Thursday, April 3, 2014

NSSF na mpango kujenga nyumba gharama nafuu



 

Dkt. Ramadhani Dau mkurugenzi mkuu wa NSSF

Na Christian Gaya Majira Machi 18, 2014
Asilimia kati ya 70 na 75 ya wananchi wa Tanzania wanaishi katika makazi holela. Hadi sasa Tanzania ina mahitaji ya zaidi ya nyumba milioni tatu kwa ajili ya makazi ya watu katika maeneo mbalimbali ya nchi 

Kwa ajili ya kusaidia serikali katika kutatua changamoto zinazolikumba taifa NSSF limekuja na sera yake ya uwekezaji wa kuhakikisha ya kuwa angalau asilimia ya 75 ya fedha za uwekezaji kila mwaka wa fedha zinatengwa kwa ajili ya uwekezaji na asilimia 25 inayobakia inatumika kwa ajili ya kulipa mafao, shughuli za utawala na uendeshaji wa mfuko na shughuli zingine za maendeleo za shirika

“Tumeamua kuweka mikakati zaidi kwenye mradi wa nyumba za gharama nafuu kwa ajili ya kuhakikisha ya kuwa wateja wetu wanamiliki nyumba zao za kisasa zinazouzwa kwa bei nafuu ili kumwezesha kila mwanachama mchangiaji wa  mfuko huu wa NSSF  anamiliki nyumba na kuboresha maisha yake” Daktari Dau ambaye ndiye mkurugenzi mkuu anasema.



Shirika la taifa la hifadhi ya jamii linasema linategemea kupanga muda wa kumaliza wa kujenga mradi wa nyumba za gharama na nafuu zipatazo kama 7600 kama jitihada za mfuko huo katika kujenga nyumba zenye staha kwa watanzania 


Mkurugenzi mkuu anasema ila isipokuwa nyumba hizi za gharama nafuu zimelengwa hasa kuuziwa wanachama wa NSSF kwa mkopo wa muda mrefu na zinategemewa kujenga maeneo na sehemu za kijiji cha Dege na kigamboni wilayani Temeke. Daktari Dau anaeleza ya kuwa mradi huu utagharimu kiasi cha tabribani fedha za kimarekani zipatazo dola 5048 na zinategemewa kumalizika kujenga ufikapo mwaka 2018

Kulingana na maelezo yake Dau anasema mradi huu utamepakiwa kutekelezwa kwa awamu kuu tatu, wakati awamu ya kwanza itakayokuwa imejenga nyumba zipatazo 2,500 imepangwa kumalizika mwisho mwa mwaka 2016

Na awamu ya pili inategemewa kumalizika mnamo mwaka unafuata wa mwaka 2017 ambapo nyumba zitapato 2,500 zitakuwa zimesha ezekwa tayari kwa mauzo kwa wanachama  wa mfuko wa NSSF. Wakati kwa awamu ya tatu mpaka kufikia mwaka 2018 nyumba zipatazo 2,460 zinategemewa kumalizika

“Nyumba hizo zinategemewa kuuzwa katika ya fedha za kimarekani dola 80,000 mpaka dola 130,000 na mfuko uko tayari kupokea fedha hizo kuanzia sasa kwa wanachama yeyote anayetaka kutanguliza malipo” anasema.

Daktari Dau anawahakikishia kwa yeyote atayekuwa mkazi wa huko Dege, ya kwamba kijiji cha Dege kitakuwa na huduma zote za muhimu za kijamii zikiwemo shule, hospitali, nyumba za ibada, sehemu za kupaki magari, sehemu za burudani na starehe na vifaa vyote vya usalama na ulinzi

Pamoja na hayo mwenyekeiti wa bodi ya wakurugenzi Bwana  Abubakar Rajabu anasema ya kuwa bodi yake imeridhika na maendeleo ya mradi huo na ana uhakika ya kuwa wa muda uliopangwa kumaliza kazi utatekelezwa vile vile bila wasiwasi.

