Monday, October 12, 2020

Maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani yafanyika Njombe ,


 
Wananchi wakipata maelezo ya ufugaji bora wa samaki kutoka kwa Afisa Uvuvi Mwandamizi, Nelson Mbawala wakati wakitembelea mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya Maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mjimwema kitaifa mkoani Njombe tarehe 10-16, Oktoba 2020.
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC)  Dkt. Elifatio towo (Kulia) akifafanua jambo kwa Mgeni rasmi kwenye Uzinduzi wa Maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Chakula duniani Waziri wa Kilimo, Omary Mgumba (kushoto) muda mfupi baada ya kufika kwenye banda la taasisi hiyo leo (10.10.2020).  Katikati ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt.Rashid Tamatamah.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt.Rashid Tamatamah akiwasilisha taarifa ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo (10.10.2020) kwenye uzinduzi wa Maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Chakula Duniani uliofanyika Mkoani Njombe.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt.Rashid Tamatamah (kulia) akifafanua jambo kwenye banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi baada ya  Mgeni rasmi kwenye  uzinduzi  wa Maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Chakula duniani ambaye pia Naibu Waziri wa Kilimo, Omary Mgumba (kushoto) kufika katika banda hilo leo (10.10.2020)

 

No comments :

Post a Comment