Friday, October 9, 2020

WAKANDARASI MIRADI YA MAJI WATAKIWA KUFANYA KAZI SAA 24



Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba (kulia anayeandika) akikagua moja ya kazi inayofanywa na mkandarasi kampuni ya Musons Engeneers Ltd inayotekeleza mradi wa maji mjini Chato. Mhandisi Kemikimba akikagua kazi zilizofanyika katika mradi amewataka wakandarasi kufanya kazi kwa saa 24 ili wananchi na taasisi za umma ikiwemo shule na hospitali zipate maji ya kutosha kwa shughuli mbalimbali za maendeleo


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba (kulia) akiangalia mtambo wa kusukuma maji katika chanzo cha maji cha Rubambagwe ambacho kimefanyiwa maboresho ili kuimarisha huduma ya maji kwa wananchi wa Chato. 

Mhandisi Jackson Kyelekule kutoka kampuni ya Musons Engeneers Ltd akionyesha hatua zilizofanyika katika ujeni wa tanki la kuhifadhi maji, ujenzi huo unaendelea na utakamilika mwezi Novemba hivyo kuimarisha hali ya upatikanaji maji kwa wananchi .

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba pamoja na ujumbe wake, akiwa katika kikao kilichojadili hali ya huduma ya maji kwa wananchi na namna yakutatua changamoto katika Mamlaka ya Maji Muleba (MLUWASA) . Wa pili kulia ni Meneja Ufundi wa Mamlaka ya Maji Muleba (MLUWASA) Pontian Thomas.

 

No comments :

Post a Comment