Kijiji cha Dege kinajengwa na NSSF baada ya NSSF kuingia ubia na Kampuni ya Azimio ambayo inamiliki ekari karibu 3000 zilizoko Dar es Salaam

Mpaka kumalizika kwake daraja la Kigamboni litagharimu fedha za kimarekani zipatazo dola milioni 33 ambazo ni sawa sawa na shilingi za kitanzania bilioni 214.6 ikitekelezwa na NSSF kwa asilimia 60 ya fedha ikishirikiana na serikali kwa asilimia 40 ya gharama hizo za ujenzi. Ambayo inahusisha kwa upande mmoja kujenga barabara ya lami ya kilomita moja( km 1) zikiwa na barabara nyembamba zipatazo sita kutoka kurasini zikiwa juu ya daraja lenye meta 680 na barabara nyingine ya lami yenye kilometa moja na nusu (km1.5) ambayo vile vile kwa upande mwingine itakuwa na barabara nyembamba zipatazo sita
kulingana na mpango yakinifu daraja la kigamboni lilitegemewa kumalizika  mwezi Januari mwaka 2015 lakini kutokana na mwingiliana wa changamoto  mbalimbali , zikiwemo  na baadhi ya wakazi kukataa kuondoka huenda mradi huo ukaishia kumalizika mnamo mwezi wa sita au wa saba mwakani 


kwa upande wa meneja wa mradi Bwana Karim Mattaka anasema kutokana na wakazi kukataa kuhama wamesababisha ujenzi wa daraja kupungua kasi ya ujenzi wake. Tulikuwa tulipanga  kumaliza mradi huu mwezi wa juni  mwaka ujao, lakini kutokana na changamoto hii, huenda ikachukua miezi sita au zaidi alisisitiza


Mattaka ambaye ndiye meneja wa mradi huo anawakumbusha serikali kuchangia asilimia 40 ya fedha inayotakiwa kwa ajili ya kutoa msukumo wa mwendelezo wa ujenzi wa mradi, anasema mpaka sasa NSSF imekuwa ikitumia fedha yake na kama serikali watachelewesha sana hizo fedha  huenda wakawa ndiyo kizuizi cha maendeleo ya mradi na mradi kutomalizika kwa muda wake uliopangwa 


Mkurugenzi mkuu anasema katika mwaka wa fedha 2012/2013 Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii yaani NSSF liliweza kupata mapato ya kiasi cha shilingi milioni 678,708.5 ambalo ilikuwa sawa na asilimia 88.7 ya lengo.  Makusanyo haya ya mapato yaliweza kutumika katika kulipa mafao ya Wanachama, kuwekeza katika vitega uchumi, kulipa gharama za uendeshaji na miradi ya maendeleo.

Daktari anabainisha ya kuwa wakati huo huo wa mwaka fedha semina 542 zilifanyika kwa waajiri na wanachama nchi nzima ili kuweza kuelewa vizuri mfumo mpya wa Hifadhi ya Jamii kwa ujumla ukiwemo na Mkutano Mkuu wa Tatu wa wadau uliofanyika mwezi Februari 2013 ambao ulihudhuriwa na wanachama na wadau wa sekta ya jamii wapatao 745. Vile vile katika mwaka wa fedha 2012/2013 Shirika liliweza kupima afya za wanachama wake wapatao 6,283 kama wajibu wa sehemu yake wa fao bima ya afya na  Wanachama wapatao 78,670 ambao ni sawa na asilimia 68.11 ya lengo la wanachama 115,500 waliweza kuandikishwa kwa kipindi hicho cha katika mwaka wa fedha 2012/2013.

Aidha, katika mwaka wa fedha 2012/2013 Shirika lilipa mafao mbalimbali kama vile mafao ya muda mrefu ambayo ni kama vile pensheni ya uzee, pensheni ya ulemavu na pensheni ya urithi  na kundi la pili ni mafao ya muda mfupi ambayo ni kama vile mafao ya uzazi, mafao ya kuumia kazini na magonjwa yatokanayo na kazi, msaada wa mazishi na mafao ya bima ya afya yaani “mafao ya matibabu” (SHIB). Shirika pia hulipa mafao ya kujitoa uanachama kwa mfumo wa akiba kwa wanachama aliyeondoka katika ajira kwa sababu mbalimbali ya jumla ya shilingi bilioni 185.32 ambazo ni asilimia 183.03 ya lengo la shilingi bilioni 101.24 kwa wanachama 54,840. 


