Saturday, September 5, 2020

Fahamu kuhusu umuhimu wa kujipanga kustaafu mapema

Black Seniors at the End of Life - SocialWorker.com

Mstaafu mtarajiwa akiwa na mwenzi wake wakitafakari juu ya maandalizi ya kustaafu.(Na Mpigapicha Wetu)

Na Christian Gaya, Majira Ijumaa 04 Septemba 2020


Kustaafu huhitaji wa muda wa kupumnzika, kuburudika na kula matunda na ya nguvukazi yako ulipokuwa mtumishi kwa miaka yote. Ni wakati mdau kukaa na kutulia kwenye...
nyumba yake aliyokuwa amejenga kijijini kwake au mjini, kutembelea mbuga za wanyama au sehemu nyingine yoyote ile, ni wakati wa kucheza na wajukuu wake.
Baada ya hapo unatakiwa kurudi kwenye ndoto yako ya kipaji chako ulichopewa na Mwenyezi Mungu ulichotaka mara kwa mara kukifanyia kazi, ambapo ulipoajiriwa ulikuwa unashindwa kwa sababu huenda muda mwingi ulikuwa unamtumikia mwajiri wako.
Kwa aina ya maisha yeyote utakayochagua kuishi baada ya kustaafu, kitu muhimu ambacho ni kukumbuka sana kutodhubutu kufanya yaani mtindo wa mkono kinywani bila kujishughulisha na kazi yeyote ya kukuongezea kipato.

Kupanga kujiandaa mapema kwa ajili ya kustaafu, unatakiwa uwe muda wa kukaa chini na kuburudika, ni muda unaotakiwa kutokuwa na aina ya msongo wa mawazo ya aina yoyote yale, kumbuka ya kuwa utakuwa ni wakati ambapo hutakuwa tayari kufanya kitu chochote kama una madeni yanayokusubiri pembeni uyalipe. Hivyo unatakiwa uanze sasa kulipa madeni yako makubwa kabla ya wakati hujaanza kunufaika na malipo ya pensheni yako mara tu baada ya kustaafu.
Unatakiwa kujiwekee muda wa kustaafu mapema, ikiwezekana kabla ya kufika tayari muda wa kuachia ngazi ya kazi yako kwa mwajiri wako akilini, kwa maana ya mwaka na hasa wakati wowote ambapo bado una nguvu zako za kutosha za kuweza kujiandaa mapema kwa ajili ya kustaafu na si kusubiri mpaka mwaka wa kustaafu kwako utakapofika au kukaribia hodi.
Hivyo wakati huo sekta rasmi au sekta isiyo kuwa rasmi itakuwa ndiyo njia ya maamuzi yako kuingia huko kuendelea na shughuli zako baada ya kustaafu kama bado hali ya afya yako itakuruhusu kufanya hivyo, lakini pamoja na kutegemea kujiunga na sekta isiyo rasmi itategemea na fursa ulizonazo, pamoja na baadhi ya raslimali ikiwemo na akiba yako ya fedha ulizonazo.
Kumbuka ya kuwa mapato ya mtu mara nyingi hupungua hasa pale baada ya kustaafu labda mtu awe na biashara ambayo haimshirikishi yeye na biashara yenyewe iwe labda na mapato makubwa. Kwa sababu hata njia nyingi za vyanzo vya mapato wakati mwingine hupungua kama vile mikopo mbalimbali ambayo hutumia mshahara wako kuwa ndiyo dhamana ya kupatiwa mikopo hiyo. Ingawa kuna baadhi ya mabenki hutumia pensheni za wastaafu za kila mwezi kama dhamana ya kuwakopesha baadhi ya wastaafu.
Kwa bahati mbaya sana, huwezi ukaamini ya kuwa utafiti unaonesha ya kuwa karibu asilimia themanini (80%) ya nguvukazi ya Afrika Mashariki siyo wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii. Kwa hapa Tanzania ni asilimia 6 tu ya nguvukazi ndiyo wanalio katika mifuko ya hifadhi ya jamii, wakati kwa Kenya ni asilimia 20 ya nguvukazi na Uganda ambapo ni sawa na asilimia 16 tu ya nguvukazi ndiyo wanaohudumiwa na mifuko ya jamii tu.
Kwa hiyo ina maana ya kwamba itakapofikia mwaka wa kustaafu kundi hili halitaweza kujitegemea lenyewe pamoja ya kuwa karibu miaka yote wamekuwa wakifanya kazi. Na kama hutaki kuingia katika kundi hili, hebu jaribu kufahamu mambo muhimu yanayoweza kukusaidia kujiandaa kustaafu bila hofu yeyote ile.
Kama uko kwenye umri wa miaka 20 au mapema ukiwa na umri wa miaka 30 kustaafu kwako kunaonekana ni mbali sana kuanzia umri huo, lakini kumbe ndiyo muda mzuri wa kuanza kuweka akiba yako kwa ajili ya kustaafu baadaye. Pamoja na hayo yote ni kwamba kwa sasa una majukumu machache ukilinganisha na mtu ambaye yupo kazini muda mrefu na anakaribia huenda kustaafu.
Kwa sasa unatakiwa kujiunga na Mfuko Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kama umeajiriwa kwenye sekta rasmi au umejiajiri mwenyewe kwenye sekta isiyorasmi, na kama ni mtumishi wa umma basi jiunge na Mfuko wa hifadhi ya jamii kwa ajili ya watumishi wa umma (PSSSF) pamoja na kujiunga na Mfuko wa hifadhi ya jamii wa Zanzibar ZSSF
Jiunge haraka iwezekanavyo ili uweze kunufaika na mafao ya muda mrefu kama vile pensheni ya kustaafu, pensheni ya ulemavu, pensheni ya urithi, na mafao ya muda mfupi ni kama vile mafao ya uzazi, mafao ya kuumia kazini, mafao ya matibabu na mafao ya msaada wa mazishi.
Mifuko pia hutoa amana ya mikopo ya nyumba ya makazi wakati huo huo unapoelendelea na kazi. Hivyo usipoteza miaka yako ya faida na mapato yanayovutia yapotee bure bila kuweka akiba na kuwekeza.
Kampuni nyingi za bima hazitoi bima za afya kwa ajili ya watu waliofikia umri mkubwa zaidi kulingana na taratibu na miongozo ya bima. Na hata wakitoa hiyo bima ya afya kwa mzee zaidi inaweza kuwa na tozo kubwa mno. Kumbuka kwa sasa tuna mifuko ya hifadhi ya jamii inayotoa mafao ya matibabu kama vile NSSF na Mfuko wa taifa wa bima ya afya (NIHF)
Baada ya kustaafu katika kampuni iliyokuwa ukipata bima ya afya na familia yako kwa kukulipia kila mwezi gharama za matibabu, sasa unatakiwa ujiunge na mifuko ya hifadhi ya jamii ili usije ukapata hofu na kuanza kulipa mwenyewe gharama za matibabu kutoka mfukoni mwako na hatimaye kukusababishia mshituko wa moyo.
Tambua ya kuwa kampuni nyingi zinasimamisha huduma ya bima ya afya mara tu baada ya wewe kuacha kazi au kustaafu.
Kwa hali hii kunaweza kukusababishia kuanza kuwa na matumizi makubwa ya fedha, na hivyo kukupelekea kuanza kula akiba yako yote na kukuacha na bila kitu chochote katika maisha yako yote na familia yako. Na ndiyo maana kuna umuhimu mkubwa wa kuanza kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo inatoa mpango mahususi wa bima ya afya yaani fao la matibabu haraka iwezekanavyo.
Wakati upo kwenye mpito wa kutoka kampuni moja na kujiunga na nyingine pengine,  unatakiwa kuwa mwangalifu na makini sana, kwa sababu unaweza kushawishika kutaka kuondoa michango yako ya pensheni. Hapa ukiwa na mategemeo makubwa ya kuwa unakokwenda huko kwa mwajiri mpya utakuwa unapata mshahara mnono na marupurupu mengi. Kinachotakiwa hapa ni kwenda kumwonesha mwajiri wako mpya kadi yako ya uanachama ili aendelee kukuchangia kwenye akaunti yako hiyo hiyo ya zamani ili kutunisha pensheni yako ya baadaye.
Labda uwe umejipanga vizuri sana vinginevyo hiyo michango ya pensheni uliyochukua itaishia kutumika tu bila hata kuwekezwa kwenye vitega uchumi. Na utafiti unaonesha ya kuwa wafanyakazi wengi wanaochukua michango yao kabla ya kuiva kufikia kuwa pensheni hawawekezi katika vitega uchumi kama vile kwenye hatifungani za muda mrefu na za muda mfupi.
Wakati mwingine unapochukua michango ya pensheni kabla ya wakati wake inaishia kukatwa faini kwa kuchukua kabla ya muda wake haujafika na kuanza kulalamika kwamba ni kidogo bila ya kujua ya kuwa huenda hata mahesabu yake hayakufanywa kwa utaratibu na kanuni zinazotakiwa kisheria.

Mwandishi wa Makala hii ni mwanzilishi wa Kituo cha HakiPensheni, mshauri na mtaalamu wa masuala ya pensheni. Kwa maelezo zaidi: gayagmc@yahoo.com unaweza kutembelea hakipensheni website, Simu +255 655 13 13 41, info@hakipensheni.co.tz

No comments :

Post a Comment