Wednesday, September 2, 2020

Wanafunzi Shule ya Msingi Baobab watia fora kwa vipaji

 Wanafunzi wa shule ya awali na msingi ya Baobab iliyoko Mapinga Bagamoyo wakionyesha umahiri wa kucheza nyimbo mbalimbali za asili katika bonanza la aina yake lililofanyika shuleni hapo kwaajili ya kuibua vipaji.
 Wanafunzi wa shule ya awali na msingi ya Baobab iliyoko Mapinga Bagamoyo wakionyesha umahiri wa kucheza nyimbo mbalimbali za asili katika bonanza la aina yake lililofanyika shuleni hapo kwaaajili ya kuibua vipaji. 
Wanafunzi wa shule ya awali na msingi ya Baobab iliyoko Mapinga Bagamoyo wakionyesha mitindo ya mavazi kwenye bonanza lililoandaliwa na shule hiyo kwaajili ya kuibua vipaji vya wanafunzi.

========   ========

WANAFUNZI wa Shule ya Msingi na Awali ya Babobab ya Mapinga Bagamoyo, wametia fora kwenye bonanza ambapo wameonyesha vipaji vya aina mbalimbali.

Katika bonanza hilo lililowashirikisha wanafunzi wa shule ya awali na msingi, wanafunzi hao walionyesha umahiri kwenye kuigiza michezi mbalimbali ikiwemo ile ya maonyesho ya mavazi.

Miongoni mwa vitu vilivyotia fora kwenye bonanza hilo ni mitindo mbalimbali ya mavazi iliyoonyeshwa na wanafunzi hao na namna walivyomudu kuwasilisha sanaa hiyo kwa ubunifu mkubwa.

Mkuu wa shule hiyo, Ireneus Njelekela alisema waliandaa bonanza hilo kwaajili ya kuendeleza vipaji vya wanafunzi hao kwenye fani mbalimbali.

Alisema mbali na masomo ya darasani shule imeona umuhimu wa kuwakutanisha wanafunzi hao kwenye bonanza ili waonyeshe vipaji walivyonavyo kwenye mitindo ya mavazi, muziki wa bongo fleva na maonyesho ya mitindo ya mavazi.

Alisema watakuwa wakiandaa bonanza kama hilo kila miezi mitatu kwaaajili ya kuvumbua vipaji na kuvile kwani vinaweza kukua na kuwanufaisha kwenye maisha yao ya baadaye.

“Mbali na masomo ya darasani tumeona kuna umuhimu wa kubaini vipaji vya wanafunzi na kuvikuza mtoto lazima alelewe katika Nyanja mbalimbali kwasababu mwisho wa siku anawez kuishi kutegemee kipaji chake,” alisema

“Kuna mifano ya wanamuziki wengi ambao wamefanikiwa sana kwenye maisha kutokana na vipaji mbalimbali, mwanafunzi anaweza asifany vizuri sana darasani lakini akawa na kipaji kitakachompa maisha mazuri sana,” alisema

No comments :

Post a Comment