Thursday, April 3, 2014

Mifuko ya hifadhi ya jamii na huduma kwa wateja




 http://www.emporis.com/images/show/881463-Large.jpg
 Mojawapo ya majengo ya vitega uchumi ya Mfuko wa pensheni wa PSPF lililopo mjini Dar es salaam

Na Christian Gaya majira April 01,  2014

Mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii nchini inatakiwa kujiwekea malengo na mikakati mbalimbali ili kuleta ufanisi na tija katika shughuli za ulipaji wa mafao. Nafikiri mmeona baadhi ya taasisi za kifedha hasa mabenki na mengineyo wana na utaratibu wa kuwa na mapatano ya utoaji wa hudhuma baina taasisi hizo na wateja wao kwa kuanzisha mikataba ya huduma kwa wateja.



Ambapo mikataba hiyo inakuwa ni hatua muhimu sana katika utoaji wa huduma bora katika misingi ya uwazi na uwajibikaji. Kwa kufanya hivyo kwa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii wateja wao ambao ni wanachama, wastaafu na familia zao, waliojiajiri wenyewe, na  wageni wanaofanya kazi kwa mikataba watapata uhuru na uelewa wa kufahamu matarajio yao katika huduma zinazotolewa na mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii na hata viwango vya muda ambavyo vitawawezesha kupanga mambo yao wateja vyema kabisa bila kusumbuka, badala ya kusubiri huduma bila ya kufahamu upatikaji wake wa huduma hizo na kwa viwango fulani vilivyoanishwa wazi kwa wateja wa ndani na wa nje. 


Mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii kwa kufanya hivyo itawezesha kuwa na mapatano yatakayowawezesha wateja wao kufahamu huduma zinatolewa na mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii, vikiwemo na hata viwango vya huduma na hatua ambazo mteja anaweza kuzichukua iwapo viwango vya huduma vitakuwa kinyume na matarajio ya mkataba.


Jambo la kuangalia kuhusu mifuko ya pensheni ni kujua bidhaa au huduma zake. Je huduma hiyo inahitajika na watu wote, chukua mfano wa chumvi. Hivyo jaribu kujiunga na mfuko wa pensheni ambayo huduma zake zinahitajika na wengi au wafanyakazi wengi na familia zao, pamoja na wazee, vijana, watoto, walemavu, wajane, pamoja na watoto yatima kwa kukidhi mahitaji yao wanapopatwa na majangwa ya aina mbalimbali. Lazima ujiulize kama je huduma zinazotolewa na mfuko wa pensheni zina mbadala au hazina mbadala. Na hiyo huduma ina uhakika mkubwa wa soko. Ina nguvu kubwa ya ukiritimba nikiwa na maana ya kuwa na uwezo wa huduma kuwa na soko kubwa lenye uwezo wa kudai bei kubwa bila kupunguza uhitaji na matumizi. Hivyo tafuta andika na jiunge na mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii wenye huduma zenye sifa nzuri. 


Unahitaji kufanya uchunguzi wa kutosha au kina kuhusu utendaji wa mifuko hii hasa kwa kufanya utafiti wa kutambua thamani, soko, kutatua udhaifu, kutoa majibu ya maswali tata, kupata taarifa zaidi na za uhakika. Kujiunga na mfuko wa pensheni wowote wa hifadhi ya jamii ni kutafuta sehemu yenye usalama ya kuweza kuwekeza michango yako ya kila mwezi  kwa ajili ya aina mbalimbali ya majanga yanayoweza kusababishwa na ugonjwa, kuumia ukiwa kazini, kifo, kupata ulemavu, na kadhalika. Hivyo unahitaji kufanya utafiti wa makini sana kwa kuchunguza taarifa mbalimbali juu ya mfuko huo wa hifadhi ya jamii unaotaka kujiunga nao ili taarifa hizo ziweze kukusaidia kutoa maamuzi wa busara wa kukuwezesha kuzingatia kanuni misingi na vigezo maalumu ambazo vitakusaidia kujibu maswali mengi. 


