Monday, October 5, 2020

MKUU WA MKOA DAR, VIONGOZI WA DINI WATEMBELEA MRADI WA TANKI LA MAJI WA DAWASA


 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge, Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Daniel G. Chongolo pamoja na viongozi wa Dini wakiwasili kwenye mradi wa maji wakiongozwa na  Meneja wa miradi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Valentina Njau walipofika kutembelea mradi wa tanki la maji na sehemu ya kuzsambazia maji katika mkoa wa Dar es Salaam wakati wa ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ya Mkoa huo.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge, Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Daniel G. Chongolo pamoja na viongozi wa Dini wakitembela mradi wa Maji unaotekelezwa na DAWASA
Meneja wa miradi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Valentina Njau akitolea ufafanuzi kuhusu mradi wa ujenzi wa Tanki la maji na sehemu ya kusambazia maji uliopo Makongo Juu wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge pamoja na viongozi wa Dini waliokuwa wanatembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ya Mkoa wa Dar es Salaam 
Meneja wa miradi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Valentina Njau akiwaonesha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge pamoja na viongozi wa Dini namna mradi huo ulipofikia kwenye mchoro ili kuweza kuongeza ufanisi kwenye usambazaji wa maji katika mkoa wa Dar es Salaam wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge pamoja na viongozi wa Dini waliokuwa wanatembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ya Mkoa wa Dar es Salaam 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge akiwapongeza DAWASA kwa kuweza kutekeleza mradi huo utakaoweza kuongeza nguvu ya usambazaji wa maji katika mkoa wa Dar es Salaam na kuwaondiolea hadha ya upatikanaji wa maji kwa wakazi wa jiji wakati wa ziara yake pamoja na viongozi wa Dini  wa jijini Dar es Salaam waliokuwa wanatembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ya jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge akitoa mjumuhisho  kuhusu mradi wa  usambazaji wa Maji katika jiji la Dar es Salaama unaotekelezwa na  Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)  kwa viongozi wa Dini  wa jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembembelea mradi huo uliopo Makongo Juu Jijini Dar es Salaam leo.

Baadhi ya mitambo za kusukumia maji iliyopo kwenye mradi wa Makongo Juu

 

No comments :

Post a Comment