Wednesday, June 2, 2021

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII, MHE.MASANJA AELEZA UMUHIMU WA BONDE LA KILOMBERO .

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akijibu swali Bungeni leo Jijini Dodoma  ambapo pamoja na mambo mengine amesema Bonde la Pori tengefu la Mto Kilombero ni muhimu Kitaifa na Kimataifa kutokana na uhifadhi wa bionuwai zilizo  adimu Duniani kama vile mnyama aina ya sheshe.

********************************

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja amesema Bonde la Pori Tengefu la  Kilombero ni sehemu ya ardhioevu linalochangia asilimia 62.5 ya maji yote ya mto rufiji hivyo kuwa

chanzo muhimu cha maji kwa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere

Amesema Bonde hilo lina umuhimu  kitaifa na Kimataifa kutokana na uhifadhi wa bionuwai zilizo  adimu Duniani kama vile mnyama aina ya sheshe.

 

No comments :

Post a Comment