Baadhi ya maswali muhimu yanaweza kuwa kama vile utawezekeza wapi? Na mfuko upi wa pensheni ya hifadhi ya jamii, na watakata kiasi cha asilimia ngapi kutoka katika mshahara wangu, na mwajiri wangu yeye atatoa kiasi cha asilimia ngapi kama umeajiriwa. Hivyo ni juu ya mfanyakazi mwenyewe kama mwekezaji kufanya utatafiti wa kina ili kujua ubora wa mfuko huo unaotegemea kujiunga nao kabla ya kujisajiri. Unatakiwa usiwe mwepesi wa kufanya maamuzi bila kwanza kuwekeza kwenye utafiti hasa kama vile kuwaona wataaalamu wanao weza kukusaidia kukupa ushauri mahiri. 


Ni muhimu kuangalia mifuko hii ya pensheni kwa kuangalia uongozi, yaani menejimenti, hali ya kifedha, thamani ya mfuko wa pensheni kwa sasa, taarifa mbalimbali, matarajio ya mfuko wa pensheni  kwa kipindi kijacho kama pamoja na thamani ya mfuko wa pensheni kwa miaka ijayo.  Uchambuzi unahitajika uwe unaolenga zaidi katika kuchambua thamani ya mfuko wa pensheni kutokana na taarifa halisi zilizopo na siyo taarifa za matarajio ya baadaye. Mchangiaji wa michango au Mwekezaji makini anatakiwa aweke mkazo katika kufanya makosa makubwa kwa sababu uchunguzi au utafiti au upembuzi wa mifuko hii ya pensheni ya hifadhi ya jamii inatakiwa ufanyike kisanyansi kwa kuzingatia uchambuzi wa takwimu na uchambuzi nyinginezo ingawa vigezo hivi vya takwimu vinaweza kuwa muhimu lakini mara nyingi huwa havijitesholezi hata kidogo. Hivyo shughuli kubwa katika mambo ya kujiunga au kujisali na mifuko hii ya pensheni ya hifadhi ya jamii inatakiwa kufanya utafiti, ingawa unagharimu muda mwingi kabla ya maamuzi sahihi. 


Uamuzi wa kuwa mwanachama wa mfuko wa pensheni ya hifadhi ya jamii unatakiwa utokana na takwimu na taarifa nyinginezo makini zinazotakiwa zifanywe na mfanyakazi mwenyewe na siyo kufuata mkumbo wa watu wengi wanasemaje. Kwa kufanya hivyo tumeona mara nyingi wafanyakazi wengi hukosea kwa sababu alifuata mazungumzo ya watu wengi juu ya mfuko fulani wa pensheni hivyo anatakiwa kufanya utafiti na uamuzi wake ufuate utafiti na takwimu siyo uzushi au habari motomoto ambazo hazijafanyiwa uchunguzi wowote. unahitaji wewe kama mfanyakazi kuhakikisha ya kuwa unafanya utafiti au uchunguzi wa kina  na kuchambua ripoti za kila mwaka za mifuko ya hifadhi ya jamii huku ukuzingatia yale yanayotendeka katika sekta tofauti nchini na kwingineko katika nyanja za mifuko ya hifadhi ya jamii.  


Unahitaji kujua usalama wa michango yako unayochangia kila mwezi. Lazima ujue hiyo michango yako huwekezwa mahali ambapo uwezekano wa kupata hasara ni mdogo sana, na kuchunguza kama huwekezwa sehemu ambapo kuna uwezekano mkubwa wa kupata faida. Hii ijulikane na itambulike ya kuwa kiupambele katika ufuatiliaji wake kwenye michango yako au fedha yako unayochangia kwanza inatakiwa kuwa na usalama wake na siyo faida. Kipa umbele hapa kwanza ni inatakiwa kuwa michango yako na siyo faida unayotakiwa kutarajia. Faida inatakiwa kushika nafasi ya tatu na siyo nafasi ya kwanza au ya pili. 


