Friday, December 18, 2020

JAJI MKUU JUMA AMEUTAKA UONGOZI WA IJA KUHAKIKISHA WAHITIMU CHUONI KUMUDU MATUMIZI YA TEHAMA

*********************************

Jaji mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma ameutaka uongozi wa chuo cha uongozi wa mahakama lushoto[ IJA ] kuhakikisha wahitimu wanaomaliza chuoni hapo kumudu matumizi ya

tehama pamoja na kutoa mafunzo kwa njia ya mtandao ili kuingia katika kazi ya ushindani.

Ameyasema hayo katika mahafali ya ishirini chuoni  hapo yakiwa yameambatana na maadhimisho ya kilele cha miaka 20 toka kuanzishwa kwa chuo hicho.
Profesa Ibrahimu amesema wanafunzi wanaotokana na chuo hicho lazima wawe wanafunzi wa karne ya 21 na karne ya 21 inaongozwa na wanawake tofauti na karne zilizopita ilikuwa zikiongozwa na wanaume.
Hivyo amewataka wajaribu kuwapandisha wanafunzi wa astashahada na stashahada ili wawe sambamba na mapinduzi makubwa yanayoendelea katika matumizi ya tehama katika huduma mbalimbali.
;wahitimu wenu lazima wafahamu namna kanuni za ufunguaji wa mashauri kwa njia ya elecronic zinazotumika kila siku mahakamani ili wawe wanafahamu namna gani tehama inatumika mahakamani; Alisema Profesa Ibrahimu.
Nae  Mwenyekiti wa baraza la uongozi wa wa chuo  Dkt Gerald Ndika amesema tafiti mbalimbali za wataalamu wa uchumi duniani zinaonyesha kuwa nchi ambazo uchumi wake umekuwa kwa kiasi ni nchi ambazo zimewekeza zaiodi kwenye maarifa na ujuzi.
Amesema chuo kimeendea kufanya vizuri katika technologia ya habari ya mawasiliano tehama kwa kuakisi hilo chuo kimeendelea kutoa mafunzo kwa njia ya mtandao kwa kushirikiana na taasisi nyingine za kimataifa ikiwemo taasisi ya mafunzo na utafiti ya umoja wa mataifa [united nations institute for trainning and research -unitar] iliyopo uswisi.
Pia Dkt Ndika ameeleza kuwa zimekuwepo juhudu zinazofanywa na uongozi wa chuo katika kukarabati majengo yaliyopo ili kukidhi mahitaji na nyezo za ufundishaji na huduma bora kwa wanachuo na wafanyakazi.
;Pamoja na hatua iliyofikiwa na uongozi wa chuo katika ukarabati wa majengo yapo maombi ya kuendeleza kazi hiyo pamoja na kutafuta ufadhili ya kufanikisha malengo mengine ya chuo; Alisema mwenyekiti huyo.
Mkuu wa hicho Dkt,  Paul Kihwelo alisema licha ya mafanikio yaliyopo chuoni hapo katika ngazi ya stashahada na astashahada chuo kimeendelea kutekeleza kwa vitendo malengo ya kuanzishwa kwake kwa kutoa mafunzo elekezi kwa watumishi wa mahakama ngazi mbal;imbali ikiwemo majaji wa mahakama kuu na mahakama ya rufani lakini pia mahakimu wapya.
Dkt Kihwelo amebainisha kwamba katika miaka ya hivi karibuni chuo kimejihimalisha katika kutoa ushauri [consultancy]pamoja na uitafiti sasa chuo kinamiradi kadhaa.

 

No comments :

Post a Comment