Pamoja na hayo mkurugenzi mkuu anasema mchakato umeanza wa utekelezaji wa mradi wa uzalishaji umeme wa megawati 150 katika eneo la Mkuranga. Hivi sasa mradi upo katika hatua ya kupata washauri elekezi kwa ajili ya usanifu wa njia ya kusafirishia umeme kutoka Mkuranga hadi kwenye Gridi ya Taifa Kinyerezi-Dar es Salaam na mradi huu, utatekelezwa kwa ushirikiano na TANESCO. “Wakati taratibu za kupata mshauri elekezi kwa ajili ya kituo cha kufua umeme wa megawati 300 zimeshaaanza mwaka wa fedha 2013/14, baada ya kufahamu mazingira ya mradi na njia ya usafirishaji umeme. Lengo ni kufanya miradi hii itekelezwe na kumalizika kwa wakati mmoja” anasema


“Ujenzi wa daraja la Kigamboni unaendelea vizuri. Aidha, daraja la muda la kusaidia ujenzi wa daraja la kudumu limekamilika na kazi ya ujenzi wa daraja la kudumu imeanza. Mbali na mafanikio hayo, kuna changamoto ya kulipa fidia kwa wamiliki wa maeneo ya upande wa Kurasini na Kigamboni ambayo yamo ndani ya eneo la barabara unganishi ambapo tathmini imefanyika ingawa huu mradi wa ujenzi wa daraja la kigamboni unategemewa kukamilika Januari, 2015” mkurugenzi mkuu wa NSSF anaeleza.

Daktari Dau anaendelea kusema ya kwamba ujenzi wa ofisi na vitega uchumi umekamilika katika mikoa ya Arusha, Kigoma pamoja na wilaya ya Kahama. Aidha, ujenzi unaendelea katika mikoa ya Morogoro, Shinyanga, Moshi, Mwanza, wilaya za Ilala na Temeke pamoja na ujenzi wa kambi ya Jeshi eneo la Kihangaiko, Wami za Jeshi la wananchi (TPDF) kwa kutumia mitambo ya UBM  pamoja na ujenzi wa ofisi za kumbukumbu za wanachama katika mikoa ya Kilimanjaro na Mara tayari umeshakamilika.

Dau anasema shirika limeshamekamilisha utayarishaji wa eneo la zahanati ya Apollo kwenye jengo la Mwalimu Julius Nyerere lililopo barabara ya Bibi Titi/Morogoro, Dar es Salaam ikiwemo na Ujenzi wa ofisi za Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) unaendelea na ujenzi wa jengo la Mzizima jijini Dar es Salaam ambao nao umeshaanza. Aidha ujenzi wa hoteli ya kisasa Mwanza, ujenzi wa kijiji cha kisasa Kigamboni (Tuangoma na Dungu “Farm”) upo katika hatua za kupata makampuni ya ujenzi na katika kutekeleza mpango wa kufanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam mpaka Chalinze, NSSF imeingia makubaliano na kampuni ya Malaysia kwa kuwasilisha maombi ya kazi ya ujenzi wa barabara hiyo.

“Aidha katika mwaka wa fedha 2013/14 Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii linategemea  kukusanya jumla ya shilingi trilioni 1.2 na kutumia kiasi hicho cha fedha kulipia mafao ya wanachama, kuwekeza kwenye vitega uchumi mbalimbali, gharama za uendeshaji na miradi ya maendeleo;na kuendelea kutoa elimu kwa wanachama, waajiri na umma kwa ujumla ili waweze kuelewa vizuri mfumo wa hifadhi ya jamii, Shirika litaendelea na mpango wa kupima Afya za wanachama wake, Kufanya Mkutano Mkuu wa Nne wa wadau wa NSSF, Kufanya tathimini ya uwezo wa mfuko kifedha ili kulipa mafao kwa wanachama wake kwa muda mrefu ujao na kuanza utekelezaji wa mradi wa uzalishaji umeme wa megawati 300 katika eneo la Mkuranga; na mradi wa uzalishaji umeme megawati 49 katika eneo la Malagarasi mkoa wa Kigoma” Daktari Dau anasema”

Anasema mwaka wa fedha 2013/14 Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii litaendelea na ujenzi wa Daraja la Kigamboni na ujenzi wa ofisi na vitega uchumi katika mikoa ya Morogoro, Shinyanga, Mbeya, Kilimanjaro, Mara, Mwanza, wilaya za Ilala, Temeke na Kinondoni, kushiriki katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Apollo jijini Dar es Salaam, na kuendelea na ujenzi wa ofisi za RITA na ujenzi wa jengo la Mzizima jijini Dar es Salaam, hoteli ya kisasa Mwanza, ujenzi wa kijiji cha Kisasa Kigamboni (Tuangoma na Dungu “Farm”), ujenzi wa kijiji cha kisasa Kigamboni (Azimio) na Ujenzi wa Jengo la Maadili Dar es Salaam pamoja na kuanza ujenzi wa kituo cha mabasi Mwandiga Kigoma, Kijiji cha Bunge Dodoma (MP’s Village); ofisi za Bunge Dar-es-Salaam na nyumba za watumishi wa Serikali nchi nzima.