Unatakiwa kulikumbuka hili jambo sana ukitaki ufanikiwe kutokana na mifuko hii ya pensheni ya hifadhi ya jamii hakikisha unafanya utafiti au uchunguzi kuhakikisha ya kuwa mfuko unafuata utaratibu wa kisayansi wa uwekezaji wa michango yako kwa kufuata kanuni za kulinda usalama wa fedha zako unazotegemea kuchangia na uwekezajji uwe ule wa kuleta faida na kuwa na uwezo wa kitega uchumi kubadili kuwa fedha taslim na siyo vinginevyo, na mfuko ambao unajitoa kuchangia masuala ya kijamii inayoizunguka na kuwa na uwezo mkubwa wa kutawanya uwekezezaji wa michango yako bila kufuata misukumo ya wanasiasa badala ya kufuata kanuni za kulinda usalama wa michango yako ya pensheni. 


Hata hivyo, ili mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii iweze kutoa huduma bora kwa wakati kama ulivyokusudiwa katika mapatano hayo, lazima wategemee kupata muuitikio na ushirikiano kutoka kwa wateja ili kutimiza makubaliano yaliyowekwa katika mkataba. Na mifuko ya pensheni ya hifadhi ikumbuke ya kuwa wateja ndiyo viungo muhimu katika kufanikisha utekelezaji wa malengo ya kila siku ya mifuko, kwa kuwa taarifa zinazotoka ndizo zinazowezesha mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii kutoa huduma stahiki. 


Utahitaji kujifunza zaidi utendaji wa mifuko ya pensheni kutoka kwa wataalamu na mamlaka inayohusika kama vile mdhibiti na msimamizi wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii yaani SSRA na hata kwenye makala za kijamii kama vile makala za hakipensheni


Sawa umepewa uhuru huo wa kuchagua kujiunga na mifuko hii ya pensheni, hivyo ningependa kukuuliza wewe mfanyakazi uliyeajiriwa leo je unajua mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii unaotoa mafao bora zaidi ya kulingana na kiwango cha shirika la kazi duniani ILO? yaani kwa idadi ya mafao, ubora wa mafao, na kulipwa pensheni kulingana na ukali wa maisha ya kila siku. 


Mfanyakazi unahitaji kujua kiundani zaidi juu ya ubora wa mifuko hii ya pensheni ya hifadhi ya jamii, lazima ujue hata viwango vya ubora huduma zao, mazingira ya sehemu unapopatiwa huduma kuanzia getini kwa askari mpaka unapofungulia madai ambapo yanahitaji kuwa sehemu za kuvutia zaidi. Je huchukua siku ngapi kupata hundi yako ya pensheni au ya mafao ya kujitoa, je ahadi zako zinatekelezwa kama walivyokuahidi, na anayekuhudumia anakuchagamukia na kukuhudumia kama ndiye mfalme wa mfuko huo wa pensheni. Je hao wafanyakazi wa mifuko ya pensheni wanajua ya kuwa wewe ndiye mwajiri wao. 


Wanaandaa pensheni yako ya kustaafu baada ya mwezi mmoja kama walivyokuahidi. Kuna mambo mengi ya kuchunguza kwanza kabla ya kujiunga hasa kama mwanachama mchangiaji utahitaji kujua kwanza utaratibu wa kujisajiri kiwango cha kuchangia ni asilimia ngapi ya kipato chako cha mwezi, mchango huo unakatwa kwenye mshahara kabla ya marupurupu mengine au baada ya kuchanganya na marupurupu mengine yaani kwenye basic salary au kwenye gross salary. Je mafao yako ya pensheni yanakatwa kodi au hayakatwi.


