Wednesday, December 16, 2020

KATIBU MALIASILI NA UTALII AZINDUA MFUMO WA UPANGAJI WA HUDUMA ZA MALAZI KATIKA DARAJA ZA UBORA JIJINI DODOMA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce K. Nzuki
(katikati) akiwa kwenye  picha ya pamoja na Balozi wa Rwanda nchini,
Mhe. Maj Jen. Charles Karamba ( (kushoto) Katibu Mtendaji wa Shirikisho la vyama vya UtaliiTanzania , Richard Rugimbana kabla ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuzungumza na waandishi wa Habari wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfumo wa upangaji wa huduma za malazi katika Daraja za ubora   uliofanyika mapema leo Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce K. Nzuki
akizungumza na waandishi wa habari wakati wa  hafla ya uzinduzi wa
mfumo wa upangaji wa huduma za malazi katika Daraja za ubora
uliofanyika mapema leo Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce K. Nzuki
akizungumza wakati wa wa uzinduzi wa mfumo wa upangaji huduma za
malazi katika Daraja za ubora iliyofanyika leo Jijini Dodoma. Katika
hafla hiyo Dkt, Nzuki amesema mfumo huo utapunguza gharama na muda wa
kufanya kazi ya kuhakiki na kupanga huduma za malazi katika Daraja za
ubora.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce K. Nzuki
akizindua rasmi mfumo wa upangaji huduma za malazi katika Daraja za
ubora iliyofanyika leo Jijini Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Philip Chitaunga akieleza namna
mfumo wa upangaji wa huduma za malazi  unavyofanya kazi wakati wa
hafla ya Uzinduzi wa Mfumo huo uliofanyika mapema leo Jijini Dodoma.
Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii akiwa pamoja
na Katibu Mtendaji wa Shirikisho la vyama vya Utalii Tanzania Richard
Rugimbana (kushoto) na (kulia) Balozi wa Rwanda nchini Tanzania,  Mhe.
Maj Jen. Charles Karamba.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt Loyce K. Nzuki (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfumo wa upangaji wa huduma za malazi katika Daraja za ubora uliofanyika mapema leo Jijini Dodoma.

 

No comments :

Post a Comment