Mratibu
wa Shirika Lisilo la Kiserikali la Paradigm Initiative Afrika, Peter
Mmbando akizungumza na waandishi wa habari na mashirika yasiyo ya
Kiserikali katika mkutano wa kujadili masuala ya habari katika mitandao
ya jamii na internet ,jijini Dar es Salaam.
Mwanasheria
wa Shirika la Organsation for Peace and Consensus Building (OPCB) Ice
Erick akichangia mada katika mkutano namna ya kufuata sheria katika
uhabarishaji wa habari,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji Serengeti Bytes Kennedy Mmari akichangia mada katika mkutano
namna ya kufuata sheria za katika kuhabarisha jamii katika masuala ya
Mitandao
Baadhi ya wadau wakifatilia mada kwa njia ya mtandao
Picha ya pamoja ya waandishi habari na mashirika yasiyo ya kiserikali mara baada ya kumaliizika mkutano kwa njia ya mtandao.
Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
WAANDISHI
wa habari nchini wametakiwa kufuata taratibu za uandishi wa habari
zilizowekwa ili kulinda haki za wananchi kupata taarifa hasa katika
matumizi ya mitandao ya jamii pamoja na Internet .
Akizungumza
na waandishi wa habari katika mkutano uliokutanisha wadau kuangalia na
kujadiliana namna ya sheria ya mtandao kwa Tanzania jijini Dar es
Salaam Mratibu wa Shirika Lisilo la Kiserikali la Paradigm Initiative
Afrika, Peter Mmbando amesema kuwa uhuru wa vyombo vya habari na
sheria katika matumizi ya mitandao na internet ni kuangalia namna ya
kusaidia kuboresha ufanisi, bora ya upashanaji wa habari na kufuata
taratibu zilizowekwa katika kupasha habari jamii zenye kuzingatia
ukweli na uhakika.
“Rai
kwa Wanahabari kufuata taratibu ambazo zimewekwa na mamlaka husika ili
kulinda haki za wananchi katika kuwapasha habari,Habari zinatakiwa
ziwe za kweli hazitakiwi ziwe za kutengeneza kwani mtu anapodanganya
jamii kwa sauti/video anaharibu taratibu uliowekwa kisheria.”Amesema.
Aidha
aliyaonya makundi ambayo hayajasomea mambo ya habari, wanatakiwa kuacha
kutoa taarifa ambazo hazina ukweli na kupotosha umma ni kuharibu
utaratibu za mamlaka.
Kwa
upande wake Ice Erick kutoka shirika masuala ya umoja, Amani na
maendeleo(OPCB), alisema kupitia mkutano huo wamejifunz amambo mengi
yanayo husu matumizi sahihi ya mitandao na kuongeza kuwa changamoto za
matumizi ya kimtandao ni jukumu lao kuhakikisha watu ambao wanaweza
kupata maafa kutokana na matumizi yasiyosahihi.
“Nadhani
katika matumizi ya mtandao ni kuna umhimu wa kuchukua hatua nzuri kwa
sasa kuiga mfano kwa nchi zingine kama jambo litakuwa na matokeo mazuri
kutoka nchi zingine kuweza kulinda uhuru wa matumizi ya
mtandao.”Amesema.
Hata
hivyo mmoja wa mshiriki wa mkutano huo, Kenedy Mmari alisema majadiliano
hayo muhimu hasa katika kushirikisha wadau katika michakato mbalimbali
ya uundaji wa sera na sharia inayosimamia sekta mbalimbali ikiwemo
mawasiliano ya kimtandao na vyombo vya habari.
“Katika
miaka ya hivi karibuni sheria nyingi zenye mlengo mzuri zinazingatia
habari sahihi mtandaoni, usimamizi mzuri wa mtandaoni lakini sababau za
msingi kunapokuwa hakuna msimamizi wa habari za ukweli inaleta
athari.”Alisema.
No comments :
Post a Comment