Na lazima ujue ni kwa sababu gani ukate kwenye basic au gross salary. Na ni nani anayetakiwa kukuandikisha wewe kwenye mfuko huo wa pensheni. Na kiwango gani mwajiri naye inatakiwa akuchangie ili ichanganye pamoja na kupelekwa kwenye mfuko wa pensheni. Na hiyo michango inatakiwa ipelekwa kwenye huo mfuko kwa wakati gani wa muafaka. Je ni wajibu wa nani kuhakikisha kuwa michango hiyo inapelekwa kwenye mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii. Na chama cha wafanyakazi kina wajibu gani juu ya michango hii ya pensheni kazini. 


Je mfumo gani wa hifadhi ya jamii ni wa pensheni au wa akiba ya wafanyakazi. Ni aina gani ya mafao yanayotolewa na mfuko huo wa hifadhi ya jamii. Je kuna mafao ambayo unaweza kunufaika wakati unapoendelea kufanya kazi yaani ya muda mfupi na ya yale ambayo utanufaika baada ya kustaafu yaani ya muda mrefu. Je familia yako unawezaje naye kunufaika na mafao hayo ya muda mrefu na ya muda mfupi. Je ukusanyaji wa michango ya pensheni una urasimu mwingi na usio na uwazi na ukweli kwa mchangiaji. 


Je mipango ya malipo ya mafao kwa mwanachama inalipwa kwa wakati muafaka na kwa usahihi wa uhakika kabisa bila ya mapunjo au kuzidishiwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Je wanachama anaweza kutegemea kupata habari zote na ushauri na zilizokamilika karibu na mahali karibu anapoishi. Mwanachama anaweza kupata habari na ushauri wowote hata bila ya kuanza yeye kudai huduma hiyo. Je muda unaotumika kukokotoa mafao yake ya pensheni ni mfupi au ni wa muda mrefu. 


Je maamuzi yeyote juu ya huduma za mwanachama zinahudumiwa kirafiki. Ni muhimu vile vile kama mwanachama kujua wewe kama mchangiaji pamoja na mwajiri wako kila mmoja ana wajibu gani kwenye mfuko huo wa hifadhi ya jamii. Mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii lazima uweke wazi juu ya haki za wanachama hasa zile za kumruhusu mwanachama kuapili kwenye bodi ya sheria au mahakamani atakapoona kwamba pale hajatendelewa haki inavyotakiwa na mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii. Kama wanachama mchangiaji wa mfuko wa pensheni je utashirikishwaje kwenye maamuzi na uendeshaji wa mfuko huo na kwa faida ya nani. Sasa ni juu ya mfanyakazi mwenyewe kuchagua kwa kutumia vigezo vya kitaalamu 


Hivyo kuna haja kubwa kila mfuko wa pensheni ya hifadhi ya jamii kuwa na mkataba wa huduma kwa wateja wao ili kukuza uelewa kuhusu upatikanaji wa huduma na ubora wa huduma zinazotolewa  na mifuko hii pensheni ya hifadhi ya jamii. Hii itawezekana kabisa hasa kwa kuwa na dhamira ya kuwasaidia wanachama, wastaafu na familia zao na wadau wengine wa hifadhi ya ja namna ya kuboresha na kutoa huduma bora zaidi mii nchini kuzielewa shughuli za mifuko kwa ujumla, na namna ya kuwasiliana na mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii pamoja na viwango vya huduma vinavyotarajiwa na jinsi hata kutatua matatizo kwa muda muafaka pale yanapojitokeza. Mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii itambue ya kwamba kuwa na mkataba wa huduma kwa wateja utawezesha wateja wao kujua mafao yatolewayo, haki na wajibu wao ndani ya mifuko hiyo na kwa upande mwingine mifuko hii ya hifadhi ya jamii itatoa fursa za wazi kwa wateja kuwasiliana na mifuko ili kutoa mapendekezo ya namna ya kutoa huduma bora zaidi.

No comments :

Post a Comment