine ya hifadhi ya jamii ikiwemo PSPF
wanaweza kujiunga na mpango huu, jiunge sasa ufaidike”
Mayingu anatamka bayana. Kiasi
cha michango ni shs 10,000/= kwa
mwezi, hakuna kiwango cha juu, na mwanachama yuko huru kuchagua
kuwasilisha michango kwa wiki,
mwezi, au kwa msimu, na michango inaweza
kuwasilishwa kwa kupitia:-Akaunti za Benki na Wakala wa malipo wa M-Pesa na
Airtel money
Mpaka kufikia mwezi Juni, 2012 idadi ya wanachama
wachangiaji ilikuwa 309,767 ambayo ilivuka lengo la kuwa ikiwa kama ongezeko la
asilimia 4 kufikia wakati huo. Wakati mpaka kufikia mwezi Juni mwaka 2013 mfuko
ulikuwa na jumla ya wanachama wapatao 367,402. Ambapo kati ya hao wanachama
wachangiaji walikuwa 320, 860. Mpaka June mwaka 2012 mfuko ulikuwa na idadi ya
waastafu wapatao 36, 535 na mpaka kufikia June mwaka 2913 idadi ya wastaafu
iliongezeka mpaka kufikia wastaafu 46,542 ambayo ilikuwa ni sawa na ongezeko la
asilimia 27 kwa mwaka.
Mkurugenzi mkuu anasema majukumu ya
mfuko huu wa PSPF ni Kusajili wananachama wapya ambapo hadi kufikia mwezi Novemba
2013 Mfuko ulikuwa na jumla ya wanachama wapatao 398,717. Kutunza kumbukumbu za
wanachama na wastaafu ambapo hadi Novemba 2013 mfuko ulikuwa na wastaafu
48,206. Kukusanya michango na kutunza taarifa za michango ya wanachama.
Kuwekeza michango katika vitega uchumi mbalimbali na salama. Kulipa Mafao na
kufanya Tathmini ya Mfuko na kuweka mikakati endelevu ambapo hadi kufikia
tarehe 30/06/2013 ambapo Mfuko ulikuwa na thamani ya shs trilioni 1.25 kutoka
shs bilioni 36.0 mwaka 2000
Anasema
dira ya mfuko ni mtoa huduma bora wa
huduma za hifadhi ya jamii nchini kwa dhima ya kutoa huduma zenye ushindani
katika sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa wateja wao kwa kutumia watumishi wenye ari
ya kazi na teknolojia inayofaa. “Maadili Yetu ni kuhakikisha ya
kuwa Mfuko unatoa huduma zake kwa wateja, wadau na umma kwa kuzingatia misingi ya
Uwajibikaji, Wajibu, Muitikio, Nidhamu, Juhudi. Uwazi na Unyenyekevu kwa wote”
anasema
Mkurugenzi
anajaribu kutofautisha kati mifuko hii miwili mfuko wa lazima kisheria yaani
PSPF na ule wa hiyari yaani PSS anasema kwa upande wa Mwanachama Wa Mfuko wa
lazima kisheria Mtu yeyote aliyeajiriwa au kujiajiri katika sekta rasmi au
isiyo rasmi anaweza kuwa mwanachama. Mafao yanayotolewa na Mfuko huu Mkuu ni
kama vile: Mafao ya Uzeeni (Old Age Benefits), Mafao ya Ulemavu (Invalidity
Benefits), Mafao ya Kifo (Death Benefits), Malipo ya“pensheni” ya Wategemezi
(Survivors’ Pensions), Rambirambi ya mazishi (Funeral grants) na Mafao ya
Kujitoa (Withdrawal Benefits)
Na
kwa upande wa mafao yanayotolewa na Mpango wa Hiari (PSS) ni: Fao la Elimu
(Education benefit), Fao la Ujasiriamali (Entrepreneurial Support Benefit), Fao
la Uzeeni, Fao la Ugonjwa au Ulemavu (Retirement benefit). Fao la Kifo na
(Death gratuity), Fao la Kujitoa (withdraw benefit). Huduma nyinginezo
zinazotolewa ni: Mkopo wa kujenga/kununua nyumba kwa wanachama wake waliobakiza
miaka mitano kabla ya kufikia umri wa kustaafu kwa lazima ambapo mwanachama
huweza kukopeshwa hadi 50% ya mafao yake yanayokokotolewa wakati wa maombi.
