Wednesday, May 5, 2021

UZALISHWAJI WA BIDHAA ZINAZOKIDHI MATAKWA YA VIWANGO VIWANDANI HUKUZA UCHUMI WA NCHI

Mkakati mmoja wapo wa kukuza Uchumi wa nchi kupitia viwanda ni kuhakikisha viwanda vinazalisha bidhaa ambazo zinakidhi matakwa ya viwango husika na kufanya hivyo bidhaa zitapata masoko yawe ya ndani ama ya nje.

Ameyasema hayo leo Meneja wa Mafunzo na Utafiti katika Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mwl.Hamisi Mwanasala alipokuwa akizungumza na mwandishi wetu katika ofisi za TBS Jijini Dar es Salaam.

Aidha Mwl.Mwanasala amesema kuwa viwango vinasaidia kutayarisha bidhaa iwe na ubora na kukubarika katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

"Kiwango ni muhimu katika kuona kwamba bidhaa inazalishwa iliyobora na salama na kuwezesha kupata masoko na kukubarika na wateja wa bidhaa husika". Amesema Mwl.Mwanasala.

Pamoja na hayo Mwl.Mwanasala amesema kusudio la uwepo wa maadhimisho ya siku ya viwango Afrika ni kwaajili ya kuenzi kazi kubwa iliyofanywa na wadau mbalimbali wanaosimamia na kujishughulisha na masuala ya uendelezaji wa viwango.

Shirika la Viwango Afrika (ARSO) liliandaa mashindano Insha kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati ambapo Tanzania mashindano yanasimamiwa na Shirika la Viwango Tanzania TBS, ikiwa Siku ya Maadhimisho ya Siku ya Viwango Afrika Mei 6 mwaka huu washindi 10 watakabidhiwa zawadi na watapelekwa kwenye mashindano ya Afrika kuiwakilisha Tanzania.

 

No comments :

Post a Comment