Tuesday, May 29, 2012

Balozi Seif aitaka NSSF kuongeza wanachama

3rd February 2012
Chapa
Maoni
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd
Mfuko wa Hifadhi za Jamii nchini (NSSF), umetakiwa kuhakikisha unaongeza  idadi ya wanachama wake,  ili kuongeza idadi iliopo zaidi.

Changamoto hiyo ilitolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, katika sherehe za ufunguzi wa kongamano la pili la wadau wa mfuko huo wa kimataifa.
Balozi Idd alisema NSSF na mifuko mingine imeelekeza nguvu zake kwa kupata wanachama kutoka sekta rasmi tu na ndio maana wanachama waliopo hawafiki milioni moja.
Alisema hiyo ni kasoro kubwa inayohitajika kurekebishwa mara moja na kuna haja kwa uongozi wake kuchukua juhudi za makusudi kuongeza wanachama kutoka sekta kama kilimo ambayo Watanzania wengi zaidi wanajishughulisha nayo kuliko sekta nyingine.
Alisema zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanajishughulisha na kilimo na kundi hilo ni muhimu sana kwa mfuko huo kama sekta hiyo itaandaliwa utaratibu mzuri.
Alisema mafanikio yaliyofikiwa na NSSF ni makubwa katika uwekezaji wa vitega uchumi vya ndani ya nchi, kwa misingi hiyo mafanikio hayo yanapaswa kwenda sambamba na kuyafanya mafao ya wanachama wake kuwa bora zaidi na makubwa zaidi.
Pia alitoa changamoto kwa mifuko yote ya hifadhi za jamii nchini kujitahidi kuyafanya mafao na malipo mengine kwa wanachama wao kuwa mazuri zaidi.
Balozi Idd aliisifu NSSF kuwa na mradi wa nyumba za bei nafuu jijini Dar es Salaam na kusema kuwa mradi huo unapaswa kuendelezwa nchini kote kwani gharama za ujenzi za nyumba kwa wanachama wa kawaida au hata mtu wa kawaida ni kubwa mno.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pia inao mpango wa aina hiyo kutokana na hali hiyo inaialika NSSF kwenda Zanzibar kushirikiana na ZSSF kuwekeza katika mpango huo.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa NSSF, Dk. Ramadhani Dau, alisema  mafaniko mengi ya mfuko huo nchini ni kwa kubuni miradi mingi ya maendeleo na kuongeza kiwango cha pensheni ambacho kimepanda kutoka Sh. 52,000 hadi Sh. 80,000.
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment