Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akimsikiliza
Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Donald Wright alipokuwa akizungumza
masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani, jijini
Dodoma, leo. Simbachawene amemhakikishia balozi huyo kuwa, Tanzania ipo
salama na itaendelea kuwa salama kwa raia wake na wageni mbalimbali
waliopo na wanaoingia nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto) akizungumza na
Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Donald Wright, wakati alipomtembnelea
ofisini, Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma, leo. Simbachawene
amemhakikishia Balozi huyo kuwa, Tanzania ipo salama na itaendelea kuwa
salama kwa raia wake na wageni mbalimbali waliopo na wanaoingia nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
George Simbachawene (kushoto) akimuaga Balozi wa Marekani Nchini, Dkt.
Donald Wright, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika, Mji wa Serikali,
Mtumba, jijini Dodoma, leo. Simbachawene amemhakikishia Balozi huyo
kuwa, Tanzania ipo salama na itaendelea kuwa salama kwa raia wake na
wageni mbalimbali waliopo na wanaoingia nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
George Simbachawene (wapili kushoto), Balozi wa Marekani Nchini, Dkt.
Donald Wright (katikati), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya
kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika, jijini Dodoma. Simbachawene
amemhakikishia Balozi huyo kuwa, Tanzania ipo salama na itaendelea kuwa
salama kwa raia wake na wageni mbalimbali waliopo na wanaoingia nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
******************************
Na Mwandishi Wetu MOHA-Dodoma
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
George Simbachawene ameihakikishia Marekani kuwa, Tanzania ipo salama na
itaendelea kuwa salama kwa raia wake na wageni mbalimbali waliopo na
wanaoingia nchini.
Akizungumza na Balozi mpya wa
Marekani Nchini, Dkt Donald Wright, ofisini kwa Waziri huyo, Mji wa
Serikali Mtumba, jijini Dodoma, leo, Simbachawene amesema usalama wa
nchi upo juu na kwamba tumefanya vizuri katika kutambulisha wageni
katika maeneo ya uwekezaji na utalii.
“Mheshimiwa Balozi nikuhakikishie
tu, nchi yetu ipo salama sasa kuliko wakati mwingine wowote, na
hatujawahi kuwa na kesi za ajabu, hii kutokana na uimara wa Serikali ya
Rais Magufuli ambayo ipo wazi na imefanikiwa kudhibiti rushwa,” alisema
Simbachawene.
Pia Waziri Simbachawene alisema
Serikali inaendelea kudhibiti biashara haramu ya binadamu ambapo mpaka
sasa imeweza kuwarudisha Wasomali 1,300,000 wanaopita nchini kwenda
Afrika Kusini.
“Mafanikio haya ya kudhibiti
biashara hii haramu ya binadamu ni kutokana na kuwepo kwa sheria ya
mwaka 2008 na kanuni zake ambapo imeweza kutusaidia kudhibiti biashara
hii kwa kutumia sheria za nchi,” alisema Simbachawene.
Aliongeza kuwa, mipaka ya nchi ipo
imara na Serikali inaendelea kuimarisha zaidi ambapo imeweza kudhibiti
watu wanaoingia na kutoka katika mipaka mbalimbali nchini.
Kwa upande wake Balozi Dkt. Wright
aliipongeza Tanzania inavyoshughulikia biashara haramu ya binadamu na
alikiri hajawahi kukutana na kesi za ajabu zinazohusiana na biashara
hiyo.
“Watanzania watu wakarimu,
wastaarabu na wenye furaha wakati wote, hivyo nafurahi kuwa Tanzania
kama Balozi wa Nchi hii, na Marekani itaendelea kushirikiana na Tanzania
katika masuala mbalimbali” alisema Balozi Dkt. Wright.
Pia Waziri Simbachawene
alimuhakikishia Balozi huyo kuwa, Serikali itaendelea kushirikiana na
Marekani katika maeneo ambayo yana maslahi kwa Tanzania na Marekani.
No comments :
Post a Comment