Tuesday, December 8, 2020

RAIS MAGUFULI AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MAJENGO MAPYA YA IKULU, CHAMWINO DODOMA ,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa Msimamizi wa ujenzi Luteni Kanali George William Nyisa wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa majengo ya ofisi mpya za  Ikulu Chamwino, Dodoma, leo Desemba 8, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua sehemu mbali mbali wakati akikagua ujenzi wamajengo ya ofisi za  Ikulu Chamwino, Dodoma, leo Desemba 8, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua sehemu mbali mbali wakati akikagua ujenzi wamajengo ya ofisi za  Ikulu Chamwino, Dodoma, leo Desemba 8, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimia mafundi wa kiraia wakati akikagua ujenzi wa  majengo yaofisi za  Ikulu Chamwino, Dodoma, leo Desemba 8, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wajenzi wa kijeshi baada ya kukagua  majengo ya ofisi za Ikulu Chamwino, Dodoma, leo Desemba 8, 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia wajenzi wa kijeshi baada ya kukagua  majengo ya ofisi za
Ikulu Chamwino, Dodoma, leo Desemba 8, 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiongea na mmoja wa askari wajenzi walati akikagua  majengo ya ofisi za  Ikulu Chamwino, Dodoma, leo Desemba 8, 2020
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 08 Desemba, 2020 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Ofisi za Ikulu Mkoani Dodoma na kuelezea kuridhishwa na kiwango na kasi ya ujenzi wa majengo ya ofisi hizo unaofanywa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

Ujenzi wa Ofisi hizo ulioanza tarehe 17 Februari, 2020 unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 3 ijayo na unafanywa kwa usanifu na muonekano sawa na Ofisi za Ikulu zilizopo Jijini Dar es Salaam.

Msimamizi wa ujenzi wa ofisi hizo, Luteni Kanali George William Nyisa amemueleza Mhe. Rais Magufuli kuwa ujenzi huo utakamilika kwa wakati uliopangwa.
Akikagua majengo yanayojengwa, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kufurahishwa kwake na uimara wa nguzo na kuta zinazojengwa na amesema ni fahari kubwa kwa Taifa kujenga ofisi yake ya Ikulu kwa kutumia Jeshi badala ya kutumia wakandarasi kutoka nje ya nchi.

Mhe. Rais Magufuli pia amezungumza na Vijana wa JKT wanaoshiriki ujenzi huo ambapo amekumbusha ahadi yake kuwa vijana hao 2,424 wataandikishwa katika JWTZ mara watakapomaliza jukumu la ujenzi wa Ofisi za Ikulu.
Pamoja na kuwapongeza vijana hao, Mhe. Rais Magufuli pia amewapongeza vijana wa kiraia wanaoshiriki katika ujenzi huo ambao ni mafundi, na amewaahidi kuwa atawaangalia mara baada ya kumaliza kazi hiyo.

No comments :

Post a Comment