Nyumba zilizojengwa na Mfuko wa PSPF zinazouzwa kwa wananchi wote na nyumba
hizo zipo katika mikoa ya Dar es Salaam- Ilala (Buyuni), Morogoro (Lukobe),
Tabora (Usule), Mtwara (Mang’amba) na Shinyanga (Ibadakuli).
Na kwa upande mwingine mkurugenzi
mkuu anasema mkopo wa nyumba zilizoko katika mradi wa nyumba wa PSPF, ambapo
mwanachama aliyechangia kwa muda usiopungua miaka mitano sawa na miezi 60
anadhaminiwa na Mfuko kupata mkopo wa kununua nyumba hizo kupitia benki za
Azania Bank, CRDB Bank, Exim Bank na NMB.
Anasema mpaka sasa nyumba
zilizojengwa ni 666. Mikopo kwa wanachama inatolewa kupitia mabenki yalioingia mikataba maalum na Mfuko ambapo riba ndogo ambayo ni asilimia 12
hutozwa kwa marejesho ya hadi miaka 25.
Pia nyumba zinauzwa kwa fedha taslimu kwa mwanachama na mwananchi yeyote.
Mpango wa uchangiaji wa hiari ni msaada mkubwa kwa watu wote walio na wasio katika sekta rasmi ambao kwa kujiunga na mpango huo watanufaika na mafao ya elimu, ugonjwa, ujasiliamali, fao la uzeeni, kujitoa na mkopo wa nyumba kwa wale watakaokidhi vigezo.
“PSPF sasa ni kwa watu wote walio kwenye sekta rasmi na wale ambao hawako kwenye sekta rasmi maana lengo letu ni kuwafikia watu wengi ndani na nje ya nchi kupitia mpango huu wa uchangiaji wa hiari PSS ambao kiwango chake cha chini cha uchangiaji ni sh.10,000 kwa mwezi” anasema Mayingu.
Akizungumzia mwamko wa watu kujiunga na mpango huo wa hiari PSS, mkurugenzi mkuu anasema kumekuwa na mafanikio makubwa kwani tangu kuzinduliwa kwake mapema machi 7 mwaka 2013 tayari wanachama zaidi ya 5,000 wamejiunga na mpango huo. “Makundi zaidi ya 25 yamejiunga na mfuko huu kutokana na ubora wa mafao yake na mikopo inayotolewa kwa wanachama waliojiunga na mfuko huo kwa miaka mitano tofauti na wakati wa nyuma ambapo mikopo ya nyumba ilitolewa kwa wanachama waliobakiza miaka mitano ya kustaafu” anasema .
Mkurugenzi
mkuu anasema ya kwamba uanachama ni wa
hiari kwa mtu yeyote aliyeajiriwa au kujiajiri mwenyewe, mwanachama aliye
katika mifuko mingine, na kwamba mwanachama wa mpango wa hiari anayo fursa ya
kuhamia kwenye mpango wa uchangiaji kwa mujibu wa sheria ya mfuko wa pensheni
wa PSPF
Awali PSPF ilikuwa inahudumia
watumishi wa Serikali Kuu na Wakala wa Serikali tu. Kufuatia mabadiliko ya
sheria katika Sekta ya Hifadhi ya Jamii Tanzania; sasa mtu yeyote awe kwenye
sekta binafsi, sekta rasmi na isiyo rasmi anaweza kujiunga na PSPF. PSPF ni
Taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoanzishwa kwa Sheria Namba 2 ya Mafao ya
Hitimisho la Kazi kwa Watumishi wa Umma ya mwaka 1999 yaani The Public Service
Retirement Benefits Act No.2 of 1999, sura ya 371, hivyo pia Mtanzania aliyepo
nje ya nchi anaweza kujiunga na PSPF na wageni wote wanaofanya kazi nchini.
No comments :
Post a Comment