Wednesday, May 5, 2021

SOKO JIPYA KISUTU JIJINI DAR KUANZA MEI 30, MACHINJIO YA VINGUNGUTI KUMENOGA


 
Meya wa Jiji la Dar es Salam Omari Kumbilamoto(katikati) akiwa na watendaji wengine wa Jiji hilo pamoja na madiwani wa Kamati ya Fedha wakiangalia mchoro wa jengo jipya la soko la Kisutu ambalo linatarajiwa kuanza kutumika rasmi Mei 30 mwaka huu.
Ofisa Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa Jiji la Dar es Salaam Tabu Shaibu(wa pili kulia) akifafanua jambo wakati wa ziara ya madiwani wa Kamati ya Fedha pamoja na watendaji wa Jiji hilo kufanya ziara ya kutembelea soko hilo leo Mei 3,2021.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam Omari Kumbilamoto akifafanua jambo wakati alipotembelea soko la Kisutu akiwa na wajumbe wa Kamati ya Fedha pamoja na watendaji wa Jiji hilo.



Mmoja wa maofisa wa Jiji la Dar es Salaa akielezea jambo kwa Meya wa Jiji hilo pamoja na wajumbe wa Kamati ya Fedha baada ya kufanya ziara ya kutembelea soko hilo.
Mhandisi wa Jiji la Dar es Salaam John Magori akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua mbalimbali za ujenzi zinazoendelea katika soko la Kisutu.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha wa Jiji la Dar es Salaam wakiwa na Meya wa Jiji hilo Omari Kumbilamoto baada ya kufanya ziara katika soko la Kisutu ambalo linatarajiwa kuanza kutumika rasmi Mei 30 mwaka huu.
07:Meya wa Jiji la Dar es Salaam akiwa na wajumbe wa Kamati ya Fedha wakipata maelezo kuhusu ujenzi wa machinjio ya kisasa ya Vingunguti baada ya kutembelea machinjio hayo.





Muonekano wa nje wa jengo la Machinjio ya kisasa yaliyoko Vingunguti Jijini Dar es Salaam ambapo ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 97.


Meya wa Jiji la Dar es Salaam Omari Kumbilamoto akijadiliana jambo na maofisa wa Jiji hilo kabla ya kuanza kukagua ujenzi katika Machinjio ya kisasa Vingunguti.

 

Na Said Mwishehe, Michuzi TV

SOKO jipya la kisasa la Kisutu jijini Dar es Salaam linatarajiwa kuanza kutumika rasmi Mei 30 mwaka huu ambapo zaidi ya wafanyabiashara 1500 watakuwa wakifanya biashara zao sokoni hapo.

Hayo yamesemwa leo Mei 3,2021 na Meya wa Jiji la Dar es Salaam Omari Kumbilamboto baada ya Kamati ya Fedha kufanya ziara ya kukagua miradi ya kimkakati inayoendelea kutekelezwa katika Jiji hilo ukiwemo mradi wa soko hilo la kisasa la Kisutu pamoja na mradi wa ujenzi wa machinjio ya kisasa Vingunguti.

kizungumzia soko la Kisutu lenye ghorofa nne, Kumbilamoto amesema ujenzi wake umegharimu Sh.bilioni 13.49 na ujenzi umefikia asilimia 97." Leo tumefanya ziara ya kukagua miradi ya kimkakati iliyopo jijini Dar es Salaam, miradi ambayo tumeitembelea ni mradi wa soko la Kisutu pamoja na machinjio ya Vingunguti.

"Kwenye soko hili la Kisutu ni matarajio yetu Mei 30 mwaka huu wafanyabiashara waanze kufanya biashara zao hapa tutakuwa na wafanyabiashara wa aina zote.Awali kabla ya ujenzi huu kulikuwa na wafanyabiashara 696 lakini baada ya ujenzi huu litachukua wafanyabiashara 1500, hivyo hata mapato ya Jiji la Dar es Salaam yataongezeka,"amesema.

Kwa upande wa machinjio ya Vingunguti, Kumbilamoto amesema machinjio hayo nayo yanatarajiwa kuanza kutumika mwishoni mwa mwezi huu na ujenzi umekamilika kwa zaidi ya asilimia 96 na kiasi cha zaidi ya Sh.bilioni 12 zimetumika kujenga machinjio hayo.

Amefafanua kabla ya ujenzi wa machinjio hayo ya kisasa kwa siku zilikuwa zinachinjwa ng'ombe kati ya 500 hadi 550 lakini baada ya ujenzi ya ujenzi zitakuwa zinachinjwa ng'ombe 1500 na mbuzi 1000 , hivyo mapato yatakuwa makubwa yatakuwa yakipatikana na hivyo kutatua changamoto mbalimbali zilizopo.

"Lengo na madhumuni yetu ni kukagua miradi yote ya kimkakati inayosimamiwa na Jiji la Dar es Salaam ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa Ilani ya CCM ambayo tuliahidi kwa wananchi,"amesema Kumbilamoto.

No comments :

Post a Comment