Friday, May 3, 2013

Utawala na uongozi bora wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii



 


Kama manejimenti inayohusika na kuendesha na kusimamia mfuko  wa hifadhi ya jamii wafahamu ya kama kweli wanazingatia utaratibu na kanuni za utawala bora kuwa utawala bora basi hawana budi kuhakikisha kuwa mfuko unaendeshwa na kuongozwa na utawala bora na kwa ufanisi wa hali ya juu zaidi. Na ikumbukwe ya kuwa wanachama ndio waliotoa fedha zao kila mwezi kama mtaji wa kuendesha mfuko na wanatarajia ya kuwa watapata huduma kama walivyoahidiwa pale wanapokumbana na majanga ya aina mbalimbali kama vile ya kuumia na kupatwa na magonjwa yanayotokana na kazi, ujauzito na kujifungua mtoto, kuugua kufiwa na aliyekuwa mwanachama na alikuwa anategemewa na familia, kufikia umri wa kustaafu  na mengineyo.



Hivyo kama mwanachama na kama unahitaji kuwa mwanachama unahitaji kujiuliza maswali mengi juu ya mfuko wa hifadhi ya jamii unaotaka kujiunga nao kama linazingatia kanuni na vigezo vya utawala bora. Kama mfuko huo unazingatia kanuni za uongozi bora huenda kukawa na uwezokano mkubwa kwa mfuko kuwa na utendaji mzuri unaofikia malengo na kukidhi matarajio ya wanachama wake na familia zao. Nafikiri mmeshuhudia hata baadhi ya taasisi na makampuni makubwa ya kimataifa ufilisika na kuanguka na mara nyingi makampuni haya yamekuwa yakitoa taarifa za uongo za matumizi ya fedha na za kiutendaji, na wizi uliokithiri, malipo na marupurupu yasiyoya kawaida kwa viongozi, mifumo ya ndani dhaifu ya udhibiti wa fedha, kushidwa kudhibiti hatari na majanga, mawasiliano duni kati viongozi na wanachama na uendeshaji mbaya unaosababisha wanahisa kupoteza mitaji yao na kupata hasara. Mara nyingi wanachama wamekuwa wakijiuliza kuwa imekuwaje viongozi hawakujua kuwa kuna hatari ya kufilisika? 

Mfano mzuri ni huu wa mfuko pensheni wa watumishi wa serikali (PSPF) kaimu mkurugenzi mkuu ndugu Adam Mayingu anasema kuwa mfuko katika hali mbaya kifedha na mambo yakiendelea hivyo hivyo kwa muda wa miaka mitatu mfululizo huenda mfuko ukafilisika na mpaka sasa mfuko umepungua uwezo wa asilimia 10 kutoka katika kiwango kiwango kinachotakiwa cha asilimia 40. Na kwamba hali ikiendelea hivi itabidi serikali kama mdhamini wa mfuko na mdaiwa mkubwa wa mfuko huo itabidi iwajibike kulipa michango na mafao yote ya wanachama 



Taarifa inaonyesha kuwa kutokana na utafiti uliofanya na wataalam wa pensheni unaonyesha kuwa PSPF hauna fedha tena za kulipia mafao ya wanachama wake, ingawa kabla ya kuanzishwa mfuko huu wa PSPF mwaka 1999 serikali ilifanya utafifi na kuonyesha ya kuwa serikali ilikuwa na malimbikizo ya jumla ya bilioni 250 za kitanzania kama michango ya wafanyakazi. Kabla yamwaka 1999 mfuko ulikuwa ukichangiwa na serikali tu na watumishi wote wa serikali walikuwa hawakatwi katika mishahara yao, lakini baada ya kubadilishwa mwaka 1999 na kiuitwa PSPF wanachama wake wote  walianza rasmi kuchangia nao. Na mpaka kufikia mwaka 2006 malimbikizo hayo yalifikia kiasi cha shilingi bilioni 658.23 na kama serikali haijalipa mpaka leo njia nyingine ni kwamba PSPF inatakiwa kuongeza kiwango cha kuchangia kutoka katika mishahara ya wanachama wake ili kuendeleza mfuko ama ndio uwe mwisho wake.


PSPF ni taasisi ya hifadhi ya hifadhi ya jamii iliyoanzishwa kwa sheria namba 2 ya mafao ya hitimisho la kazi kwa watumishi wa umma ya mwaka 1999. Mpaka sasa watumishi wa serikali pamoja na wakala za serikali huchangia asilimia 5 ya mshahara wa mtumishi na waajiri wao huchangia asilimia 15. Inaonyesha mfuko ulianzishwa bila kuwa na mtaji wa kuanzia kutokana na malimbikizo ya michango ya watumishi (wafanyakazi) wa serikali kutolipwa na serikali



Kiwango au kiasi cha mfuko wakati huo kilichotakiwa na serikali ilitakiwa kuchangia asilimia 93.3 ingawa tangia hapo serkali haikuweza kutoa kiasi chochote, ingawa naibu wa fedha mheshimiwa Janeth Mbene aliiambia kamati ya mahesabu ya umma ya bunge ya kwamba kwa mwaka huu wa fedha serikali itapunguza deni hilo kwa kiasi cha shilingi bilioni 50 kwa kuilipa PSPF. 


Katika kipindi cha pili cha utafiti uliofanywa baaada ya PSPF kuanza kulipa mafao kwa wanachama wake mwaka 2007, taarifa za kifedha ilionyesha kuwa mfuko ulizidi kuzorota zaidi kwa kuwa na upungufu wa fedha za mafao kufikia trilioni 3.3 za kitanzania ukilinganisha na malimbikizo ya kabla ya mwaka 1999 ya billion 250 za kitanzania zilizokuwa zinadiiwa na PSPF kutoka serikalini.

No comments :

Post a Comment