RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia wakati wa sherehe za kupongezwa zilizoandaliwa na Wauguzi wa Zanzibar kwa kutimiza miaka miwili ya Uongozi wake, zilizofanyika leo 20-12-2022 katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu) WAUGUZI Zanzibar wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) wakati wa sherehe za kumpongeza kwa kutimiza miaka miwili ya Uongozi zilizofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja Jijini Zanzibar leo 20-12-2022.(Picha na Ikulu) RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Bi.Rabia Mzee Mataka wa Kitengo cha Shirikishi cha Afya na Uzazi Zanzibar, wakati akitembelea maonesho ya sherehe ya kumpongeza kwa kutimiza miaka miwili ya uongozi wake, iliyoandaliwa na Wauguzi Zanzibar,katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Wilaya ya Mjini Unguja na (kulia kwa Rais) Waziri wa Afya Zanzibar Mhe.Ahmed Nassor Mazrui na Mkuu wa Wilaya ya Mjini Unguja Mhe.Rashid Simai Msaraka.(Picha na Ikulu) RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa TUZO Maalum ya Kutimiza Miaka Miwili ya Uongozi wake,iliyotolewa na Wauguzi Zanzibar akikabidhiwa na Muunguzi Bi. Maryam Rashid Suleiman, wakati wa sherehe za kumpongeza zilizofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja leo 20-12-2022, na (kulia kwa Muunguzi) Waziri wa Afya Zanzibar Mhe.Nassor Ahmed Mazrui na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Wilaya ya Mjini Unguja Mhe.Rashid Simai Msaraka.(Picha na Ikulu) 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikata keki maalum ya kumpongeza kwa kutimia miaka miwili ya Uongozi wake, wakati wa sherehe za kumpongeza zilizoandaliwa na Wauguzi Zanzibar katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja Jijini Zanzibar leo 20-12-2022, na (kulia kwa Rais) Muunguzi Bi. Maimuna Ibrahim, Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui na Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hassan K. Hafidh na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Wilaya ya Mjini Mhe. Rashid Simai Msaraka na Mwenyekiti wa Baraza la Wauguzi Zanzibar Prof. Amina Abdulkadir Ali.(Picha na Ikulu)