Waziri wa Madini Dotto Biteko aipongeza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti
wa Madini Tanzania (GST) juu ya tafiti za jiosayansi inazofanya katika
sekta ya Madini.
Waziri Biteko ametoa pongezi hizo alipofika katika Banda la GST lililopo katika maonesho ya Tatu ya Tekinolojia na Uwekezaji katika sekta ya Madini yanayoendelea mkoani Geita.
Waziri Biteko ametoa pongezi hizo alipofika katika Banda la GST lililopo katika maonesho ya Tatu ya Tekinolojia na Uwekezaji katika sekta ya Madini yanayoendelea mkoani Geita.
Akiwa katika Banda la GST na Mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel
waziri Biteko alisema kuwa Serikali inatambua mchango wa sekta ya Madini
nchini na kushauri kuwa bidhaa za sekta ya Madini zinazozalishwa
nchini ziuzwe ili kufuata utaratibu wa Mpango ushirikishwaji kwa Wazawa
katika sekta ya Madini nchini.
Katika maonesho haya GST kupitia Idara zake imemuonesha na kumuueleza
mafanikio mbalimbali ikiwapo vyungu maalum vya kuyeyushia dhahabu na
akapendekeza ufanyike utaratibu wa kuuza vyungu hivyo katika mgodi wa
dhahabu wa STAMIGOLD
No comments :
Post a Comment