Wednesday, February 10, 2021

MFUKO WA SELF WATOA ZAIDI YA BILLIONI 215 KATIKA KUWEZESHA WANANCHI KIUCHUMI

Waziri mkuu Kassim Majaliwa akisiliza jambo baada ya kutembelea banda la mfuko wa Self katika maonesho ya nne ya mifuko ya programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi kushoto ni Mkurugenzi wa biashara wa mfuko huo Mary Kipeja.
Mjasiriamali Lupen Tajiri akielezea namna alivyonufaika na mikopo kutoka mfuko wa Self.
Mmoja wa wananchi akiangalia jambo baada ya kutembelea banda Ia Self.
……………………………………………………………………………………
NA NAMNYAK KIVUYO, ARUSHA.
Tasisis ya serikali iliyopo chini ya wizara ya fedha ya Mfuko Self unaojihusisha na utoaji wa mikopo ya biashara, kilimo pamoja na mkopo  wa haraka wa wajasiriamali  umetoa mkopo wa billion 215 kwa wanufaika zaidi ya 100,000.
Akiongea na waandishi wa habari  mkurugenzi wa maendeleo ya biashara wa  mfuko huo  Mary Kipeja katika maonesho ya nne ya mifuko ya programu za uwezeshwaji wanawake kiuchumi yanayoendelea mkoani alisema kuwa mpaka sasa wameweza kuwafikia  wananchi 158,000 ambapo wana matarajio ya kuwafikia wananchi wengi zaidi.
Bi Kipeja  alisema wataweza kuwafikia wananchi wote kwani watafungua matawi mikoa yote nchini ambapo kwa sasa wapo Dar es salaam, Mbeya, Arusha, Mwanza, Zanzibar, Shinyanga pamoja na Dodoma.
Alieleza mfuko huo mbali na kutoa mikopo wanatoa elimu kwa wateja wao ili waweze kufikia malengo yao baada ya kuchukua mkopo wakaelekeze walipokusudia nasio kwenda kufanyi mambo mengine yatayowafanya washindwe kulipa.
Alifafanua kuwa lengo la mfuko huo ni kukuza na kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi hasa wa vijijini kwa kuwapa fursa ya kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali.
“Tunataka wananchi wajiongezee kipato na kuondokana na umasikini ambapo tunatoa mikopo ya jumla na mikopo ya kwaajili ya mtu mmoja mmoja hivyo na wakaribisha watanzania wrote wenye uhitaji kuja Self na kuondokana na changamoto ya ukosefu wa mitaji,” Alisema mkurugenzi huyo.
Mmoja wa wajasiriamali aliyenufaika na mkopo kutoka katika mfuko huo Lupen Tajiri ambaye no msindikaji wa maziwa kutoka katika kata ya Olturumet iliyopo wilayani Arumeru mkoani Arusha alisema kuwa  alishazungukabkatika tasisi nyingi za fedha lakini hakupata mafanikio kutokana na kuonekana kuwa hakopesheki lakini mfuko huo uliweza kumsaidia.
“Waliona andiko langu litaenda kuwasaidia wananchi wa chini ambao ndio ninanunua maziwa kutoka kwao na kuyasindika  kwa muda wa mwaka mmoja sasa na ninanunua kwa watu wa kawaida kabisa,” Alisema Lupen Tajiri.
Alieleza mfuko huo umemsaidia kutimiza malengo yake ya kuendeleza sekta ya maziwa ambapo awali hali nilikuwa ngumu kwani mabenki waliona kumkopesha ni kuingiza taasisi mashakani.
Aliendelea kusema kuwa biashara yake imekua na inahakikisha maziwa wanayoyasindika yana ubora ili kuweza kudumu sokoni  na kuendelea kupata faida itayoongeza kiwango cha ulipaji wa mkopo.

 

No comments :

Post a Comment