Tuesday, December 15, 2020

COSTECH yawajengea uwezo waandishi wa habari kuandika habari za utafiti wa Sayansi.

**************************
Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma.
Tume ya Sayansi na Teknolojia COSTECH imewakutanisha wanahabari na watafiti mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo namna ya tafiti hizo kuwafikia walaji kwa njia rahisi kwa kutumia wanahabari.
Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika Jijini Dodoma Mkurugenzi wa Menejimenti ya maarifa kutoka COSTECH Dkt Philibert Luhunga amesema lengo ni kuona teknolojia ya Sayansi inayobuniwa na watafiti inawafikia wananchi au walaji kwa lugha rahisi.
“Lengo la kuwakutanisha hapa ni tafiti mbalimbali zinazofanywa na hawa watafiti ziwafikie wananchi kiurahisi kwa sababu tafiti hizo zinakuwa katika Lugha ya Sayansi, lakini tafiti hizo zikipelekwa kwa wananchi kwa kutumia wanahabari ni rahisi kueleweka na walaji wa tafiti hizo” amesema Dkt Luhunga.
Amewataka waandishi wa habari kuandika mara kwa mara habari zinazohusu Sayansi hasa tafiti zinazofanywa na wataalamu wetu ili wananchi wanufanike na tafiti zinazofanywa na wataalamu wetu.
Amesema hasa katika kipindi hiki nchi imejipambanua kuwa nchi ya viwanda Teknolojia za ndani ni muhimu sana maendeleo ya Taifa ili kama nchi tufikie azima ya kuwa nchi ya Viwanda.
Amebainisha kuwa tayari wameshafanya semina kama hizo katika Mikoa ya Dar es saalam, Tanga, Mtwara na Unguja na katika maeneo hayo kumeonekana matokeo chanya kwa waandishi kuwa na mwamko mkubwa wa kuripoti na kuandika habari za utafiti mbalimbali.
“Kote ambako tumefanya semina kama hizi kumeonyesha mwamko mkubwa Sana wa kuripoti taarifa za Sayansi na kitafiti zilizosaidia kuokoa maisha ya watu, hasa tafiti za hali ya hewa kwa kanda ya mashariki” amesema.
Aidha amewashauri wananchi kuendelea kufuatilia habari za utafiti wa kisayansi katika nyanja mbalimbali na wasisite kuwasiliana na Mamlaka husika wanapoona mabadiliko ya kisayansi katika maeneo yao.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo cha TARI Makutupora Dkt Cornel Masawe amesema waandishi wa habari ni watu muhimu katika kufanikisha usambaaji wa tafiti za Kisayansi kuwafikia walengwa wa tafiti hizo.
Amesema kwa upande TARI wanavituo kumi na saba (17) nchini nzima ambavyo vinafanya utafiti wa mbegu mbalimbali za mazao na wamekuwa wakizalisha Teknolojia tofauti tofauti za mbegu za kilimo zinazoweza kuwanufaisha wakulima hapa nchini.
Amebainisha kuwa hapo mwanzo walikuwa wakitumia siku ya 88 kutangaza tafiti zao tukio lililokuwa likifanyika mara moja kwa mwaka lakini Sasa wamefungua Ofisi katika kanda zote hapa nchini katika ofisi za maonyesho ya 88 na vituo hivyo vitakuwa wazi wa siku zote ili kuwahudumia wakulima.

 

No comments :

Post a Comment