Saturday, February 25, 2023

JK AMSHUKURU RAIS MSTAAFU BUSH KWA KUANZISHA MPANGO WA PEPFAR KUOKOA MAISHA YA WATANZANIA

 

Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  amemshukuru Rais Mstaafu wa Marekani George W. Bush kwa uamuzi alioufanya kusaidia mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kuanzisha mpango wa Dharura wa Rais wa kupambana na UKIMWI PEPFAR ambapo serikali ya Marekani hutoa fedha za kununua dawa (ARVs) za kufubaza vijidudu vinavyosababisha maambukizi ya UKIMWI kwa watu walioathirika. 
Dkt. Kikwete amesema mpango huo umeokoa maisha ya mamilioni ya binadamu ambapo kwa sasa UKIMWI sio "adhabu ya kifo". Dkt. Kikwete ambaye alialikwa na muasisi wa mpango huo, Rais Mstaafu wa Marekani George W. Bush,  katika kusherehekea miaka 20 tangu kuanzishwa kwa mpango huo jijini Washington DC. Ijumaa, Feb. 24, 2023.
Katika tulio hili, tutaangalia Mafanikio yaliyopatikana kutokana na mpango wa PEPFAR na kujifunza ni modeli gani inaweza kufanyia ushiriki wa Marekani katika masuala ya Afya Duniani na kuendelea kwa upana zaidi.

Wakati Rais Bush anatangaza PEPFAR mwaka 2003, kwa uchache watu 50,000 chini ya jangwa la Sahara ndio Walikuwa na fursa ya kupata ARVs.

Leo hii inakadiriwa mpango wa PEPFAR ambao unaendelea kutekelezwa katika Nchi zaidi ya 50 umeokoa maisha ya watu milioni 25.

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha na Bi. Nancy Pelosi, Spika Mstaafu wa Bunge la Marekani kutoka Chama cha Democratic, walipokutana katika Maadhimisho ya Miaka 20 ya PEPFAR Jijini Washington DC, Marekani
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na Bilionea Bill Gates.

PEPFAR ILIVYOANZISHWA

Wakati Rais Bush anatangaza PEPFAR mwaka 2003, kwa uchache watu 50,000 chini ya jangwa la Sahara ndio Walikuwa na fursa ya kupata ARVs.

Leo hii inakadiriwa mpango wa PEPFAR ambao unaendelea kutekelezwa katika Nchi zaidi ya 50 umeokoa maisha ya watu milioni 25.

Ingawa jukumu la PEPFAR ni kuzuia, kujali na kutibu HIV, athari chanya za mpango huo zimepindukia malengo hayo.

 PEPFAR imeweza kuimarisha mifumo ya utoaji huduma za Afya,  kushajihisha demokrasia, kukuza uchumi na kuendelea haki za binadamu.

Mafanikio ya mpango wa PEPFAR, kwa kiasi kikubwa yanatokana na uwajibikaji, uwazi, athari chanya, usawa.

Msingi wa maadili haya, PEPFAR umekuwa  katika ukusanyaji taarifa na kuitumia kwa wakati.

Hali hii inapelekea kuwa na programu endelevua, imara na isiyotetereka, ambayo umetoa fursa ya kupanua Huduma za kuokoa maisha licha ya ufinyu wa bajeti.

PEPFAR umekuwa ni ushindi kwa pande zote mbili Mataifa nufaika na sera za mambo ya kigeni za Marekani.

 Lakini kazi bado haijaisha hususan kujali miongoni mwa makundi ya mabinti, akina mama, watoto na makundi mengine ambayo YAKO hatatini na maambukizi.  

Baraza la Congress na wananchi wa Marekani lazima waendelee kuungamkono mpango wa PEPFAR hadi hapo HIV/AIDS sio tishio tena.

Kuacha kuunga mkono mpango huu kutapelekea uwekezaji wa PEPFAR na maisha ya watu hatatini.

Katika tulio hili, tutaangalia Mafanikio yaliyopatikana kutokana na mpango wa PEPFAR na kujifunza ni modeli gani inaweza kufanyia ushiriki wa Marekani katika masuala ya Afya Duniani na kuendelea kwa upana zaidi.

Tutawasikia wale wote walioasisi uanzishwaji wa mpango huu, waliofaidika, na wote ambao wanaendelea kufanyia Kazi kila siku katika mapambano ya kutokomeza UKIMWI Duniani.

 Chanzo:Bush Centre.

No comments :

Post a Comment