Shirika la taifa la hifadhi ya jamii linakupa nafasi ya kumiliki nyumba ya kisasa zilizojengwa mtoni kijichi, kigamboni katika eneo la kuvutia lenye eneo maalumu la maduka, kituo cha afya. Nyumba hizi zinauzwa moja kwa moja na NSSF bila kupitia benki. Anasema nyumba hizo zipo 300 ndani ya eneo la mtoni kijicchi, kigamboni, umbali wa kilometa 15 kutoka katikati ya jiji la Dar es Salaam , Nyumba ni za vyumba 2 hadi 4 vyenye ukubwa wa mita za mraba 75 hadi 125. Unaweza kununua kwa fedha taslim au kwa mkopo wa miaka 15 kwa kutozwa riba ya asilimia 11.4 kwa mwaka na fomu zinapatikana ofisi za NSSF nchi nzima kwa tozo la shilingi 5000/ tu.

“Kwa ujumla nyumba ina sakafu ya vigae vyoo na bafu ndani , chumba kikuu chenye choo, jiko kubwa pamoja na maji ya moto, umeme na maji, na ili kuhakikishia usalama ni kwamba nyumba imejengwa kwa nondo za usalama kwenye milango na madirisha, madirisha ya kisasa, eneo la kuegesha gari na ukuta wa uzio kwa kila nyumba 50”. anasema mkurugenzi mkuu. 

“Sifa kubwa ya kuuziwa nyumba hizi na kumilikishwa ni kwa watanzania ambao ni wanachama wa NSSF au wanachama wapya watakaojiandikisha wakati wa manunuzi au watakao jiandikisha kama wanachama wa hiari kama tayari wapo kwenye mfuko mwingine wa hifadhi ya jamii na watanzania waishio nje ya nchi wenye mafao ya WESTADI”  Daktari Dau anabainisha.


Anasema utaratibu wa ununuzi wa nyumba hizi kwa kutoa fedha taslimu yaani papo kwa papo na kwa  kwa mkopo na kwamba fomu zote zinawasilishwa NSSF makao makuu ghorofa ya 11, kwa ajili ya kufanyiwa uchambuzi na baadaye mnunuzi mwenye sifa ataarifiwa kwa barua aina ya nyumba aliyopata na kupewa mkataba wa manunuzi na mnunuzi mwenye sifa atalipa kwa mkupuo au malipo ya miezi mitatu ya awali na bei inategemea ukubwa wa nyumba, idadi ya vyumba.  “Bei inaanzia shilingi milioni 65 hadi milioni 113 bila kodi na malipo yote yanatakiwa kufanyika NSSF na vigezo na masharti kuzingatiwa” mkurugenzi mkuu anasisitiza.


Mkurugenzi mkuu anasema shughuli za uwekezaji za shirika zinafanywa chini ya ibara ya 62 ya sheria Na 28 ya mwaka 1997 na sera ya uwekezaji ya shirika ambayo inafanyiwa marekebisho ya mara kwa mara ili iendane na mabadiliko ya uchumi ndani na nje ya nchi.

Shirika linafanya uwekezaji katika miradi mbalimbali kwa malengo ya kulinda thamani ya michango ya wanachama, kupata fedha za uendeshaji wa shughuli za shirika, kuboresha mafao kwa wanachama na kuchangia juhudi za serikali katika kuinuia uchumi wa nchi, shirika kwa kufuata kanuni za usalama wa mtaji, uwezo wa kuleta faida, uwezo wa kitega uchumi kubadilika kuwa fedha taslimu, kuchangia masuala ya kijamii, na kutawanya uwekezaji” anasisitiza
kwa kuzingatia kanuni zilizopo hapo juu shirika huwekekeza katika maeneo tofauti kwa viwango tofauti kulingana na sera ya uwekezaji kama vile kwenye dhamana za kiserikali, akiba ya muda maalumu, miradi ya ujenzi, hisa kwenye makampuni, mikopo kwa makampuni, dhamana za makampuni na hisa kwenye soko la mtaji.

No comments :

Post a Comment