Friday, November 13, 2020

Eneo la Kuruka na kutua Ndege Ziwa Manyara na kwingine kujengwa kwa kiwango cha Lami

Na John Walter-Manyara

Rais Dr. John Pombe  Magufuli leo Novemba 12,2020 akihutubia wakati wa ufunguzi wa Bunge la 12 Jijini Dodoma, amesema katika kipindi cha miaka mitano katika usafiri wa anga, kutajengwa kiwanja Kikubwa  kipya cha Msalato, kufanya upanuzi na ukarabati wa Viwanja kumi na moja (11) vikiwemo vya Kigoma, Shinyanga,Sumbawanga, Tabora, Mtwara, Songea.
Pamoja na hayo ameeleza kuwa kutajengwa viwanja vya kutua na kuruka ndege kwa kiwango cha lami kwenye Viwanja vya Iringa, Lake Manyara, Tanga, Musoma, Lindi, Kilwa Masoko, Njombe,Singida,Simiyu na kadhalika.
Mbali na hayo, Rais Dr. John Pombe  Magufuli  amesema atanunua Ndege mpya tano,  moja ikiwa ni ya mizigo.
Aidha Dr. Magufuli amesema kuwa Mwaka huu wametunga sheria mpya ya kusimamia na kuendeleza uvuvi wa bahari kuu  ambapo wamepanga kununua meli nane za uvuvi kwa kushirikiana na shirika la IFAD, meli hizo nane, Nne zitakuwa upande wa Zanzibar na Nne zitakuwa upande wa Tanzania Bara ambazo  meli hizo zitashiriki katika uvuvi wa bahari kuu huku wakikusudia kujenga bandari kubwa ya uvuvi itakayotoa ajira elfu 30.
Katika  Dr. Magufuli amesema ili kuvutia Uwekezaji, kwenye Sekta ya viwanda wataendelea  kuboresha mazingira ya Biashara na uwekezaji ikiwemo kuangalia masuala ya kodi na kuondoa vikwazo na urasimu ambapo kumekuwepo na Urasimu mwingi na kusumbuliwa kwa wawekezaji kwa kuzungushwa hali inayowafanya wakate tamaa.
Amesema anataka mwekezaji mwenye fedha akija apate kibali ndani ya muda wa siku kumi na nne (14),  na kwa sababu hiyo  ameamua suala la uwekezaji ikiwa ni pamoja na kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) kulihamishia kutoka ofisi ya waziri mkuu kwenda ofisi ya Rais ili wanaokwamisha akapambane nao yeye mwenyewe.
Rais John Pombe Magufuli anaendelea kuongoza nchi ya Tanzania katika awamu ya pili na ya mwisho ambapo awali aliingia madarakani  mwaka 2015 akiwa na kaumbi mbiu “HAPA KAZI TU” na sasa mwaka 2020-2025  akiongozwa na Kauli mbiu  ya “ACHA KAZI IENDELEE

 

No comments :

Post a Comment